Wapenda sherehe tukutane hapa

Babumawe

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2014
Posts
2,556
Reaction score
2,571
Kuanzia harusi, kitchen party, maulid, birthday, kipa imara na kadhalika kwa pamoja tuje hapa tualikane siunajua undugu ni kujuzana na kupeana mialiko.
Binafsi napenda sana sherehe yaani kwa wiki nikikosa hata mbili basi roho yangu hairidhiki kabisa.

Utamu wa shughuli kwanza hakunaga limit unakunywa tungi unavyojisikia wewe tena free hutoi hata senti tano sasa balaa linafika wakati wa maakuli pale unagonga vyuku vyako vya kutosha na nyama choma zako pembeni huku ukishushia zako na safari ya baridiiii.

Faida ya sherehe unakutana na totozi za kila aina unaweza na wewe ukajiokotea zako toto pale kimasihara masihara.

Haya ndugu zangu mimi binafsi nawakaribisha weekend hii pale mbezi makonde kuna bonge la sherehe mimi sio mbinafsi nyie wote humu ndugu zangu karibuni tufurahi kwa pamoja.

Usisahau pia nawewe kutukaribisha mapema shughuli zilizo kwenye ratiba zako ili tuandae suti zetu mapema
 
Aisee usinisahau unapopata mialiko.
 
Picha ipi hiyo tuizoom
Kwakuwa hajakuwa specific mi nahisi ni hiyo ya pilau..πŸ˜‚

Mkuu usimuite tafadhari nitachambwa mie mpk nione nyotanyota..πŸ™
 
Umenikumbusha mbali mkuu acha tu πŸ˜‚πŸ˜‚
..... Wali acha uitwe ubwabwa asee
 
Hahah

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
Nshavamia sherehe mingi sana yani sana tu... Alafu nlikua naonewa huruma kamwili kangu kadogo kinoma, imagine unazamia harusi humjui muoaji wala muolewaji ila kila kundi la ndugu likitajwa unainuka bila wasiwasi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
... Alieutaja umaskini kama adui wa mTZ hakukosea hata chembe
 
Basi mie nipo tofauti kabisaaah, sipendi sherehe km nini yaan,
Nkipewa mualiko ntatoa tyuuh mchango, pia zawadi bas. Ila sihudhurii mie. Labda iwe muhimu sana kwangu.
 
Hahaha

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…