Wapenzi wa Kiswahili Nisaidieni: Ajali Mbaya, Mafuriko ya Maji, Chini ya Mvungu, Msitu wa Miti nk

Wapenzi wa Kiswahili Nisaidieni: Ajali Mbaya, Mafuriko ya Maji, Chini ya Mvungu, Msitu wa Miti nk

SHIEKA

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
8,240
Reaction score
4,265
Enyi wadau wa Kiswahili. Habari zenu? Nawasilisha hapa misemo hii ninayoisikia kwenye radio na tv na kuisoma kwenye magazeti (hata hapa JF) na napata shida kuielewa.
Naanza kuzungumzia moja baada ya nyingine:
1. Ajali Mbaya: Karibu kila siku nasikia na kusoma msemo huu. Huwa najiuliza, je kama kuna ajali mbaya, ipo vilevile ajalinzuri? Ajali zote zinajulikana ni mbaya. Kwa hiyo ukisema 'Kuna ajali mbaya imetokea Msata, hakuna jipya ulilosema kuhusu hiyo ajali. Pengine ungesema 'Ajali kubwa imetokea Msata',ingekuwa bora zaidi. Kwa hiyo neno 'mbaya' kulitumia kuzungumzia ajali kwangu haileti maana. Wewe waonaje?

2.Mafuriko ya Maji: Hii nimeisikia sana juzijuzi kuhusiana na mvua kubwa zinazonyesha huko Indonesia. Mtangazaji alisema hivi: 'Mafuriko makubwa ya maji yameukumba mji wa Djakarta huko Indonesia baada ya mvua kubwa kunyesha'
Mimi najiuliza mtu akitaja mafuriko, si tayari mtu unapata picha ya maji meeengi yanayotiririka? Kwa nini useme tena
mafuriko ya maji? Kwangu hiyo mimi ninaona ni matumizi mabaya ya maneno. Mawazo yako je?

3.Chini ya Mvungu. Hii nimeisikia sana na inanishangaza. Chini ya mvungu ndo wapi tena huko jamani? Mimi najua mvunguni, yaani chini ya kitanda lakini chini ya mvungu mmhh! Nini maoni yako.

4.Msitu wa miti:Niliisikia siku moja hii nikapigwa na bumbuazi! Nikajiuliza: Kwani msitu ni wa nini? Mawe? Majani?
Mimi naona ukishataja msitu hakuna haja ya kuongeza neno 'miti' Umeshakutana nayo? Tupe maoni.

5. Faulo Mbaya:Hii niliisikia kwenye kipindi cha michezo. Mtangazaji alisema: 'Mchezaji wa timu X alimfanyia faulo mbaya mchezaji wa timu Y na refa akaamuru ipigwe penalti' Kwani kuna faulo nzuri? Ebu toa maoni yako.

6.Amekufa kabisa: Nayo hii nimekutana nayo mara kadhaa. Maoni yangu ni kwamba kufa ni kufa hakuna kufa nusu wala kufa kidogo.

Pengine ipo misemo mingi zaidi isiyoleta maana ambayo sijaitaja. Kama waifahamu ee mpenda kiswahili, iweke hapa

Asanteni.
 
Enyi wadau wa Kiswahili. Habari zenu? Nawasilisha hapa misemo hii ninayoisikia kwenye radio na tv na kuisoma kwenye magazeti (hata hapa JF) na napata shida kuielewa.
Naanza kuzungumzia moja baada ya nyingine:
1. Ajali Mbaya: Karibu kila siku nasikia na kusoma msemo huu. Huwa najiuliza, je kama kuna ajali mbaya, ipo vilevile ajalinzuri? Ajali zote zinajulikana ni mbaya. Kwa hiyo ukisema 'Kuna ajali mbaya imetokea Msata, hakuna jipya ulilosema kuhusu hiyo ajali. Pengine ungesema 'Ajali kubwa imetokea Msata',ingekuwa bora zaidi. Kwa hiyo neno 'mbaya' kulitumia kuzungumzia ajali kwangu haileti maana. Wewe waonaje?

1.Matumizi ya neno hili(Ajali mbaya) ni sahihi kabisa kwani yanazingatia usanifu wa lugha. "Mbaya" ni kivumishi cha sifa kinachotuelezea sifa ya hiyo AJALI. kivumishi unaweza kukipa viwango ili kuonyesha au kujenga picha na kuitofautisha na nyingine( degree of adjectives) mfano. Ajali mbaya-Ajali mbaya sana-Ajali mbaya kuliko zote:
kwangu mimi matumizi ya aina hii ya Lugha ni sahihi.

2.Mafuriko ya Maji: Hii nimeisikia sana juzijuzi kuhusiana na mvua kubwa zinazonyesha huko Indonesia. Mtangazaji alisema hivi: 'Mafuriko makubwa ya maji yameukumba mji wa Djakarta huko Indonesia baada ya mvua kubwa kunyesha'
Mimi najiuliza mtu akitaja mafuriko, si tayari mtu unapata picha ya maji meeengi yanayotiririka? Kwa nini useme tena
mafuriko ya maji? Kwangu hiyo mimi ninaona ni matumizi mabaya ya maneno. Mawazo yako je?

2.Katika Lugha ya kiswahili neno Mafuriko lina matumizi zaidi ya moja, mfano watu wanapoonekana mitaani kwa wingi wakati wa sikukuu utasikia wengi wakisema mitaa imefurika watu. maji yakiongezeka na kuna kuvuka kingo za mito au kuvamia makazi ya watu watu husema mafuriko ya maji.
Hivyo ili kutofautisha na kuondoa maswali je ni mafuriko ya nini au ya kitu gani ndipo matumizi kama haya hutumika.
jiulize iwapo ukisema " Sikukuu ya leo mtaani kumefurika"
ni wa ngapi watajua unaongelea maji? na niwangapi wataelewa unaongelea wingi wa watu?.
Ili kuondoa mchanganyiko huo ni sahii kusema mafuriko ya maji ili ueleweke ukimaanisha maji au mafuriko ya watu ukimaamisha watu.


3.Chini ya Mvungu. Hii nimeisikia sana na inanishangaza. Chini ya mvungu ndo wapi tena huko jamani? Mimi najua mvunguni, yaani chini ya kitanda lakini chini ya mvungu mmhh! Nini maoni yako.

3. Nijuavyo mimi ni UVUNGU na siyo MVUNGU. Lakini nakubaliana nawewe katika matumizi, siyo sahihi kusema chini ya Uvungu. ni Uvnguni au katika uvungu
4.Msitu wa miti:Niliisikia siku moja hii nikapigwa na bumbuazi! Nikajiuliza: Kwani msitu ni wa nini? Mawe? Majani?
Mimi naona ukishataja msitu hakuna haja ya kuongeza neno 'miti' Umeshakutana nayo? Tupe maoni.

4.100% Nakubaliana na wewe

5. Faulo Mbaya:Hii niliisikia kwenye kipindi cha michezo. Mtangazaji alisema: 'Mchezaji wa timu X alimfanyia faulo mbaya mchezaji wa timu Y na refa akaamuru ipigwe penalti' Kwani kuna faulo nzuri? Ebu toa maoni yako.

5.Rejea malezo ya ngu katika namba Moja haina tofauti na ile. Nasahii kutumia Lugha namna hii

6.Amekufa kabisa: Nayo hii nimekutana nayo mara kadhaa. Maoni yangu ni kwamba kufa ni kufa hakuna kufa nusu wala kufa kidogo.

6. Hapa pia nakubalina na wewe 100%

Pengine ipo misemo mingi zaidi isiyoleta maana ambayo sijaitaja. Kama waifahamu ee mpenda kiswahili, iweke hapa

Asanteni.

Nakubali kukoselewa kwani nami nitajifunza
 
Asante BUTTER. Umejieleza vizuri sana.
 
Last edited by a moderator:
Waungwana , Mimi naomba niongeze kidogo hapo kwenye kifungu kisemacho ´´Msitu wa Miti´´
Unaweza kusema Msitu wa Miti ya Asili,
Msitu wa Miti ya Kupanda.
Msitu wa miti ya Miyombo,
Msitu wa miti ya Mbao.

Hata hivyo nakubalina na maelezo aliyotoa mkuu BUTTER.
 
Enyi wadau wa Kiswahili. Habari zenu? Nawasilisha hapa misemo hii ninayoisikia kwenye radio na tv na kuisoma kwenye magazeti (hata hapa JF) na napata shida kuielewa.
Naanza kuzungumzia moja baada ya nyingine:
1. Ajali Mbaya: Karibu kila siku nasikia na kusoma msemo huu. Huwa najiuliza, je kama kuna ajali mbaya, ipo vilevile ajalinzuri? Ajali zote zinajulikana ni mbaya. Kwa hiyo ukisema 'Kuna ajali mbaya imetokea Msata, hakuna jipya ulilosema kuhusu hiyo ajali. Pengine ungesema 'Ajali kubwa imetokea Msata',ingekuwa bora zaidi. Kwa hiyo neno 'mbaya' kulitumia kuzungumzia ajali kwangu haileti maana. Wewe waonaje?

2.Mafuriko ya Maji: Hii nimeisikia sana juzijuzi kuhusiana na mvua kubwa zinazonyesha huko Indonesia. Mtangazaji alisema hivi: 'Mafuriko makubwa ya maji yameukumba mji wa Djakarta huko Indonesia baada ya mvua kubwa kunyesha'
Mimi najiuliza mtu akitaja mafuriko, si tayari mtu unapata picha ya maji meeengi yanayotiririka? Kwa nini useme tena
mafuriko ya maji? Kwangu hiyo mimi ninaona ni matumizi mabaya ya maneno. Mawazo yako je?

3.Chini ya Mvungu. Hii nimeisikia sana na inanishangaza. Chini ya mvungu ndo wapi tena huko jamani? Mimi najua mvunguni, yaani chini ya kitanda lakini chini ya mvungu mmhh! Nini maoni yako.

4.Msitu wa miti:Niliisikia siku moja hii nikapigwa na bumbuazi! Nikajiuliza: Kwani msitu ni wa nini? Mawe? Majani?
Mimi naona ukishataja msitu hakuna haja ya kuongeza neno 'miti' Umeshakutana nayo? Tupe maoni.

5. Faulo Mbaya:Hii niliisikia kwenye kipindi cha michezo. Mtangazaji alisema: 'Mchezaji wa timu X alimfanyia faulo mbaya mchezaji wa timu Y na refa akaamuru ipigwe penalti' Kwani kuna faulo nzuri? Ebu toa maoni yako.

6.Amekufa kabisa: Nayo hii nimekutana nayo mara kadhaa. Maoni yangu ni kwamba kufa ni kufa hakuna kufa nusu wala kufa kidogo.

Pengine ipo misemo mingi zaidi isiyoleta maana ambayo sijaitaja. Kama waifahamu ee mpenda kiswahili, iweke hapa

Asanteni.

Ajali mbaya inawezekana,kama vile ambavyo kuna kifo kizuri na kifo ambacho huwezi kumuombea yoyote,hata adui yako.
 
Nadhani tatizo laweza kuigiza lugha nyingine iwe za kikabila au za kimapokeo. Mfano Mafuriko ya maji. Je kuna mafuriko ya watu au melee kwa kiingereza ambapo mtu anaweza kutafsiri maneno kama people flooded the whole area to see the king.
Hili la ajali nadhani hakuna ajali nzuri. Mvungu ni neno geni kwangu. Kama mwandishi anamaanisha uvungu basi huwa ni uvunguni na si chini ya uvungu. Msitu wa miti nalo sina uhakika nalo. Sijui hata kama mtu akilinyambua toka lugha nyingine kama atapa msitu wa miti. Huenda kwa vile kuna msitu wa ndevu, vitabu na nywele basi kwa utohozi huu unaweza kuja na msitu wa miti.
 
Umesahau ule msemo wa 'watu takriban kama 5000' sikiliza watangazaji hasa wa vipindi vya michezo.
 
Mara nyingi kwenye Lugha ya kuzungumza kunakuwa na makosa mengi ya kisarufi, lakini tunapoandika tunapaswa kuondoa kasoro hizo..kwa sababu hata katika lugha ya Kiingereza, unaweza kumsikia mzungu mwenyewe akisema kwa mfano, "..very very difficult.." au hujasikia? Sehemu pekee ambapo mtu anapaswa kuwa makini na sarufi ni wakati wa kuandika. Hayo ni maoni yangu ..:shut-mouth:
 
Ajali zipo mbaya na za kawaida mfano mnapata ajali gari inapinduka inapondeka na kuwaka moto lakini inakuwa hakuna majeruhi walioumia sana au vifo
pia ajali zinakuwa mbaya pale uharibifu unapokuwa mkubwa na majeraha makubwa na vifo vingi hiyo ni ajali mbaya, rejea mv bukoba, ile ya pemba, ajali ya train Dodoma, moto Shauritanga sec na ajali za mabasi yaliyoteketeza roho nyingi kwa wakati mmoja
Lowasa na Igp mwema kwa nyakati tofauti wk iliyopita walipata ajali lakini hazikuwa mbaya
 
Back
Top Bottom