Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,501
- 28,711
Kamwene wadau wangu wangu wa JF.
Kuna riwaya moja ipo pale Form Five na Six inaitwa Vuta N'kuvute ebhana ni moja ya love story iliyojaa ufundi mkubwa sana wa sanaa ya uandishi. Kwa wale walosoma HKL, HKL wataelewa ninachosema; nyie mliosoma PCM kuna chand [emoji6]. Hiyo riwaya ukiangalia dhamira ya mapenzi na mahusiano imeguswa kinagaubaga sana, nenda katafute usome halafu umkumbuke mwanadada Wanda Nara.
Ukizunguka pale Ufaransa utakutana na mitaa yenye mataa na mnara mkubwa na mrefu sana pale katikati ya jiji, napo si pengine ni Paris. Kuna chama la wana linaitwa PSG.
Pale PSG Kuna kiumbe mmoja wa kuitwa Mauro Icardi [emoji1544][emoji1544].Yes, huyu ni streika matata sana ambaye amekichafua sehemu nyingi sana.
Ukienda kule Argentina yeye na Paulo Dyabala mitaani kwao wanaheshimika hata zaidi ya Messi na wanaamini wao ndo Messi wao na madogo wengi wanajiita kina Icardi au Dyabala.
Nani asiyeujua uwezo wa Icardi katika kufumania nyavu? Lakini hakuwa na maisha mazuri sana akiwa Inter Milan na hata timu yake ya taifa na mara nyingi skendo yake na Wanda Nara ilitawala sana kuliko hata kipaji chake.
Wanda ni mke wa Icardi kwa sasa lakini alikuwa ni mke wa Maxi Lopez ambaye kipindi wapo Sampdoria ilitokea mwanamama akamuelewa mzee wetu fundi wa mpira Icardi.
Ilitokea msuguano sana na kitu hicho kilimfanya Messi amchukie na akatoa amri kwa kocha asiwe anamjumuisha kwenye timu ya taifa, na hi ilitengeneza bifu kati ya Messi na Icardi.
[emoji1544]Lakini unaambiwa mapenzi ni kikohozi hayawezi kufichika. Mtoto Wanda akamuelewa jamaa, wakadumu mpaka Icardi alivyotoka Sampdoria mpaka safari yake ya PSG mwanadada hakuonesha ajizi ya upendo wake kwa fundi wetu huyu.
Wanda amekuwa mwanamke mwenye upendo sana kwa mume wake na mpaka jamaa akamfanya awe wakala wake .
Wakala na kichuna wa Icardi, Wanda amempambania sana mume wake kutoka pale Inter kwani baada ya jamaa kuporwa kitambaa cha unahodha. Ilisemekana wasingemuuza na wala asingepata nafasi ya kucheza kwani alikuwa hana nidhamu Wala hakujituma akiwa na kikosi cha Inter.
Lakini Wanda kupitia ushosti wake na mke wa mkurugenzi mkuu na rais wa PSG akawaita hotelini, akawaambia shemeji yenu kule analetewa za kuleta embu ongeeni na majamaa tumlete goalgetter huyu chap aje aungane na akina Mbappe na kina Di Maria bila kuwasahau kina Neymar.
Dili lilikaribia kukwama lakini unaambiwa wakati bwana ake anapasha gym, mke wake na wakala wake alikuwa hana hata muda wa kuegesha kichwa, kujibebisha alihakikisha mteja wake anapata timu.
Wakati jamaa akiwa hana hili wala lile, simu iliingia ikimtaka akafanyiwe vipimo tayari kwa kukichafua PSG na ilikuwa ni mida ya lala salama.
[emoji1544] Icardi yupo PSG ndiyo lakini kuna mkono mkubwa sana wa mke wetu Wanda Nara pale. Mwanamke anaepambana kama kina Mino Raiola na akina Pogba wao au akina Mendes na kina Ronaldo waoo[emoji1544][emoji1544][emoji1544].
Licha ya kuwa mapenzi yanatokea na kuanza popote bila kujali utachukuliwa vipi na jamii kikubwa na mapenzi ya dhati, lakini jiulize mke wako anawaza kupambana upate pahala pa kujibanza au naye anasubiri tu upambane ulete nyumbani[emoji1550][emoji1550][emoji1550][emoji1550].
Kuna riwaya moja ipo pale Form Five na Six inaitwa Vuta N'kuvute ebhana ni moja ya love story iliyojaa ufundi mkubwa sana wa sanaa ya uandishi. Kwa wale walosoma HKL, HKL wataelewa ninachosema; nyie mliosoma PCM kuna chand [emoji6]. Hiyo riwaya ukiangalia dhamira ya mapenzi na mahusiano imeguswa kinagaubaga sana, nenda katafute usome halafu umkumbuke mwanadada Wanda Nara.
Ukizunguka pale Ufaransa utakutana na mitaa yenye mataa na mnara mkubwa na mrefu sana pale katikati ya jiji, napo si pengine ni Paris. Kuna chama la wana linaitwa PSG.
Pale PSG Kuna kiumbe mmoja wa kuitwa Mauro Icardi [emoji1544][emoji1544].Yes, huyu ni streika matata sana ambaye amekichafua sehemu nyingi sana.
Ukienda kule Argentina yeye na Paulo Dyabala mitaani kwao wanaheshimika hata zaidi ya Messi na wanaamini wao ndo Messi wao na madogo wengi wanajiita kina Icardi au Dyabala.
Nani asiyeujua uwezo wa Icardi katika kufumania nyavu? Lakini hakuwa na maisha mazuri sana akiwa Inter Milan na hata timu yake ya taifa na mara nyingi skendo yake na Wanda Nara ilitawala sana kuliko hata kipaji chake.
Wanda ni mke wa Icardi kwa sasa lakini alikuwa ni mke wa Maxi Lopez ambaye kipindi wapo Sampdoria ilitokea mwanamama akamuelewa mzee wetu fundi wa mpira Icardi.
Ilitokea msuguano sana na kitu hicho kilimfanya Messi amchukie na akatoa amri kwa kocha asiwe anamjumuisha kwenye timu ya taifa, na hi ilitengeneza bifu kati ya Messi na Icardi.
[emoji1544]Lakini unaambiwa mapenzi ni kikohozi hayawezi kufichika. Mtoto Wanda akamuelewa jamaa, wakadumu mpaka Icardi alivyotoka Sampdoria mpaka safari yake ya PSG mwanadada hakuonesha ajizi ya upendo wake kwa fundi wetu huyu.
Wanda amekuwa mwanamke mwenye upendo sana kwa mume wake na mpaka jamaa akamfanya awe wakala wake .
Wakala na kichuna wa Icardi, Wanda amempambania sana mume wake kutoka pale Inter kwani baada ya jamaa kuporwa kitambaa cha unahodha. Ilisemekana wasingemuuza na wala asingepata nafasi ya kucheza kwani alikuwa hana nidhamu Wala hakujituma akiwa na kikosi cha Inter.
Lakini Wanda kupitia ushosti wake na mke wa mkurugenzi mkuu na rais wa PSG akawaita hotelini, akawaambia shemeji yenu kule analetewa za kuleta embu ongeeni na majamaa tumlete goalgetter huyu chap aje aungane na akina Mbappe na kina Di Maria bila kuwasahau kina Neymar.
Dili lilikaribia kukwama lakini unaambiwa wakati bwana ake anapasha gym, mke wake na wakala wake alikuwa hana hata muda wa kuegesha kichwa, kujibebisha alihakikisha mteja wake anapata timu.
Wakati jamaa akiwa hana hili wala lile, simu iliingia ikimtaka akafanyiwe vipimo tayari kwa kukichafua PSG na ilikuwa ni mida ya lala salama.
[emoji1544] Icardi yupo PSG ndiyo lakini kuna mkono mkubwa sana wa mke wetu Wanda Nara pale. Mwanamke anaepambana kama kina Mino Raiola na akina Pogba wao au akina Mendes na kina Ronaldo waoo[emoji1544][emoji1544][emoji1544].
Licha ya kuwa mapenzi yanatokea na kuanza popote bila kujali utachukuliwa vipi na jamii kikubwa na mapenzi ya dhati, lakini jiulize mke wako anawaza kupambana upate pahala pa kujibanza au naye anasubiri tu upambane ulete nyumbani[emoji1550][emoji1550][emoji1550][emoji1550].