Wapo Watanzania wapambanaji lakini hawajafanikiwa kwasababu ya kurogwa na ndugu au majirani zao

Hakuna uchawi naishi kwetu miaka kibao ,nimesoma mpaka nimepata kazi hapa Sijaonw huo ujinga.
Mambo ya Walawi 20:27
[27]Tena mtu mume au mtu mke aliye na pepo, au aliye mchawi, hakika atauawa; watawapiga kwa mawe; damu yao itakuwa juu yao.
A man also or woman that hath a familiar spirit, or that is a wizard, shall surely be put to death: they shall stone them with stones: their blood shall be upon them.
 
Hiyo ni imani ya hovyo ,hakuna anayeweza kukurudisha nyuma ...Hakuna ndugu Yako anayekuroga ..

Ukishaanza kuamini hayo mambo basi unakuwa kama zombie.
Wewe bado hujarogwa, ukirogwa ndo utajua uchawi upo au haupo
 
Uchawi ni sanaa ,Rudi ukasome ...Vitabu vya kichawi vipo kibao hata wazungu wanatumia.

Kuhusisha matukio na uchawi mda mwingine hakuna uhusiano kabisa..
 
Mtoa mada katoa mifano ya watu walioanza kufanya maendeleo huko kwao wote walirogwa wakafa
Si kweli😅😅😅...Nauliza huo uchawi una nguvu ya kurudisha watu nyuma tu ila sio mafanikio.
 
Hizo ni hadithi tu za kufikirika
 
Ukifanikiwa kutoka kwenye lindi la umasikini wakati 89% ya ndugu zako ni masikini bado punguza WEMA. Na ni vyema ukajivisha u freemason ili uongeze umbali kati yako na wao.

Kwepa sana matukio ya mikusanyiko ya nyumbani kwenu,km ni sherehe jaribu kutokuonekana kabisa.
Msibani nenda na USIELEWEKE KWA YEYOTE HATA SEKUNDE MOJA.
 
Shida huku Bongo mtu akipatwa na matatizo ya kiafya au kiuchumi basi anaamini karogwa mwishowe anatupa pesa kwa waganga au manabii uchwara.
 
Hakuna uchawi naishi Tanga tangu miaka ya 90's ,stori zenu ni za kutunga 😅😅.

Uchawi ni sanaa ya kiini macho ila haiko serious mpaka kuua mtu.

Hata kuishi wapi sasa wewe kama unaona anadanganya si upite zako, uzi umeukalia kama wako.

Fix fix tu
 
Imani za watu wajinga.
 
Ili kutoboa katika jamii za Watanzania usisahu kuzingatia jadi. Nafikiri imeeleweka. Kuna watu ni komesha, wamefuata jadi wapo maofisi makubwa yenye hela, hata uweke sumu kwenye chakula hali na anashtukia. Hao ndio wanadumu katika ulimwengu huu!

Atakuja kufa Mungu akipenda. Katika Tanzania ye leo watu wanaharibiana sana kupitia jadi.

Nakuhakikishia, katika Tanzania hii, ukiwa na mafanikio na nguvu zako za kiroho ni dhaifu haufiki mbali. Watu wana wivu balaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…