KERO Wapiga Debe wanaotafuta Abiria wa Mabasi katika Kituo cha Daladala Mbezi Luis ni kero kubwa

KERO Wapiga Debe wanaotafuta Abiria wa Mabasi katika Kituo cha Daladala Mbezi Luis ni kero kubwa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Mshobaa

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2013
Posts
1,714
Reaction score
677
Wapiga Debe katika Stendi ya Daladala ya Mbezi Luis wamekuwa kero kubwa kutokana na yale wanayoyafanya kila siku kutuoni hapo kwa nia ya kutafuta Abiria wanaoelekea katika Kituo cha Mabasi cha Magufuli Bus Terminal.

Kwanza Daladala ikiwa inaingia hasa majira ya asubuhi ambapo kuna mpishano wa watu wengi kituoni hapo, wao wanadandia magari yanapoingia kituoni na kuyakimbiza, jambo linahatarisha usalama wao na watumiaji wengine wa stendi.

Daladala ikisimama wanaanza kuwasumbua abiria wanaoshuka na hata wale wanaotaka kupanda kwenye usafiri huo, wakiona kuna Abiria anayeelekea Stendi Kuu ya Magufuli ndio kabisaa kero inazidi

Wanaanza kuwavutavuta Abiria wenye mizigo, wanajidai wanawasindikiza na kutaka kubeba mizigo yao bila ridhaa ya Abiria na wapo wanaotumia nafasi hiyo kufanya vitendo vya wizi.

Kuna matukio kadhaa yametokea ya wizi hasa wakati wa msongamano wa Abiria wanaoshuka na wanaoingia kwenye daladala huku Wapiga Debe hao wakiwa ni kati yao kwenye kundi hilo

Mamlaka zinazohusika na kituo hicho zinapaswa kufanya jambo kwa kulishughulikia suala hili kwa kina ili kudhibiti watu hawa, kwani baadhi yao hujichomeka kwa lengo la kusaidia abiria kumbe ni vibaka na wengine wana malengo mabaya zaidi.
 
Stendi ya Daladala Mbezi ipo chini ya TANROADS.

Magufuli Bus Terminal ipo chini ya Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.

Hawa jamaa wanajulikana pale Mbezi kama Masalange.

Ni wakupiga vita kwa sababu ni wasumbufu sana na ni kero.
 
Nimaisha yao na ajira yao achana na Hawa waizi wadogo wadogo mkuu

kemea wale vigogo majizi ya mabilioni ambayo Yana safishwa na jina fisadi
 
Inasikitisha sana unakuta pale pa kuingilia Pana rundo la askari lakini hawana hata mpango wa kinachoendelea zaidi ya kuwaangalia tu
Wale vibaka wamewekwa na hao askari wakiiba wanawapa askari mgao ndo maana ukienda kulalamika umeibiwa askari wanakufukuza au kukubàmbikia kesi.
 
Unataka na sisi wapiga debe tule wapi mkuu?Yani badala ya kukemea mafisadi uko waizi wa mali za umma unatupigia kelele sisi.
 
. Ukitaka kusafiri kwenda mikoani, nenda ofisi za ma-basi husika... Utapanda basi kwa raha mstarehe....

. Pale maguli stand ni kero kiwango cha rami.
 
Hivi bado watu wanakata ticket kupitia wapiga debe?
Wapo mkuu we nenda pale utashangaa wanakua na vijitabu vya risiti kabisa utakuta msafiri katoka mbali haelewi utaratibu wa kupanda mabasi ndio hao wanapotumia mwanya huo kuwaibia
 
Hiyo ni moja ya biashara ya udalali au uwinga Tanzania, na wanakuwa backed up na wenye mabasi hasa Yale yasiyo na jina. Ndo waingo namba moja , Kata tiketi basi hii ya mwisho inaondoka baada ya nusu saa, Sasa toa pesa, massa 4 baadae ndo unaondoka
 
Back
Top Bottom