Wapinzani msije mkaingia au kuingizwa chaka, CCM ni ile ile

Wapinzani msije mkaingia au kuingizwa chaka, CCM ni ile ile

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Hii ni mbiu ya mgambo kwa upande wa Upinzani, msilegeze kamba katika kuhakikisha madai ya tume huru na iliyobora inapatikana sambamba na Katiba mpya, hayo ya CCM ya kutumbuana kuhamishana, kusifiana kukandiana hayo ni yao na yawachwe kama yao.

Leo mnasema au inasemwa ndani ya CCM kuna wanaosabotaji, wanaokandia na mambo mengi ya kufanya kuonekanwe kama kuna mvutano ndani ya CCM, Kuna mambo ya kitaifa zaidi ambayo yasiachwe kupigiwa kelele hata kama yanaenda vizuri, huo ndio siasa za upinzani.

Inawezekana wengi waliondani ya upinzani haswa ya kisiasa hawaelewi vizuri nembo ya upinzani katika duru za kisiasa, niseme tu ni sumu kwa chama cha upinzani kuisifu serikali ya chama inayoongoza nchi ni mwiko. Unatakiwa uponde hata Rais anavyotembea labda iweke kionjo.

Rais anatembea kwa kujilabu na kutanua mikono yote ni kuonyesha dharau, mmeona hivyo ndivyo inavyotakiwa, kuna waziri anaitwa sijui Jafo amefanya sijui madudu gani, amewajaza wazinifu waliokubuhu katika skendo mbalimbali eti ndio wawe maraisi wa maendelea kisa tu wana followers wengi katika account zao za social media nahisi hicho ndio kigezo. Hapo pekee upinzani wangevalia barakoa na njuga wakapiga makelele ya kila rangi alimuradi Jafo ajute alichokifanya.

Msiingizwe choo cha kike CCM .sisi wananchi tunaijua inatumia mambo mengi kuwapumbaza wapinzani lakini siku za uchaguzi zinapokaribia wote huwa pamoja katika kuhakikisha wanaikandamiza haki na cha haramu kukifanya kwao kuwa halali, mnajua yaliyotokea uchaguzi mkuu uliopita.

Kuweni macho na hila zao hakikisheni msiwape nafasi CCM kufurukuta mnawabana kwa mwendo mdundo mpaka kieleweke, msiiwache serikali ika-relax ni hatari kwenu watawauwa na kuwazima kirahisi na mbaki mkiita vyombo vya habari.
 
Tuanze na ukomo uongozi wa wenyeviti wa vyama vyetu! Lipumba, Mbowe, nk

Tuanze kwa kutoa boriti machoni petu kabla hatujaangalia kibanzi kwenye jicho la CCM
 
Tuanze na ukomo uongozi wa wenyeviti wa vyama vyetu! Lipumba, Mbowe, nk
Tuanze kwa kutoa boriti machoni petu kabla hatujaangalia kibanzi kwenye jicho la CCM
Wewe inaonyesha hujui hata ulichokiandika au huna uelewa nacho, Chama cha siasa sio kilabu cha mpira au umoja wa vikoba, Chama Cha siasa hakitakiwi kubadilisha viongozi wakuu angalia vyama vya siasa dunia nzima tokea huko vinapigania uhuru utaelewa vizuri.

Sasa kwa hili achana nalo, CCM hawana mwenyekiti wa Chama wao kwa vile wapo madarakani wameweka utaratibu wa Mgombea wao uRaisiambae miaka yote anashinda kwa wizi wa kura ndie awe mwenyekiti wao.

Ni utaratibu wamejipangia ila usikae mbali karibu utaratibu huo utayeyuka kwani nguvu ya upinzani inakuwa kwa kasi kubwa,siku wakianguka tu utamtafuta hata balozi wa ccm usimuone wote watava magauni na barakowa.
 
Kama Mbowe, Lissu, Zitto na viongozi wengine wa upinzani ambao wana maono zaidi yako wanaonekana kukubaliana na uongozi wa mama, wewe ni nani mpaka uje na hoja mfu kama hii.

Bila shaka ww ni mmoja wa wale waliofilisika kimawazo, nakushauri uanzishe chama chako kitakachokuwa tayar kupinga pinga kila kitu kuliko kujaribu kuja kuwalisha watu uharo wako humu jukwaani.

Pinga pinga ikizidi sana ipo siku utakuja kuwapinga hata wazazi wako kwamba ww haukuzaliwa bali ulitoka chini ya mwembe.
 
Kama Mbowe, Lisu, Zito na viongozi wengine wa upinzani ambao wana maono zaidi yako wanaonekana kukubaliana na uongozi wa mama, wewe ni nani mpaka uje na hoja mfu kama hii. Bila shaka ww ni mmoja wa wale waliofilisika kimawazo, nakushauri uanzishe chama chako kitakachokuwa tayar kupinga pinga kila kitu kuliko kujaribu kuja kuwalisha watu uha.ro wako humu jukwaani. Pinga pinga ikizidi sana ipo siku utakuja kuwapinga hata wazazi wako kwamba ww haukuzaliwa bali ulitoka chini ya muembe.
Unayo sema ni sawa yakipata msikilizaji, ila kwa msomaji ni ushuzi tu, kama hao wanamuunga basi wahamie huko, lakini sio kweli wewe wacha kuzua na kuwazulia wenyeviti wa vyama kuwa wanaiunga mkono serikali ya CCM kwa Lipi, huko kuzua kwako utakuja kuzua kuwa huyo baba yako sie aliekuzaa.
 
Wewe ni kidagaa tu hapo chadema!

Wanachadema yao kina Mbowe, Lisu, lema na wengineo wamekubaliana kumuunga mkono mama ili kumkomoa marehemu.
 
Wewe ni kidagaa tu hapo chadema!

Wanachadema yao kina Mbowe, Lisu, lema na wengineo wamekubaliana kumuunga mkono mama ili kumkomoa marehemu.
Ulaghai huo haupo mnataka ionekane hivyo, ili iweje,wacha niwe kidagaa lakini wewe na wengi mliozuka kuwavisha viongozi wa upinzani ngozi ya kondoo mnajidanganya ,eti ionekane wanamkomoa marehemu ,halafu iweje marehemu atakereka ? Na kazi ipi iendelee ,wewe ni uduvi tu hapo kwenye ccm ,yule anaesema kazi ya marehemu iendelee ni nani kambale ?
 
Unayo sema ni sawa yakipata msikilizaji ,ila kwa msomaji ni ushuzi tu,kama hao wanamuunga basi wahamie huko,lakini sio kweli wewe wacha kuzua na kuwazulia wenyeviti wa vyama kuwa wanaiunga mkono serikali ya CCM kwa Lipi ,huko kuzua kwako utakuja kuzua kuwa huyo baba yako sie aliekuzaa.
Ukitaka kujua kama hao niliowataja hapo juu wanakubaliana na mama angalia jinsi nyumbu wao walivyoupuuza uzi na ushauri wako.
 
Ulaghai huo haupo mnataka ionekane hivyo, ili iweje,wacha niwe kidagaa lakini wewe na wengi mliozuka kuwavisha viongozi wa upinzani ngozi ya kondoo mnajidanganya ,eti ionekane wanamkomoa marehemu ,halafu iweje marehemu atakereka ? Na kazi ipi iendelee ,wewe ni uduvi tu hapo kwenye ccm ,yule anaesema kazi ya marehemu iendelee ni nani kambale ?
Hao viongozi wako wa upinzani ndio wako hivyo angalia wafuasi wao wa humu jf wanavyodenka kumsifia mama.

Imefika hatua hata mtu akifanya ufisadi wanasema sawa tu maana marehemu alifanya ufisadi peke yake.

Ni bora hata ZITTO anaweza kueleweka maana juzi aliweka mgombe kwenye chaguzi ndogo, ila hao viongozi wako wengine waliamua kupiga kimya ili wamuunge mkono mama na kumkomoa marehemu.

Walisingizia tume ila ukweli ni huo maana kama ni tume, wameshiriki chaguzi nyingi sana kwa tume hii hii.
 
Kama Mbowe, Lissu, Zitto na viongozi wengine wa upinzani ambao wana maono zaidi yako wanaonekana kukubaliana na uongozi wa mama, wewe ni nani mpaka uje na hoja mfu kama hii.

Bila shaka ww ni mmoja wa wale waliofilisika kimawazo, nakushauri uanzishe chama chako kitakachokuwa tayar kupinga pinga kila kitu kuliko kujaribu kuja kuwalisha watu uharo wako humu jukwaani.

Pinga pinga ikizidi sana ipo siku utakuja kuwapinga hata wazazi wako kwamba ww haukuzaliwa bali ulitoka chini ya mwembe.
Haoni hadi vikao vya ndani wanafanya. Huyu atakuwa mmoja ya lile genge anaumia
 
Tuanze na ukomo uongozi wa wenyeviti wa vyama vyetu! Lipumba, Mbowe, nk

Tuanze kwa kutoa boriti machoni petu kabla hatujaangalia kibanzi kwenye jicho la CCM
Wafaa MBOWE yupo na ataendelea kuwepo yan ,kunywa maji moyo usipanuke mkuu
 
Back
Top Bottom