Wapinzani na Utekelezaji wa Sera ya Wagawanye Uwatawale (Divide & Rule Policy)

Wapinzani na Utekelezaji wa Sera ya Wagawanye Uwatawale (Divide & Rule Policy)

Amani Msumari

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2016
Posts
1,830
Reaction score
972
Wanabodi,

Historia ni somo la muhimu sana kwani linatuonesha ni wapi tulipotoka, tulipo na kutuwezesha kupanga na kutabiri kesho yetu.

Wakoloni walipokuja Afrika hawakuja moja kwa moja. Walikuja kwa hatua, kwa kuwatanguliza wamishionari, wapelelezi na wafanyabiashara. Hawa walipeleleza tabia zetu, utamaduni wetu, uimara na udhaifu wetu. Walipoweka mambo sawa, wakatuvamia.

Katika uvamizi mpaka utawala, wakoloni walishirikiana na waafrika wenzetu. Hata sasa, hatujasahau mateso, dhiki, unyanyasaji, dharau na madhila waliyotufanyia achilia mbali unyonyaji wa rasilimali walioufanya. Kwa taarifa tuu, hata kutupa uhuru ilikuwa ni mbinu ili wasitumie tena nguvu bali akili katika kututawala.

Ukoloni mamboleo ndio unaoutumika kuidumaza Afrika. Leo hii haishangazi kumuona kiongozi mkubwa wa kisiasa akijinasibu kwa kuongea kiingereza fasaha. Tupo kwenye vita ya uchumi na wakubwa wanataka Afrika iendelee kuwa soko na mzalishaji wa rasilimali kwa viwanda vya viranja wa dunia.

Kwa mantiki hiyo, wakubwa hao watafanya kila namna ili tusiendelee maana kuendelea kwetu ni hatari kwa ustawi wa uchumi wao. Angalia kilichowapata marehemu Gaddafi na Mugabe. Libya na Zimbabwe zilikuwa nchi bora kabisa Afrika ila viongozi walipoingilia maslahi ya wakubwa "wakakiona chamtemakuni". Wenyewe hawana adui au rafiki wa kudumu Bali wana maslahi ya kudumu.

Mabeberu ni wajanja sana, hawaingilii nchi yoyote bila kupata vibaraka wao ndani ya nchi husika. Kwa bahati mbaya, sehemu nyingi wametumika "wapinzani uchwara". Sehemu yoyote ambapo wananchi wanakuwa na umoja, basi nchi hizo haziingiliki.

Niwaombe sana watanzania wenzangu kuwa makini sana kipindi hiki cha Uchaguzi kwani ndio msimu wenyewe wa kutumika. Kampeni ziende kwa amani, umoja, staha na ustaarabu.

Amani Msumari
Tanga (kwasasa Arusha kwa kazi maalumu)
 
Utskuwa unawazungumzia CCM... Wamefanya hivyo kwa muda wa miaka 60.
 
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020
 
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020
Uhuru tulishaupata siku nyingi. Sasa hivi tunafanya kazi ya kuulinda uhuru wetu kwa vitendo. Kazi zaidi, ubunifu na weledi ili tuwe na uhuru kamili wa kiuchumi
 
Uhuru tulishaupata siku nyingi. Sasa hivi tunafanya kazi ya kuulinda uhuru wetu kwa vitendo. Kazi zaidi, ubunifu na weledi ili tuwe na uhuru kamili wa kiuchumi
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020

Achana na takataka za ccm
 
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020

Achana na takataka za ccm
Siwezi kumchagua Tundu na nawashauri watanzania tumuadhibu kwa Kumnyima kura

Kura zote kwa Magufuli, mbunge na diwani wa CCM ili kuendeleza mazuri yaliyofikiwa
 
Siwezi kumchagua Tundu na nawashauri watanzania tumuadhibu kwa Kumnyima kura

Kura zote kwa Magufuli, mbunge na diwani wa CCM ili kuendeleza mazuri yaliyofikiwa
Ukipiga kura ya rais kwa Tundu Lissu, ujue unapiga kura ya katiba mpya, ujue unapiga kura kwa rais ambaye atarudisha uhuru na haki za wananchi, ujue unapiga kura kwa rais ambaye hatawasimanga..".Tundu Lissu. #Uchaguzi2020

Achana na takataka za ccm
 
CCM chini ya Rais Magufuli imedhamiria haswa kuwaletea watanzania maendeleo. Kamwe hatutakubali kukwamishwa na maadui wa ndani na nje.
 
Katika majimbo ambayo yalioongozwa na ccm kwa mafanikio, ni Musoma (kwa mkono)
 
Back
Top Bottom