Warioba: Taasisi za Kiselikali, ikiwemo ofisi ya waziri mkuu walipendekeza serikali 3

Warioba: Taasisi za Kiselikali, ikiwemo ofisi ya waziri mkuu walipendekeza serikali 3

Maswala

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2011
Posts
560
Reaction score
225
Mchanganuo wa takwimu hizi unaonyesha kuwa kwa upande waTanzania Bara, 13% walipendelea Serikali moja, 24% walipendekeza Serikali mbili na 61% walipendekeza Serikali tatu. Kwa upande wa Zanzibar, 34% walipendekeza Serikali mbili na 60% walipendekeza Muungano wa Mkataba, na 0.1% (watu 25) walipendekeza Serikali moja. Aidha, taasisi nyingi kama vile vyama vya siasa, asasi za kiraia na jumuia za kidini zil ipendekeza muundo wa Serikali tatu. Baadhi ya taasisi za kiserikali, ama moja kwa moja au kwa tafsiri ya mapendekezo yao, pia zilipendekeza Serikali tatu. Kwa mfano, Baraza la Wawakilishi Zanzibar lilipendekeza kuwe po kwa mamlaka huru ya Zanzibar, mamlaka huru ya Tanganyika na mamlaka ya Muungano na iwekwe wazi maeneo, uwezo, nguvu, utendaji na mipaka ya kila mamlaka. Ofisi ya Waziri Mkuu imependekeza mfumo wa serikali tatu ili kuondoa kero za muungano. Aidha, Mamlaka ya Mapato Tanzania imependekeza kuwepo kwa Serikali tatu ili kutoa majibu ya kero zilizopo na kuleta utulivu zaidi ilimradi upangiliwe vizuri.

http://katiba.go.tz/attachments/article/186/HOTUBA YA MWENYEKITI 30 DISEMBA, (PDF).pdf (pg13)
 
Alafu kuna watu wanachezewa akili kuwa CCM haitaki serikaki 3, ile ni zuga tu ili ioneshe kuwa hata maoni ya CCM yalipingwa kwa hiyo rasimu haikuwa biased! Utaipingaje? Sasa unakuta gazeti limeandika kichwa kikuubwa cha habari CCM YADONDOKA SERIKALI 3. Akili ku mkichwa
 
Alafu kuna watu wanachezewa akili kuwa CCM haitaki serikaki 3, ile ni zuga tu ili ioneshe kuwa hata maoni ya CCM yalipingwa kwa hiyo rasimu haikuwa biased! Utaipingaje? Sasa unakuta gazeti limeandika kichwa kikuubwa cha habari CCM YADONDOKA SERIKALI 3. Akili ku mkichwa

Unajua hata mimi nashangaa kwa maana nimewasikia viongozi mashuhuri wa CCM wakikosoa vikali tume kuingiza serikali 3.
 
Back
Top Bottom