Eliah Geofrey Kamwela
Senior Member
- Dec 30, 2018
- 184
- 507
Nimekutana na watu kadhaa wanao anza biashara au miradi, haswa waajiriwa wanao taka kuongeza kipato nje ya ajira zao, wakikata tamaa na kuachana na hab ari ya miradi pale zinapo ibuka changamoto kama Kuibiwa na wafanyakazi wao, hasara na misala mingine.
Wemgi hapa huishia kusema, "Chaaaaa!!! Kama ujasiriamali wenyewe Ndio huu, bora tu Nile mshahara inatosha", na hufikia huu uamuzi si kwamba inatosha kweli, Bali ni kwa kuchoshwa na misala isiyo isha.
Hebu nikupe machache hapa yanayo weza kukusaidia:
1: Kazi unayo ifanya unaisomea kwa wastani wa miaka isiyo pungua 12 hadi 16(ukihesabu toka elimu ya msingi) na huko na huko kote unalipa Ada.
Katika kujiajiri pia kuna ada unayo paswa kulipa, na moja ya aina ya ada ni 'misala' ya hapa na pale!!
2. Matatizo na chqngamoto katika ujasiriamali ndizo zinajenga 'misuli' ya ujasiriamali. Kujenga misuli kunahitaji kunyanyua chuma au vitu vizito, ni kitu kisicho vutia sana, ila Ndio kinampa 'Siksi paki' mbeba vyuma. Vyuma vya ujasiriamali ni Chang a moto ambavyo kadri unazitatua misuli yako inajengeka na unakua na uwezo wa kukabili Mengi magumu.
3. Kama unavyo jifunza kwa bidii ili ufanye kazi ya kuajiriwa, ni muhimu pia kujifunza kwa bidii ili utoboe pia upande huu. Sasa wengi wanataka kuchukua tu Mkopo na kuwekeza , wakipigwa wanaishia kuutukana ujasiriamali kuwa ni ufala wakati wao hawajataka kujifunza.
Ndio maana kwa mfano, nimekuandikia Kitabu cha 'NGUVU YA KUANZA KUELEKEA UHURU WA KIUCHUMI' ambapo nimeeleza namna unavyo weza kuanza na kuendelea na ujasiriamali ukiwa na ajira yako kwa mafanikio. Hutakiwi kuacha kujifunza!!!
3. Katika shule, mwanafunzi mtukutu hukimbia mitihani na werevu hupambana na mitihani hadi wafaulu.
Hata katika miradi, kuzira miradi badala ya kusaka suluhu ni sawa kabisa na mwanafunzi anaye kimbia mitihani!! Huyu hata alalamike vipi, atadharauliwa tu! Wakati unalalamika kwamba mshahara hautoshi, kuna mwingine analipwa kidogo kuliko wewe na anaishi maisha ya utoshelevu kwa kuwa anazalisha!!
4. Mwisho kwa leo, ingawa si kwa umuhimu, ni kuwa upende au usipende, ujasiriamali haukwepeki! Usipo ufanya kwa hiari sasa ukiwa kazini, utalazimika kufanya kwa lazima pale utakapo staafu!!
Huu wa lazima ni hatari kwa kuwa risk ya kufeli kwa ujasiriamali kipindi hicho ni stress zinazo weza hata kufupisha uhai wako.
Wito wangu ni kuwa usiache kujifunza na kufanya na kurekebisha makosa hadi kieleweke, hasa sasa ukiwa na nguvu zako zote.
Kwa leo hebu niishie hapa, nitaendelea wakati mwingine.
#Divine_Solutions_Carrier.
Fb: Eliah Geofrey Kamwela
IG: Eliahkamwela.
Wemgi hapa huishia kusema, "Chaaaaa!!! Kama ujasiriamali wenyewe Ndio huu, bora tu Nile mshahara inatosha", na hufikia huu uamuzi si kwamba inatosha kweli, Bali ni kwa kuchoshwa na misala isiyo isha.
Hebu nikupe machache hapa yanayo weza kukusaidia:
1: Kazi unayo ifanya unaisomea kwa wastani wa miaka isiyo pungua 12 hadi 16(ukihesabu toka elimu ya msingi) na huko na huko kote unalipa Ada.
Katika kujiajiri pia kuna ada unayo paswa kulipa, na moja ya aina ya ada ni 'misala' ya hapa na pale!!
2. Matatizo na chqngamoto katika ujasiriamali ndizo zinajenga 'misuli' ya ujasiriamali. Kujenga misuli kunahitaji kunyanyua chuma au vitu vizito, ni kitu kisicho vutia sana, ila Ndio kinampa 'Siksi paki' mbeba vyuma. Vyuma vya ujasiriamali ni Chang a moto ambavyo kadri unazitatua misuli yako inajengeka na unakua na uwezo wa kukabili Mengi magumu.
3. Kama unavyo jifunza kwa bidii ili ufanye kazi ya kuajiriwa, ni muhimu pia kujifunza kwa bidii ili utoboe pia upande huu. Sasa wengi wanataka kuchukua tu Mkopo na kuwekeza , wakipigwa wanaishia kuutukana ujasiriamali kuwa ni ufala wakati wao hawajataka kujifunza.
Ndio maana kwa mfano, nimekuandikia Kitabu cha 'NGUVU YA KUANZA KUELEKEA UHURU WA KIUCHUMI' ambapo nimeeleza namna unavyo weza kuanza na kuendelea na ujasiriamali ukiwa na ajira yako kwa mafanikio. Hutakiwi kuacha kujifunza!!!
3. Katika shule, mwanafunzi mtukutu hukimbia mitihani na werevu hupambana na mitihani hadi wafaulu.
Hata katika miradi, kuzira miradi badala ya kusaka suluhu ni sawa kabisa na mwanafunzi anaye kimbia mitihani!! Huyu hata alalamike vipi, atadharauliwa tu! Wakati unalalamika kwamba mshahara hautoshi, kuna mwingine analipwa kidogo kuliko wewe na anaishi maisha ya utoshelevu kwa kuwa anazalisha!!
4. Mwisho kwa leo, ingawa si kwa umuhimu, ni kuwa upende au usipende, ujasiriamali haukwepeki! Usipo ufanya kwa hiari sasa ukiwa kazini, utalazimika kufanya kwa lazima pale utakapo staafu!!
Huu wa lazima ni hatari kwa kuwa risk ya kufeli kwa ujasiriamali kipindi hicho ni stress zinazo weza hata kufupisha uhai wako.
Wito wangu ni kuwa usiache kujifunza na kufanya na kurekebisha makosa hadi kieleweke, hasa sasa ukiwa na nguvu zako zote.
Kwa leo hebu niishie hapa, nitaendelea wakati mwingine.
#Divine_Solutions_Carrier.
Fb: Eliah Geofrey Kamwela
IG: Eliahkamwela.