Wanyasa wanauliza Denis Phombeah ni nani katika historia ya uhuru wa Tanganyika ?

Wanyasa wanauliza Denis Phombeah ni nani katika historia ya uhuru wa Tanganyika ?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WANYASA WANAULIZA DENIS PHOMBEAH NI NANI KATIKA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA ?

1566323813664.png


1566323876291.png

Raia Mwema 14 - 20 Agosti, 2019

Raia Mwema la 14 - 20 Agosti limechapa makala ambayo kwanza ilikuwapo hapa Majlis, ''Tulikotoka Kufika SADC Kisa Cha Ally Sykes, Denis Phombeah na Kenneth Kaunda.''

Nia yangu ya kuweka hapa makala ile ilikuwa baada ya kupigiwa simu na kuombwa nishiriki katika kipindi cha Channel Ten Zahir Hotel ambako wajumbe wa SADC wangefika pale na kuniuliza maswali kuhusu historia ya mgahawa huu na wapigania uhuru wa nchi za Kusini.

Kwenye mlango wa kuingia mgahawa huu kuna kibao kinachoeleza kuwa hapo palikuwa sehemu wakikutana wapigania uhuru wakati wa nchi Kusini ya Afrika.

Kipindi hiki nilifahamishwa kitarushwa mubashara.

Ukweli nilimkatalia huyo aliyenipigia simu na sababu kubwa ni kuwa mwaliko wenyewe umenifikia mchana milango ya saa saba hivi na kipindi kinakwenda hewani saa kumi jioni kwa hiyo hapakuwa na muda wa matayarisho.

Mambo kama haya yanahitaji maandalizi hasa ikiwa kipindi ni mubashara kwa kuchukua tahadhari kusema maneno siyo.

Nikamfahamisha hilo ndugu yangu aliyenifikishia mwaliko nikamwambia hawa ni wageni wa serikali wasije wakaniuliza maswali ambayo majibu yake yanapishana na historia rasmi inayofahamika.

Ikawa nimekataa kushiriki katika kipindi kile.

Lakini ikanijia fikra kuwa ninao bado mchango wa kuchangia katika historia ya Tanganyika na SADC.

Ndiyo nikaamua kuweka hapa safari ya mwaka wa 1953 ya Ally Sykes na Denis Phombeah kwenda Lusaka Northern Rhodesia kuhudhuria mkutano wa vyama vya siasa kutoka nchi Kusini ya Sahara ulioitishwa na Kenneth Kaunda akiwa Rais wa ANC ya Northern Rhodesia.

Ndugu zetu Wanyasa baada ya kusoma gazeti la Raia Mwema na kukuta Mnyasa anaiwakilisha Tanganyiaka katika mkutano ule wamepiga simu nyingi Raia Mwema kutaka kujua mchango wao katika uhuru wa Tanganyika.

Kisa hiki hiki kilichosomwa na wengi hapa Majlis kama ningekieleza mbele ya camera za televisheni tena mubashara athari yake kwa watazamaji ingekuwa nyingine kabisa.

Lingeweza kuja swali kwangu, ''Ally Sykes na Denis Phombeah ni nani na iweje hawa wawakilishe Tanganyika kwani Julius Nyerere alikuwa wapi?''

Unajibu vipi mtu maswali kama haya?

Mhariri wa Rais Mwema kakwepa kuliunganisha jina la Ally Sykes, Denis Phombeah na jina la Kenneth Kaunda.

Si bure kwa yeye kuamua kufanya hivi.
Anazo sababu zake.

Picha: Ally Sykes na Denis Phombeah wakiwa Chileka Airport, Blantyre Nyasaland wakiwa njiani kurudi Dar es Salaam.
 
mzee wangu mohamed said itakuwa vyema kama utamuelezea kiundani huyo mnyasa hapa jf.

binafsi nataka sana kumfahamu vizuri na kufahamu uhusika wake katika harakati za kisiasa ndani ya tanganyika.

niwie radhi kwa ombi langu maana siku hizi nimekuwa sivutiwi kusoma magazeti ya hapa nyumbani hususani gazeti la raia mwema.
 
mzee wangu mohamed said itakuwa vyema kama utamuelezea kiundani huyo mnyasa hapa jf.

binafsi nataka sana kumfahamu vizuri na kufahamu uhusika wake katika harakati za kisiasa ndani ya tanganyika.

niwie radhi kwa ombi langu maana siku hizi nimekuwa sivutiwi kusoma magazeti ya hapa nyumbani hususani gazeti la raia mwema.

 
mzee wangu mohamed said itakuwa vyema kama utamuelezea kiundani huyo mnyasa hapa jf.

binafsi nataka sana kumfahamu vizuri na kufahamu uhusika wake katika harakati za kisiasa ndani ya tanganyika.

niwie radhi kwa ombi langu maana siku hizi nimekuwa sivutiwi kusoma magazeti ya hapa nyumbani hususani gazeti la raia mwema.
 
mzee wangu mohamed said itakuwa vyema kama utamuelezea kiundani huyo mnyasa hapa jf.

binafsi nataka sana kumfahamu vizuri na kufahamu uhusika wake katika harakati za kisiasa ndani ya tanganyika.

niwie radhi kwa ombi langu maana siku hizi nimekuwa sivutiwi kusoma magazeti ya hapa nyumbani hususani gazeti la raia mwema.
Smarte,
Sina taarifa nyingi kuhusu Denis Phombeah.

Phombeah
kwa mara ya kwanza nimemsoma katika kitabu, ''The Making of Tanganyika,''
(1965).

1566335354349.png


Kitabu hiki kiliandikwa na Judith Listowel na alipokuja Tanganyika kufanya utafiti wake
mwenyeji wake alikuwa Ally Sykes kupitia kwa Peter Colmore, Nairobi.

Kitabu hiki ndicho pekee katika vitabu vilivyoandikwa kuhusu historia ya TANU na harakati
za kudai uhuru ambacho kimekaribia sana kusema kweli.

Ndani ya kitabu hiki Listowel anahadithia uchaguzi wa mwaka 1953 Ukumbi wa Arnautoglo
kati ya Abdul Sykes na Julius Nyerere kuwania urais wa TAA.

Kuna kisa cha kueleza vipi Nyerere aliingizwa katika uongozi wa TAA kushindana na Abdul
Sykes
mwenyeji wake.

Kisa hiki nishakieleza hapa Majlis mara kadhaa naanimi unakijua.

Sasa kwa kuwa Denis Phombeah hakuwa anajua mipango iliyopangwa baina ya Abdul,
Hamza Mwapachu
na Ali Mwinyi Tambwe, yeye akitaka sana Nyerere ashinde uchaguzi
ule akawa anawapitia wapiga kura kuwashawishi wamchague Nyerere.

Katika uchaguzi ule Nyerere alimshinda Abdul Sykes kwa shida sana kwa hiyo akawa Rais
wa TAA.

Uongozi wa TAA 1953 kuelekea kuundwa kwa TANU 1954 ulikuwa kama hivi:

Viongozi hawa ni: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President:

J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer na Ally K. Sykes - Assistant Treasurer. Committee members Dr. Michael Lugazia, Ongalo na Patrick Aoko.

Huyu Phombeah alikuwa mmoja kati ya vijana wa Dar es Salaam wa wakati ule ambao
walikuwa katika siasa za TAA ingawa yeye alikuwa anatokea Nyasaland.

Kadi ya TANU ya Denis Phombeah ni no. 5.

Baada ya kifo cha Chihota kutoka Rhodesia ambae alikuwa meneja wa Arnautoglo Hall
nafasi ile ikashikwa na Phombeah Mnyasa.

Chihota alifariki Uingereza mwanzoni mwa miaka ya 1950.

Phombeah rafiki yake mkubwa alikuwa Oscar Kambona.
Baada ya Phombeah kwenda uhamishoni Uingereza Phombeah na yeye akamfuata huko.
 
Back
Top Bottom