we mambo yako bwana,unanikumbusha ule mkasa wa kule nyumbani mtaa mmoja unaitwa Jan'gombe, jamaa mmoja alikuwa na mchezo huo, kuna nyumba moja ya rafiki yake akiionea sana, siku mmoja katika mawindo yake kwa mshkaji alikuta hata kile kitundu cha upenu wa dirisha anapopitisha jicho lake kushuhudia kadhia za watu na wenza wao kitandani,kimeongezeka kidoogo,akaona leo ndo kufaidi, maaana siku zote nafasi ya kuchungulia haitoshi hasa jamaa anapomgeuza mwenzake kiubavu ubavu na kimbinukobinuko. Akaanza kuwachapo mara ghafla akaanza kutoa chafya kali kali, kumbe mshkaji alishatonywa na aliamua kutega kwa kunyunyiza tumbaku eneo la dirisha na jamaa kwa kitahanani cha kushtukiwa akatimua mbio...pahala fulani akidhani pana shimo aliruka na alipodondokea ndo palikuwa na shimo lenyewe...akavunjika mguu...raha ikawa karaha kwake, hajakoma mpaka leo ni mpiga chabo profeshno wa eneo la Jan'gombe na Mpendae yake.