WANAYANGA TUHAMASISHANE KUJENGA ACADEMY KWENYE KILA MKOA

WANAYANGA TUHAMASISHANE KUJENGA ACADEMY KWENYE KILA MKOA

BENEDICT BONIFACE

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2013
Posts
284
Reaction score
473
Wanayanga wenzangu napenda tushirikishane wazo hili ili kujenga Yanga imara kwa muda wote na kuendeleza soka la Tanzania kwa ujumla. Naumia sana kuona soka letu na timu zetu kongwe haziendelei wakati zina wadau wengi sana wenye uwezo wa kufanya jambo lolote likafanikiwa kwenye timu zao.

Kwa mfano, mimi nilikua na wazo la kuanzishwa kampeni maalum ya wanayanga kujenga academy kwenye kila mkoa ili kupambana na ukosefu wa wachezaji wenye viwango vya kimataifa na kuongeza mapato kwenye club yetu. Kila mkoa wanachama wahamasishwe kujenga academy yao angalau ndani ya miaka mitano wanachama wajidhatiti kwelikweli kujenga academy ya kisasa kwenye mkoa wao. Academy yenye kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya kukuza vipaji vya vijana. Pitch ya kisasa, gym, mabweni na madarasa kwa ajili ya kujifunza elimu ya mpira na elimu ya kawaida. Msiniambie hatuwezi eleza namna tutakavyoweza kufanikisha hili mbona watu binafsi wameweza kwa nini timu kongwe kubwa kama yanga ishindwe? mimi naomba tuamue kubadilika tuamue kuboresha timu yetu, tusikubali kuendelea kuwa wa kawaida kila siku miaka nenda rudi tupo vilevile tuamueni kufanya makubwa tuweke malengo na tuyatimize.
Hakuna linaloshindikana chini ya jua.

YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO
 
Manchester united yenyewe haijafanya hilo England ije kuwa Yanga inayotembeza bakuli khaaa! Mkuu makinika
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Manchester united yenyewe haijafanya hilo England ije kuwa Yanga inayotembeza bakuli khaaa! Mkuu makinika
ndo maana nikasema usiniambie hatuwezi eleza namna ya kufanikisha hili, kama manchester hawajafanya haina maana kama haiwezekani au yanga haiwezi inategemea na maamuzi yenu tu. HAKUNA LISILOWEZEKANA CHINI YA JUA
 
Fikiria kwanza kuwalipa wachezaji mishahara. Upo uchi unafikiria kununua tai.
Tumia ubongo kwa kufikiri.
 
Wanayanga wenzangu napenda tushirikishane wazo hili ili kujenga Yanga imara kwa muda wote na kuendeleza soka la Tanzania kwa ujumla. Naumia sana kuona soka letu na timu zetu kongwe haziendelei wakati zina wadau wengi sana wenye uwezo wa kufanya jambo lolote likafanikiwa kwenye timu zao.

Kwa mfano, mimi nilikua na wazo la kuanzishwa kampeni maalum ya wanayanga kujenga academy kwenye kila mkoa ili kupambana na ukosefu wa wachezaji wenye viwango vya kimataifa na kuongeza mapato kwenye club yetu. Kila mkoa wanachama wahamasishwe kujenga academy yao angalau ndani ya miaka mitano wanachama wajidhatiti kwelikweli kujenga academy ya kisasa kwenye mkoa wao. Academy yenye kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya kukuza vipaji vya vijana. Pitch ya kisasa, gym, mabweni na madarasa kwa ajili ya kujifunza elimu ya mpira na elimu ya kawaida. Msiniambie hatuwezi eleza namna tutakavyoweza kufanikisha hili mbona watu binafsi wameweza kwa nini timu kongwe kubwa kama yanga ishindwe? mimi naomba tuamue kubadilika tuamue kuboresha timu yetu, tusikubali kuendelea kuwa wa kawaida kila siku miaka nenda rudi tupo vilevile tuamueni kufanya makubwa tuweke malengo na tuyatimize.
Hakuna linaloshindikana chini ya jua.

YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO
Wazo zuri Sana mkuu tatizo viongozi wa kusimamia ndio tatizo na pia mwamko wa wa mashabiki nao sio mzuri.
 
ni wazo zuri mkuu ila naona watafute kwanza mdhamin wa kuaminka ambae atafadhili hilo kinyume na hapo inakuwa ngumu.
 
Back
Top Bottom