Elections 2015 Wanawake wanaweza, Dr. Asha-Rose Migiro lini uliweza?

heheheh....Ban KiMoon hajui mbeleko akambwaga. Cha ajabu ccm wakampokea kama shujaa.

Hata kumuaga akielekea huko alikotemwa, walimtoa hivyo hivyo kwa ngoma, nakumbuka ilikuwa mshikemshike
 
Hata kumuaga akielekea huko alikotemwa, walimtoa hivyo hivyo kwa ngoma, nakumbuka ilikuwa mshikemshike

Nasikia ile nafasi haikuwa ya Migiro...Ban alimtaka Balozi Mhiga na John Salaita alikuwa pale chuo cha diplomasia kama mwalimu. Na sasa yuko UN security Council kama consultant.

Lakini kwa sababu tz huwa hawaangalii merit, wakampeleka Migiro.
 
Nasikia ile nafasi haikuwa ya Migiro...Ban alimtaka Balozi Mhiga na John Salaita alikuwa pale chuo cha diplomasia kama mwalimu. Na sasa yuko UN security Council kama consultant.

Lakini kwa sababu tz huwa hawaangalii merit, wakampeleka Migiro.

Natambua sana usomi wao, Asha Rose Mtengeti Migiro na ndugu zake wamepata nafasi nyingi za uteuzi serikalini. Inasemekana familia ya JK na familia ya kina Asha Rose ni marafiki wa muda mrefu. Mdogo wake Asha Rose (Radhia Mtengeti Msuya) kwa sasa ni balozi wa Tanzania Afrika kusini. Dada yake Asha Rose (Mwatum Mtengeti Malale) amekuwa katika nafasi nyingi zikiwemo ukatibu mkuu wizara kadhaa na kuna wakati yeye Mwatum akiwa katibu mkuu Asha Rose alikuwa waziri wizara hiyo hiyo moja. Ilibidi mmoja ahamishwe. Kwa sasa Mwatum Malale ni Chancellor wa Muslim University of Morogoro. So Asha Rose na ndugu zake wabahatika sana kushika nyadhifa mbalimbali serikalini ila na mahusiano ya urafiki wa kifamilia na akina JK pia yapo. Inawezekana kuwa urafiki ume influence baadhi ya teuzi
 
Kwa kauli hiyo Lowasa hajichomoi kwenye tuhuma za ufisasi bali anataja alioahirikiana nao kuiba.
 
Nimesoma paragraph chache tu na kugundua kuwa mwandishi wa hilo gazeti la Mawio ni mtu ambaye aidha ameandika ya kichwani mwake au ana ghushi habari.

Asha Rose Migiro hajazaliwa Songea bali zupare, jina lake mabla ya kuolewa ni Asha Mtengeti.
Migiro ni jina la mume wake msomi wa chemistry kwa kiwango cha juu.

Pole mwanzisha mada kwa kuquote madudu.
 
Tanzania tunapaswa kupongeza; kama tunapata mtu anakwenda kutuwakilisha katika Mataifa hiyo ni sifa yetu Watanzania, hata kama tunatofautiana mitazamo kwa maana ya Sera yaani Vyama hii haiondoi Utanzania wetu. Tunakua kama ule ushabiki wa hovyo wa Simba na Yanga akija mgeni kucheza na mmoja wapo mwingine anakua mwenyeji wa mgeni na kumpa mbinu za kumhujumu nduguyo hii siyo sawa.

Lakini kubwa Uongozi ni Majaliwa yake Mola anampa amtakaye, siyo kila mtu anakwenda katika mapambano, wengine huambiwa tu njoo utuongoze au wameumbwa kua Viongozi kama Asha Migiro, huyu ni mwanamke wa kupigiwa mfano si wa kubeza. sasa ndiyo kathubutu hakuwahi kugombea Ubunge amejipima kaona anafaa kua Rais, na huenda akawa Mgombea mwenza katika kinyanga'nyiro hiki.

Madai kwamba aliondolewa katika Unaibu Katibu Mkuu kwa kutomudu majukumu yake siyo kweli, mara nyingi mara nyingi Wazungu hua wanapiga Vita sana Watu kutoka katika nchi zetu hizi za Ulimwengu wa tatu hasa hizi za Kijamaa, kumbuka Salim Ahmed Salim alipigiwa kura ya Veto na US asiwe Katibu Mkuu wa UN sote tunajua sababu zake.

Siyo kweli kwamba anabebwa na Ukaribu wake na Kikwete huyu kaanza kuhudumu Serikalini tangu awamu ya tatu, tusiwakatishe tamaa Wanawake bila kujali Vyama wanavyotoka.
 
Tz sarakasi kila kukicha,, nchi ya maigizo.. kiukweli mtoa mada Uko sahihi,,, watu wengi wenye nyadhifa katika taifa Hili huwa ni mbeleko na sio uwezo na hili utaliona kwa kuangalia utendaji wa wale ambao hawana mbeleko mfano mwakyembe, magufuli,lissu,zzk,mwigulu,msigwa,nk... Mbeleko ndizo zimetufikisha hapa,, tubadilike tuanze safari mpya.
 

Hivi ni sijui ama naota? Huko vyuo vikuu kuna pesa kama kwenye siasa? Kila munu anapenda mkwaja mkubwa
 
huyu fisadi anatumia sana wanawake eti tunaweza kumbe sifuri yuko tena yule fisadi mwingine alikua ardhi nae hivyohivyo watanzania tukaambulia matusi ya ela ya mboga hawa wanawake ni hatari sana.
 

Eeeh bwana kaka umeelezea vizuri sana hapa. Inaleta ladha hata kuisoma maana umelenga point. Mtu akisikia Tanzania spika wa bunge ni mwanamke basi wanajua Tanzania ni noumah
 
Mtusiasa unanikumbusha mbali kwel upo sahihi nimefanya kazi na wote uliowataja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…