Wanunuzi wa Almasi na Dhahabu, Tanzania

Mzalendowadamu

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2016
Posts
218
Reaction score
318
Habari wanajukwaa.
Katika pitapita zangu za mihangaiko nimekuwa nikifuatilia namna ya kupata Madini tajwa hapo juu. lengo langu ni kununua toka nje ya nchi kwa wachibaji wadogo kisha kuja kuuza hapa Tanzania au sehemu yoyote penye soko la uhakika na salama. Niliwahi kuwa nauza dhahabu kwa mfumo huu mwaka 2014 lakini kwa sasa ofisi hiyo ilifungwa na sina taarifa za wanunuzi wengine wa uhakika na salama kama ile ofisi.
Kwa sasa napenda kujua hasa wanunuzi wa Almasi ghafi (rough diamonds) kwa hapa Tanzania au nje ya Tanzania. Kwakua sasa nimepata soko la uhakika la kununulia na pia kuna watuwa nje ya nchi ambao nao wanapenda kunitumia kuja kuwauzia mzigo wao hapa Tanzania kwani wao wanaamini na wanasema wanazo taarifa kuwa Tanzania kuna bei nzuri na ni salama sana kwa biashara hii. Hivyo ningependa kupata wanunuzi wenye uhakika ili nijenge imani Kwa watu hawa walio amua kuniamini mtanzania mwenzenu, vilevile nami niweze kuwa na uhakika wa kufanya biashara hii na kujikwamua kiuchumi.
Pia kama kuna mwenye wazo lolote la kushauri au kuchukulia tahadhali basi napenda mnielimishe.
Tafadhali naomba mawazo yote yawe hapa wazi ili na wengine wajifuze kwa lolote. Naheshimu kila mchango wa mtu.
Karibuni sana.
 

Mkuu, unatakiwa uwe na leseni ama ile ya kusafirisha nje ya nchi (Export Licence) au ile ya udalali ndani ya nchi(Broker Licence) au ile ya kibali maalum yaani Special Export permit.

Na wale wenye leseni za udalali yaani Broker Licence hawaruhusiwi kusafirisha nje ya nchi.

Je, ni leseni ipi unayo kati ya hizo?
 
Asante Kwa Taafika. Bado sijawa na Leseni na kulingana na Maelezo yako nafikiria Kupata hiyo ya Dealer(Broker Licence ) Kwanza ili kupata uzoefu kisha hapo baadae nitakata hiyo ya ku Export.
Nahitaji kujenga imani kwa wadau kwanza maana najua kwenda kuuza nje inachukua muda kidogo sasa kwa mwanzo wa biashara watu wanaweza kujawa hofu ya kudhulumiwa so nahitaji kujijenga ndani kwanza ndio maana nahitaji kujua Dealers wa Ndani ya nchi kwanza.
 
Jana kuna msako ulitembea kwa masonara wa Dar. Tena ulifanywa na waziri wa madini dada yetu Kariuki. Sasa sijuwi inaweza kukuathiri vipi ktk hiyo biashara yako unayotaka kufanya.
Inabidi kufuatilia na hilo pia. Unaweza kupoteza mtaji ndani ya sekunde chache.
Fuata taratibu na sheria bila shuruti na jitahidi kuwa mkweli kwani msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
 
Asante kwa taarifa. Nitafuatilia maana sijui huko kwa masonara anataka nini maana hawa huwa ni watu wadogo sana ila pengine wanaweza kuwa wanatumia kivuli cha U sonra kumbe wanachukua mzigo mkubwa na ku export, nitafuatilia hilo, Asante
 
Hizi ndio mada ambazo zinatakiwa ziwe na wachangiaji wengi kwa kuwa zimebeba maarifa mengi ndani yake!!!!...

Naamini mtoa mada umewakilisha mawazo ya walio wengi waliokuwa wanasita kuuliza!!!..
 
wajuzi tujuzane zaid [emoji113][emoji113][emoji113][emoji113][emoji113]
 
Kipindi cha nyuma ulikuwa ukienda machimboni na wanunuzi pia walikuwepo,ingawa usalama kwa muuzaji ulikuwa ni mdogo;sijajua kwa sasa hivi kama ni rahisi wanunuzi kujulikana,labda ujaribu kudeal na hao masonara wanaweza kukupa masoko,ingawa pia wanaweza kukugeuka wakijua una mzigo wa thamani fulani.
 

Mtanzania yoyote anaruhusiwa kufanya biashara ya madini endapo tu anafuata masharti na sheria inasemaje.

Kwanza kabisa ni lazima uwe na leseni yaani dealers licence au Broker licence.

Hawa ndo wanaruhusiwa kununua, kuhodhi, kuuza na hata kuyachengua..

Mwenye leseni ya Broker haruhusiwi kusafirisha madini nje ya nchi.

Mwenye leseni ya uuzaji au Dealer licence ndiye anaruhusiwa kusafirisha madini nje ya nchi kwa kuomba kibali kingine kitwacho Export Licence.

Masharti ya kufuata ili uweze kusafirisha madini na sampuli ya madini nje ya nchi:

1. Kibali cha kusafirisha nje ya nchi au Export permit amabcho kimetoka STAMiCO au wizara ya madini

2. Kibali hicho kinatakiwa kuonyesha:

Jina la mwenye leseni
Namba ya leseni
Aina ya madini na uzito wake
Thamani ya madini hayo
Tarehe iliyotolewa
Muda wa kibali hicho
Jina la alietoa kibali hicho.

3.Stakabadhi ionyeshayo malipo ya mrahaba.

Pia vipo vibali vingine vinavyotolewa kwa ajili ya kusafirisha madini nje ya nchi ambayo yamenunuliwa kwenye maonyesho ya madini Arusha au Gem Trade fair.

Kuna cheti kinachotambulisha madini ya Tanzanite kwamba yametokea Tanzania.

Kuna cheti cha Kimberley Processing ambacho kinatolewa na kamishna wa madini ambacho kinatambulisha dhahabu ya Tanzania.

Na mwisho kuna kibali kwa wageni ambao ama wamenunua madini kutoka kwa mwenye machimbo au dalali wa madini anaetambulika na kibali hicho kinatolewa na kamishna wa madini.

Pia mgeni huyo anatakiwa alipie mrahaba madini hayo na vilevile thamani ya madni hayo isizidi dola 1000.
 
Unaposema thamani ya MADINI kwa mgeni isizidi 1 million unamaanisha nini? Unaweza kuijazia kidogo?
 
Unaposema thamani ya MADINI kwa mgeni isizidi 1 million unamaanisha nini? Unaweza kuijazia kidogo?

Mgeni mwenye viza (asie mtanzania) anaruhusiwa kuondoka na madini yenye thamani isozidi dola 1000 na ada yake analipa dola 200

Mgeni mkaazi ambae ni mtanzania yaani Non-resident wao wanalipia ada ya dola 2000 kwa madini yenye thamani inayozidi dola 1000.

Hiyo ni kwasababu mtanzania aishie nje ya nchi kama ana soko kule Antwerp au Kuala lumpur , basi anaweza kabisa kuingia Arusha na akachukua mzigo wa maana.
 
Nimekusoma MKUU...ila nna maswali kadhaa....
1.Kodi inalipwa wakati gani?
2.Serikali inakataje Kodi Yake...?
@Kulingana na mwongozo wa bei ambao Serikali inao..?
kutoka kwenye Main Value ya mzigo toka kwa Seller...?

2.Kama Mtanzania kapata Mgeni na mwisho wa siku anataka kuondoka na madini yenye thamani zaidi ya $ 1,000.....kuna gharama za kulipia..?
 
Sasa kwa Case yangu, ni kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimepata soko la kununua madini kwa bei nzuri ambapo nikienda kuuzia nyumbani Tz naweza pata faida kidogo. Lengo langu ni kuanza kwa kuwauzia hao ma broker au dealer. Kwakua madini nayatoa nje ya nchi sasa ninatakiwa kuwa na kibali gani?
 

Katika nchi unakotoka lazima utakuwa na Export Licence ya nchi hiyo ambayo ni "valid" na ukifika Tanzania unafanya Declaration kwamba una mzigo wa kiasi gani na unalipia kodi ya kuingiza nchini TZ kulingana na uzito na thamani ya madini hayo.
 

Kodi utalipia ofisi ya kamishna wa madini ambapo utapata kibali cha kusafirisha nje na utaambiwa thamani halisi ya madini na kodi unayotakiwa kulipa kulingana na sheria mpya ya madini

Kuna madawati ya jamaa waitwao TMAA kila kiwanja cha ndege na mipakani ambao ni mawakala wa serikali wenye nguvu kwelikweli ya kukamata madini, kuyapiga mnada na hata kukupekua kama unadanganya kwenye masuala kama uzito na kadhalika.

Huyo muuzaji (Seller) atakuwa amekupatia stakabadhi ambayo inaonyesha malipo halisi, uzito wake na thamani ya madini hayo.
 
Madini yanataka mtu mkweli. Ukiwa mwongo mwongo hutasogea mbele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…