Wapiga Debe, Stendi ya BODA BODA Ndani ya UDSM Main Campus!!

Hapa mleta mada anamaanisha kuwa hata kile kituo cha shuttle za kuleta na kupeleka wanafunzi kule Mabibo nacho kifutwe, kwa kuwa nacho kimo ndani ya UDSM karibu na geti la CoET! Ikiwa kitafutwa kama anavyotaka huyu jamaa, basi wanafunzi watalazimika kupanda daladala za kawaida ambazo hazina route ya kufika mabibo, so ina maana ili ufike Mabibo unatakiwa ulipe sh. 600 kwenda na 600 kurudi, minimum sh. 1200 kwa siku (iwapo utashinda huko huko campus bila kurejea hostel hapo mida ya kati). Sasa 1200 si ndogo, sijui jamaa linafikiriaje hili!
 

nadhani wewe utakua ni jitu taahira kuliko wote hapa tanzania.aliyekuambia english ndo kigezo cha kufanya kazi ni nani?wakati mwingne jaribu kuficha huo uozo ulioko kichwani mwako aisee!
 

Eti nawe msomi wa kufikia kudharau baadhi ya vyuo? hujui kuwa Magazeti ya udaku yaliyojaa kwenye madarasa na ofisi za wahadhiri wako ni hatari kuliko bodaboda, hoja nlokwambieni ni kuwa Kama kweli mnachukia bodaboda nyie wasomi wenyewe chukueni hatua kwa kutopanda badala ykupiga kelele kila kitu management
 
mimi sifahamu hili neno wapiga debe jee ni nani hawa? naomba mnifafanulie shukuran
 

Joshua nduguyangu unamuonea bure songoro.hao ma Dr&Maprofessa wanampango wa kuwatengezea vyeti hao nduguzao tu.hawezi kuona hivyo wakae kimya.kumbuka kongamano lililo rushwa na ITV kuhusu ELIMU NA MUSTAKABALI WA TAIFA HAPO BAADAE.mwanaharakati Mkinga alisema wanachangia kuporomosha Elimu TZ kisha wanaandaa makongamano kulaumu serikali,wanaaaafiq wakubwa acha wanyimwe mikataba.
 

Joshua nduguyangu unamuonea bure songoro.hao ma Dr&Maprofessa wanampango wa kuwatengezea vyeti hao nduguzao tu.hawezi kuona hivyo wakae kimya.kumbuka kongamano lililo rushwa na ITV kuhusu ELIMU NA MUSTAKABALI WA TAIFA HAPO BAADAE.mwanaharakati Mkinga alisema wanachangia kuporomosha Elimu TZ kisha wanaandaa makongamano kulaumu serikali,wanaaaafiq wakubwa acha wanyimwe mikataba.
 
Halafu nadhani mtoa mada atakuwa MWANARUZINGA
 
Mkuu bodaboda zipo jamani,mtoa hoja ana point ya msingi sana.Ninaye aunt yangu yuko pale,niliwahi kumuuliza kuhusu biashara hiyo ya boda boda akanieleza kuwa uongozi wa chuo umewaruhusu wafanyakazi kuleta bodaboda zao kwa kuwaajiri hao vijana.

Chuo kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani ni chuo kikongwe sana,ni image ya nchi kwa ujumla.Utaratibu na maadili ya kisomi lazima yaakisiwe kwa wanajumuia wote wa chuo.

Hakuna asiyejua adha na kadhia waliyonayo hao wanaojiita madereva wa bodaboda.Vitendo vya ukaidi,wizi,fujo nk kwao si msamiati.Sio mbaya kukuza ajira,lakini lazima pia tuangalie tusijenge wakati tunabomoa tulikokwishajenga.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Acha uzembe wa kufikiri, hao wasomi si ndo wateja? Boda boda ni wafanyabiashara wanaofata wateja sasa kama wasomi wenyewe hawaoni karaha basi hakuna tatizo pia kumbuka DKT NDUGULILE NA DOCTA MTARAJIWA LOWASSA walisema ni sehemu ya Ajira

Mkuu ndio kuwe na wapiga debe kweli?
 

Kweli mkuu, hata kuheshimiana katika hoja hakuna, ni majibu ya hovyo hovyo tu. Hata kama mtu kakosea kwa nini umtusi na majibu ya kejeli. Inaonyesha kutokomaa kabisa kiakili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…