Wanzania, kila unapoenda hawakosi cha kukuagiza

chiefnyumbanitu

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2015
Posts
906
Reaction score
426
Eti kila unapoenda hawakosi cha kukuagiza,ukienda mwanza utasikia tuletee samaki, ukienda mbeya tuletee mchele, ukienda tanga tuletee nazi,mtwala tuletee korosho, dodoma tuletee zabibu, bukoba tuletee ndizi bukoba,

Ukienda zanzibar tuletee deki au tv, harafu singida tuletee mafuta ya alizeti, ukienda moshi utasikia tuletee ndisi mshale babaangu, kigoma tuletee dagaa kigoma, tabora tuletee asali,

Mbaya zaidi ukienda iringa tuletee msichana wa kazi! daah... sasa mimi naenda sumbawanga kesho nikuleteeni nini?
 
Jamani Sumbawanga hakupo hivyo mnavyokufikiria. Tena nahisi Dar ina wanga na washirikina wengi kuliko Sumbawanga.
 
Yule mganga wa kuzuia mita za luku na kuzuia ziara za ghafla za Mzee wa kazi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…