Uchaguzi 2020 Wapinzani wachukue hatua zifuatazo nyakati hizi kuelekea kupiga kura

Uchaguzi 2020 Wapinzani wachukue hatua zifuatazo nyakati hizi kuelekea kupiga kura

expirience man

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2013
Posts
214
Reaction score
104
Kama inavyofahamika kuwa uchaguzi ni mchakato wenye hatua mbalimbali na huitimishwa na upigaji wa kura na utangazaji wa matokeo.

Inafahamika pia aina ya tume ya uchaguzi tuliyonayo haiko on favor ya wapiga kura ambao ndio wananchi, tume ipo kwa ajili ya kuhakikisha CCM inabakia madarakani.

Hili limejionesha wazi zaidi mwaka huu pengine kuliko chaguzi zilizopita na kuufanya uchaguzi wa mwaka huu kuwa tofauti sana na chaguzi zilizopita.

Tumeona matendo ya NEC kupitia kwa mkurugenzi wake Dkt. Wilson Mahera ni ya kutilia mashaka sana.

Pia matendo ya vyombo vya usalama wakiongozwa na polisi yanatia shaka sana.

Pamekuwepo na matamko toka NEC na jeshi la Polisi kuelekea kwa upande mmoja tu wa wapinzani kwa aina ya matendo yanatofanywa na wagombea wa vyama vyote lakini wanakemea upande mmoja tu.

Usiku wa Jana zipo taarifa kupitia mitandao ya kijamii kuvamiwa kwa ngome za wagombea wa ubunge mkoa wa Mara na Arusha na watu wanaodaiwa kuwa ni Jeshi la Polisi. Inaripotiwa kuwa vifaa mbalimbali vya kampeni za wagombea hao. Mambo hayo hapo juu yananisukuma kuandika taadhari zinazopaswa kuchukuliwa na wapinzani kulinda ngome zao na vituo vya kijumlisha matokeo Kila Jimbo.

1. Waweke vituo vyao kwa siri kubwa sana na viwe zaidi ya kimoja kwenye Jimbo.

2. Kuandaa vituo hewa ili kupoteza maboya.

3. Nyakati Kama hizi waweke vijana kwenye kambi za siri kwa ajili ya kazi hiyo ya ujumlishaji matokeo yao na ikibidi wasitoke hata nje wiki mbili kabla ya uchaguzi mpaka kutangazwa kwa matokeo. Hii itasaidia kupunguza mamluki wa kuchomekewa. Kuteuwa mawakala wanaoaminika kuwawezesha pia kuwa na timu itakayoratibu kuhakikisha kila wakala anaapishwa na anaingia kwenye kituo, asipoingia kituo husika muhakikishe hakuna upigaji kura hapo unafanyika by any means necessary.

4. Ku-rise awareness ya jamii kuwa tayari ikiwa hujuma zitafanyika, hili linapaswa kusisitizwa na kila mgombea katika Kila ngazi ili kuweka msisitizo wa kauli ya Mbowe na Lissu kuhusu hujuma za uchaguzi.

Kuhitimisha hili nisisitize tu huu uchaguzi wapinzani wakitembea na nguvu ya umma watafanikiwa zaidi.
 
Ni kwl..kwa ufupi Upinzani wanatakiwa kujiuliza "cooked votes na Raw votes ni nini, cooked votes znapatkanaje? Znaingiaje na kuwa Raw votes? Raw votes znachanganywaje na cooked?

Ni wakat gani cooked votes znaingzwa kuwa raw votes? How to trace raw votes? How to trace cooked votes"? Where are the sites or locations or centres for cooking cooked votes? But the most important "matokeo ya uchaguzi yawe ni Yale wananchi wanataka na sio ya kupikwa"

Haya maswali ya tathmin iwe kwa umakini wa hali ya juu. Hapa wezi wa Kura hawatatoboa nawambia!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu jaribu kuhariri bandiko lako, una makosa mengi ya kiuandishi mpaka unapoteza ladha ya bandiko lote.
Kweli kabisa mm imebidi niishie njiani, mwamba ameandika kwa jazba sana
 
Kura yako ni muhimu sana panga bajeti muda na pesa.Utafurahia sana ushiriki na matokeo, tuhamasishe na wengine wengi iwezekanavyo. Natamani status wosap nk zisomeke ujumbe kuhamasisha kupiga kura.
 
Taarifa...Ilani ya CCM ilofuta ualimu ngazi ya cheti hii hapaaa.

Wasambazieni walimu... Huo ndo mpango wa Magufuli.
IMG_20201006_090936_175.jpg
 
Tumeambiwa simu zitazimwa wiki moja kabla ya 28-10-2020. Warudi analogia ama 'intercom system'
 
Big point kabisa. This time kitaeleweka kabisa.
Ila sisiemu wa ajabu sana yaani wanachana mabango na kuvunja spika kweli?

Yaani watu wameshaamua mioyoni mwao this time hawatishiki kabisa kwa lolote.
 
Back
Top Bottom