Uchaguzi 2020 Wanne mbaroni tuhuma rushwa kuwania ubunge

Uchaguzi 2020 Wanne mbaroni tuhuma rushwa kuwania ubunge

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Lindi, inawashikilia watu wanne, akiwamo mtia nia wa nafasi ya ubunge, Ally Chinumba (CCM), kwa madai ya kuwashawishi wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Kata wampitishe kwenye kura za maoni.

Naibu Mkuu wa Takukuru mkoani hapa, Charles Mulebya, alitoa taarifa za kukamatwa kwa watuhumiwa hao alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana.

Alisema Chinumba alikamatwa juzi Nahukahuka, Jimbo la Mtama saa 11 jioni alasiri wakati yeye na wajumbe wasiopungua (23) wa Halmashauri ya Kata hiyo, nyumbani kwa Ally Chinumba, ambaye ni baba mzazi wa mtia nia huyo.

Mulebya alisema Chinumba ambaye pia ni mtumishi wa Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco) makao makuu jijini Dar es Salaam, alikutwa akiwa amewakusanya wajumbe hao kwa lengo la kuwashawishi wampitishe kwenye kura za maoni, ili kugombea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge mwaka huu Jimbo la Mtama.

Alisema kwenye gari la mtia nia huyo lenye namba za usajili T.527 DEY (hakutaja aina ya gari) maofisa wa Takukuru walikuta fedha kiasi cha Sh. 841,000 zilizokuwa zimewekwa maeneo tofauti tofauti, zikiwamo bahasha ndogondogo dazani moja zinazohisiwa zimeandaliwa kwa ajili ya kuwekea fedha kwa ajili ya wajumbe husika.

"Gari la mtia nia tulipolipekua, tumekuta fedha Sh. 841,000 na dazani moja ya bahasha ndogo ndogo, bila shaka zilikuwa za kuwekea fedha za wajumbe," alisema.

Alipoulizwa kama wajumbe waliowakuta wanawashikilia, kiongozi huyo wa Takukuru alijibu kuwa wanawashikilia watu wanne akiwamo mtia nia husika, lakini hakuwa tayari kuanika majina ya watuhumiwa wengine watatu.

Alisema Takukuru inaendelea na uchunguzi ili kubaini uvunjifu wa sheria, kwa mgombea huyo kujihusisha na vitendo vya kushawishi wajumbe kwa utaratibu wa kutoa rushwa.
Aliwaonya watia nia wote kwa nafasi mbalimbali zikiwamo za ubunge na udiwani kujihusisha na vitendo vya rushwa, akiwataka wafuate utaratibu, kanuni na sheria zilizowekwa.
 
Hivi bunge lijalo mh Majaliwa atakuwa mbunge wa kawaida anayeongozwa na Spika Makonda
 
Sitetei rushwa lakini Takukuru hawajaweka mazingira ya kukamata rushwa aidha kwa makusudi au kwa uzembe. Sijaona kesi hapo zaidi ya kukurupuka kabla tuhuma haijaiva. Utamshitaki na nini hapo zaidi mwisho wa siku mtamrudishia kila kitu chake.
1.Nani mwenye kuthibitisha 841,000 zilikuwa rushwa?
2.Je ni kosa kubeba bahasha kwenye gari au kuna kiasi kisichoruhusiwa?
3.Je ni kosa kukutana na hao wajumbe? Kwa kifungu kipi cha sheria au TAKUKURU wanafuata kanuni za uchaguzi za CCM?
 
Utashangaa wote watakaokamatwa kwa tuhuma za rushwa ni ccm kwani ni haiba
Halafu mwishowe hao watia nia na wajumbe wapokea rushwa hufutiwa tuhuma na hupitishwa kugombea na kuchagua.Sifa hii ya rushwa huko CCM inaanzia shinani hadi Taifa.
Wengine wamemwaga vitisho/kuzuia wenzao kutia nia/kugombea na kuhakikisha inachapishwa fomu moja pekee,hiyo pia ni aina ya rushwa.
 
Halafu mwishowe hao watia nia na wajumbe wapokea rushwa hufutiwa tuhuma na hupitishwa kugombea na kuchagua.Sifa hii ya rushwa huko CCM inaanzia shinani hadi Taifa.
Wengine wamemwaga vitisho/kuzuia wenzao kutia nia/kugombea na kuhakikisha inachapishwa fomu moja pekee,hiyo pia ni aina ya rushwa.
Hakuna kiongozi wa serikali anayeweza kupambana dhidi ya rushwa. JPM ameshindwa maana watoaji na wapokea rushwa ni chama tawala
 
Sitetei rushwa lakini Takukuru hawajaweka mazingira ya kukamata rushwa aidha kwa makusudi au kwa uzembe. Sijaona kesi hapo zaidi ya kukurupuka kabla tuhuma haijaiva. Utamshitaki na nini hapo zaidi mwisho wa siku mtamrudishia kila kitu chake.
1.Nani mwenye kuthibitisha 841,000 zilikuwa rushwa?
2.Je ni kosa kubeba bahasha kwenye gari au kuna kiasi kisichoruhusiwa?
3.Je ni kosa kukutana na hao wajumbe? Kwa kifungu kipi cha sheria au TAKUKURU wanafuata kanuni za uchaguzi za CCM?
Nami kwa mbali nimefikiria kitu kama hiki mkuu.
 
Sitetei rushwa lakini Takukuru hawajaweka mazingira ya kukamata rushwa aidha kwa makusudi au kwa uzembe. Sijaona kesi hapo zaidi ya kukurupuka kabla tuhuma haijaiva. Utamshitaki na nini hapo zaidi mwisho wa siku mtamrudishia kila kitu chake.
1.Nani mwenye kuthibitisha 841,000 zilikuwa rushwa?
2.Je ni kosa kubeba bahasha kwenye gari au kuna kiasi kisichoruhusiwa?
3.Je ni kosa kukutana na hao wajumbe? Kwa kifungu kipi cha sheria au TAKUKURU wanafuata kanuni za uchaguzi za CCM?
Acha ujuaji wa kijinga.
Wanafunzi mliosomea Sheria SAUTI mko weupe Sana kichwani.
 
Sitetei rushwa lakini Takukuru hawajaweka mazingira ya kukamata rushwa aidha kwa makusudi au kwa uzembe. Sijaona kesi hapo zaidi ya kukurupuka kabla tuhuma haijaiva. Utamshitaki na nini hapo zaidi mwisho wa siku mtamrudishia kila kitu chake.
1.Nani mwenye kuthibitisha 841,000 zilikuwa rushwa?
2.Je ni kosa kubeba bahasha kwenye gari au kuna kiasi kisichoruhusiwa?
3.Je ni kosa kukutana na hao wajumbe? Kwa kifungu kipi cha sheria au TAKUKURU wanafuata kanuni za uchaguzi za CCM?
Afrika ina mambo kiongozi Nia hapo ni kumchafua mgombea kumuwekea njia nyeupe Kaka yngu Mzee wa Goli la mkono...
 
Back
Top Bottom