Wanazuoni, Lugha za Ulaya na za Afrika: Baina ya Utumwa na Uwezeshwaji (Intellectuals, European and

Wanazuoni, Lugha za Ulaya na za Afrika: Baina ya Utumwa na Uwezeshwaji (Intellectuals, European and

Mabulangati

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2010
Posts
796
Reaction score
167
MAHAFALI YA 43 NA SHAHADA YA JUU YA HESHIMA
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Mwalimu Julius Nyerere Mlimani kinapenda kuwataarifu wadau wa Chuo na umma kwa ujumla kuwa kinafanya Mahafali ya Arobaini na Tatu (43) mwezi Novemba 2013. Mahafali haya yamegawanyika katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni la kutunuku Shahada za Uzamivu, Umahiri, na Stashahada za Uzamili, pamoja na shahada za awali kwa wahitimu wa Chuo cha Fani na Sayansi Jamii. Kundi hili lilifanya mahafali yake tarehe 16 Novemba 2013. Kundi la pili litakalofanya mahafali tarehe 23 Novemba 2013 litawahusu wahitimu wa shahada za awali zilizobakia, yaani kutoka Chuo cha Uhandisi na Taknolojia, Chuo cha Sayansi Asilia na Tumizi, Chuo cha Habari na Teknolojia za Mawasiliano, Shule Kuu ya Elimu, Shule Kuu ya Masomo ya Biashara, Shule Kuu ya Sheria, Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiano ya Umma, na Taasisi ya Taaluma za Kiswahili. Mwaka huu kumekuwa na ongezeko kubwa la wahitimu wa shahada za Uzamili (postgraduate studies) kama ifuatavyo. Shahada za Uzamivu zimeongezeka toka 28 kwa mwaka 2012 hadi 42 mwaka huu 2013 (ongezeko la asilimia 75), Shahada za Umahiri 671 mwaka 2012 hadi 1,026 mwaka 2013 (ongezeko la asilimia 75), Stashahada za Uzamili 153 mwaka 2012 hadi 167 mwaka 2013 (ongezeko la asilimia 9). Ongezeko hili linaendana na dhamira na sera ya Chuo ya kuongeza udahili wa shahada za uzamili na ongezeko hili litaendelea kukua zaidi kwa miaka ijayo. Hata hivyo, wahitimu wa Shahada za awali walikuwa 4,362 mwaka 2012, mwaka huu 2013 wapo 4,209. Tukiangalia uwiano wa jinsia kati ya wahitimu wetu, wanawake ni asilimia 35.1 ambayo ni sawa na asilimia 33.6 kwa wahitimu wa shahada za juu. Kutokana na ongezeko hilo, uongozi na wadau wa Chuo wanatafakari uwezekano wa kuwa na mahafali ya wahitimu wa Shahada za uzamili peke yao, tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo wanavyochanganywa na wale wa shahada za awali. Kama ilivyokuwa kwenye mahafali ya 42 tulipowatunuku wahitimu 902 wa shahada za awali wa kilichokuwa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi na Usanifu Majengo (UCLAS), mwaka huu pia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinaendelea kuwatunuku shahada wahitimu waliosalia. Kwa hiyo, mwaka huu tutatunuku jumla ya shahada 282, kati ya hizo, shahada 106 ni za Umahiri na 176 ni shahada za awali. Wanafunzi hawa ni wale waliodahiliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia iliyokuwa UCLAS mwaka 2007. Mpango huu ni mwendelezo wa kutekeleza hukumu ya tarehe 10 Januari 2011 iliyotolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania iliyokubaliana na walalamikaji kuwa wanastahili kutunukiwa tuzo zao na kupatiwa vyeti vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mchanganuo wa wahitimu kwa tuzo kwa mwaka 2013 ukilinganishwa na mwaka 2012 [TABLE="class: MsoNormalTable, width: 494"]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]Na.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Tuzo[/h] [/TD]
[TD="width: 287, colspan: 3"] [h=1] 2013[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1]2012[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 96"] [h=1] wanaume[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]wanawake[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1]Jumla[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]1.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Shahada ya Uzamivu[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 36[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]6[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 42[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 28[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]2.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Shahada ya Umahiri[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 658[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]368[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 1,026[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 671[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]3.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Stashahada ya Umahiri[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 123[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]44[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 167[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 153[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]4.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Shahada ya Awali[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 2,651[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]1,558[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 4,209[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 4,362[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 284, colspan: 2"] [h=1]JUMLA NDOGO[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 3,474[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]1,975[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 5,449[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 5,214[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]5.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Shahada ya Awali, UCLAS[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 156[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]20[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 176[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1]902[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]6.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Shahada ya Umahiri, UCLAS[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 76[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]20[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 96[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1]-[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 41"] [h=1]7.[/h] [/TD]
[TD="width: 242"] [h=1] Stashahada ya Umahiri, UCLAS[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 9[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]1[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 10[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1]-[/h] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 284, colspan: 2"] [h=1]JUMLA KUU[/h] [/TD]
[TD="width: 96"] [h=1] 3,715[/h] [/TD]
[TD="width: 102"] [h=1]2,016[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 5,731[/h] [/TD]
[TD="width: 89"] [h=1] 6,116[/h] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Aidha kwa namna ya pekee katika awamu ya pili ya mahafali haya, Mkuu wa Chuo atamtunuku Shahada ya Hesima ya Udaktari katika Fasihi (honoris causa) msomi, mwanafasihi aliyebobea na mwanaharakati mashuhuri hapa duniani Prof. Ngugi wa Thiong’o. Prof. Ngugi amepokea kwa furaha na shukrani kupata heshima hiyo toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na amekubali kuhudhuria mahafali na kupokea mwenyewe heshima hiyo. Prof. Ngugi anatunukiwa shahada hii kwa sababu ya mchango mkubwa alioutoa na anaoendelea kutoa kwenye fasihi, hasa za Kiafrika. Prof. Ngugi sio tu amekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza fasihi za lugha za kiafrika, bali pia ni mwanamapinduzi halisi anayepinga ukoloni, unafiki na rushwa miongoni mwa wanajamii. Hili limeshuhudiwa katika uandishi wake wa michezo, riwaya na insha mbalimbali ambazo aliziandika si tu katika lugha za Kiingereza na Kiswahili, bali pia katika lugha yake ya asili, Kikuyu. Kwa kudhihirisha hili kabla ya mahafali, Prof. Ngugi atatoa mhadhara maalumu wa uanazuoni kuhusu Wanazuoni, Lugha za Ulaya na za Afrika: Baina ya Utumwa na Uwezeshwaji (Intellectuals, European and Africa Languages: Between Enslavement and Empowerment). Mhadhara huo utafanyika katika Ukumbi wa Nkrumah, Ijumaa tarehe 22 Novemba 2013, kuanzia saa nne hadi saa sita mchana. Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unawakaribisha wadau wote wa elimu kuhudhuria na kushiriki mhadhara huo adimu wa Profesa Ngugi wa Thiong’o siku hiyo ya Ijumaa. Mwisho, tunamhamasisha kila mhitimu kwenda kulitumikia Taifa kwa moyo wote kwa njia ya kujiajiri, kuajiri au kuajiriwa na hatimaye kuwa balozi mwema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Imetolewa na Prof. Rwekaza S. Mukandala Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu ch Dar es Salaam
 

Attachments

Jamani ukipata vizuri kula na wenzio. Hii nimeipata toka kwa jamaa wa Mwananchi aliyehudhuria Press Conference pale UD. Kwakweli lazima nihudhurie hiyo Lecture
 
Back
Top Bottom