Warrant issued for Sudan's Bashir

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
Warrant issued for Sudan's Bashir
BBC News Online

The International Criminal Court has issued an arrest warrant for Sudan's president on charges of war crimes and crimes against humanity in Darfur.

Omar al-Bashir, who denies the charges, has previously said that an arrest warrant would have "no value".

Reports say Sudan's capital, Khartoum, was tense as people awaited the decision, with fears of unrest.

The UN estimates some 300,000 people have died and millions been displaced in six years of conflict in the region.

The spokeswoman for the court in The Hague, Laurence Blairon, said the violence was the result of a common plan organised at the highest level of the Sudanese government.

It is the ICC's first ever warrant issued against a sitting head of state.
 
Last edited by a moderator:
Amen! Next Mugabe then Both Raila and Kibaki!!
 
Amen,
Nashangaa kwa nini serikali yetu inamkingia kifua Bashir.
 
Labra na wale Wapemba wanaotaka kumshitaki Mkapa watapaya upenyo
 
sioni cha kushangilia hapo, ni sawa na Bush alivyovamia Iraq kwa lengo la kutetea wanaoteseka na kuuwawa, matokeo yake ni mauwaji yasiokwisha kila leo. kumkamata Bashir kutazusha vita vikali zaidi na uhasama utazidi kati ya Sudan ya kaskazini na Sudan kusini.
 
Hapana!

1. this will push back further the peace process in Darfur! May lead to more extremsm kwa jandaweed!

2. Hivi Hii Koti ni kwa ajili ya Afrika Tu? Kwa nini Waziri Mkuu Israeli asikamatwe over Gaza? Hata Bush wakiwepo Iraq commited serious crimes!

3. Way foward: hii issue itapelekwa UN Security Council..na China, Russia, Afrika and arab states watapinga na UK, France, na US wataunga mkono! then back to square One!

Hii Koti uliundwa kwa ajili ya matatizo Afrika na former Yougaslavia tu??

Hii koti can not dictate Afrivcan ways we do things! Is this not a new type of colonialism?
 
Vita ya Sudan vimechochewa na Bashir. Kusema kuwa kutolewa kwa warranty kutaongeza vita au kuzua vita kali kunaonyesha kutoelewa yale yanayoendelea Darfur. Bush hakuvamia Iraq kuwatetea wanaoteseka. Alivamia Iraq kumwondoa Saddam mamlakani. Bashir amekataa kukiri ukatili na unyama unaofanyika kila siku Darfur dhidi ya Waislamu weusi ili tu machotara wa Kiarabu au wenye asili ya Kiarabu wapanue himaya yao.
 
kwani sisi waafrika tunafanya vitu kwa vipi? What's African way? Mahakama ipo pale. Kama wengine hawapelekwi haina maana kuwa wengine wasipelekwe. Just like EPA/Twin Tower. Tunashangilia wale waliopelekwa pamona na kwamba big fish wanatanua tu.
 



Hii koti si kwa ajili ya waafrika bali ni kwa ajili ya wahalifu!

Kama hawa viongozi wetu wanajiona wako JUU YA SHERIA basi ngoja tusaidiwe kuwawajibisha maana sisi hatuwezi kuwawajibisha. Viongozi wetu wa Africa wamekuwa impossible! Ngoja waadabishwe!

HAKUNA CHA BUSH WALA ISRAEL HAPA. TWO WRONGS DONT MAKE IT RIGHT! Tuache kukimbilia uafrika hapa..haonewi mtu wala nini....BASHIR kaua millions of innocent Sudanese..in DARFUR AND THE SOUTH..LEO WANAFIKI WANAKUWA NA GUTS ZA KUMTETEA...

Mimi sifurahii BASHIR KWENDA THE HAGUE nafurahi kuona kwamba hata akiwakanyaga vichwani wananchi wake..kuna wanaume wana balls kama yeye watadeal naye!


Sasa hawa viongozi wengine wakae chonjo. You kill your own people at your own peril! Mzalendo, damu ya wananchi wanaokufa ni nyingi mno..na hakika nakwambia malipo ni hapa hapa duniani!

Hivi kwanza hiyi peace talks watu wanayoongelea Darfur ni ipi? eti itakwamishwa?..aende akakae lupango huko..aone jela kulivyo..yeye si alizoea kuwaweka wengine? Kwanza ana bahati jela za ulaya kuna TV na magazeti...huko Darfur..jela ni ahera..
 
Bwana Bashir amesahau kwamba hivi sasa kuna orodha ya mashahidi wengi tu ambao ndio wataomdidimiza kwa wimbi la ushahidi vikiwemo vitendo vya kuua watoto wadogo wasio na hatia.

Pia Bashir anatuhumiwa kutoa maagizo ya kuuwawa kwa watu wengi wenye asili ya Afrika katika eneo la Darfur.

Kwa hio umefika wakati muafaka kumfikisha mahakamani bwana Bashiri na ajibu tuhuma.
 
Hata Mkapa aliwaua wapemba na kufukia watu huko bulyangulu,shinyanga naye atafuta tu kujibu unyama huo.Watanzania kamwe tusiwatetee wahalifu kwani ni wengi sana nchini kwetu kutokana na matumizi mabaya ya madaraka.
 
Perpective: who is calling who mhalifu? Yaani Mzungu has more right kumuita african mhalifu than Arabs? Why?

Why double standards?

Kwani Afrika ndo kuna wahalifu tu?
 
Perpective: who is calling who mhalifu? Yaani Mzungu has more right kumuita african mhalifu than Arabs? Why?

Why double standards?

Kwani Afrika ndo kuna wahalifu tu?

Does it matter who's calling who a mhalifu as long as s/he is a mhalifu?
 
Huu ni mpango wa nchi za magharibi tu kuonyesha ulimwengu kuwa "uhalifu" wa kivita duniani ni shughuli ya nchi zingine -- sio wao -- na ambazo wanaziona kama vile hazijastaarabika. Mtu wa kwanza kutolewa warrant na mahakama hiyo angepaswa kuwa Bush kwa kufanya uvamizi Iraq na kusababisha vifo vya watu wasiokuwa na hatia zaidi ya milioni moja na wengine milioni mbili kuhama makazi yao na/au kukimbilia nchi za nje.

Tusisahau kuwa karibu dunia nzima ilipinga uvamizi huo kwani haukuwa na sababu yoyote. Sababu zilizoainishwa na Bush zilikuwa za kupikwa kama vile ilivyokuja kudhihirika baadaye. Kwa nini tunasahau? Kwa hivyo Bush na Blair kimakusudi wakauzunguka Umoja wa Mataifa na kufanya uvamizi.

Mahakama hiyo haikuona yote hayo kwa sababu kulikuwa hakuna taifa miongoni mwa yale yanayoendelea kuweka msukumo kwa mahakama hiyo kutoa warrant kwa Bush na chinjachinja wenzake Tony Blair na Dick Cheney.

Hivi hamushangai hata kidogo kwa nini Marekani haikutia sahihi mkataba ulioanziosha Mahakama hiyo? Ni kweli Marekani ilishiriki (wakati wa Clinton) mchakato wa kuanzisha kwake lakini alipoingia Bush aliutupilia mbali mkataba huo na ilikataa kutia sahihi.Na hapo hapo akatangaza kuwa ole wake nchi yoyote ile itakayomkamata askari au raia yeyote wa Marekani na kumpeleka kwenye Mahakama hiyo. Ilikuwa ni dharau kubwa kwa Dunia iliyokuwa inajaribu kukuomesha vitendo vya kuhalifu wa kivita vinavyofanywa na taila lolote bila kujali hadhi au utajiri wake.

Kumbe kukataa kwa Bush kutia sahihi mkataba wa Mahakama hiyo kulikuwa kwa sababu maalum, kwamba Bush mwenyewe alikuwa anatarajia kufanya uhalifu mkubwa hapa dunuiani tangu wakati wa utawala wa Pol Pot wa Cambodia katika miaka ya 70. Jee Mahakam hiyo ambayo haitambuliwi na Marekani inaweza kweli kutoa waranti kwa Bush? Inaweza, lakini nani ataotao wazo, au msukumo hilo lifanyike? Viongozi wa nchi zet ni dhaifu sana mbele ya mataifa haya makubwa

Inakadiriwa waliokufa Darfur kutokana na uhalifu huo wa Bashir wanafikia laki 3idadi ambayo ni ndogo sana ukilinganisha wale waliokufa Iraq. Tuisisahau kuwa Marekani ina undumila kuwili. Hebu ona: Kule Darfur inawaunga mkono wapiganaji wanaopigana dhidi ya Serikali ya Bashir, na ingependa sana serikali hiyo iangushwe. Lakini kule Chad, nchi inayopakana na hilo jimbo la Darfur, Marekani hiyo hiyo inaiunga mkono serikali ya Chad dhidi ya waasi wao ambao mwaka juzi almanusura waiangushe serikali ya Idris Deby.

Tatizo hapa ni jinsi tunavyopumbazwa na nchi za Magharibi. Chad na eneo la Darfur lina utajiri mkubwa sana wa mafuta ambayo Marekani inayamezea mate. Kule Chad tayari iko serikali muafaka inayokidhi matakwa ya Marekani kuchota mafuta, lakini Sudan si hivyo, kwani ingependa Bashir aangushwe, ije serikali "muafaka" itakayoiuzia Marekani mafuta.
 
Last edited:
Hapana,
Wale mnaosema kuwa ni Waaafrika tu mnakosea. Wale viongozi wa Kiserb walioshiriki katika mauaji pia wamefikishwa huko.
 

Mkuu nimekuelewa ila nataka nikambie kitu kimoja tu.

Suala la kuua kwa malengo ni tofauti na kuua kwa kukusudia. Unapoua kwa malengo kama wafanyavyo nchi za magharibi ni tofauti na mauaji yaliofanyika kule Serbia au yafanywayo kule Darfur.

Nchi za magharibi tubishe tusibishe zimetuzidi kwa kila kitu na hilo halipingiki sasa kwanini tusikubali tu suala hilo?

Kwa hio kama wao wana nyenzo na wanataka kitu ni lazima watapata na endapo kutakuwa na "irresponsible resistance" njia za vita ndio suluhu yenyewe.

Mifano ya waliokubali hali hio ipo na Muammar al-Ghaddafi ni mmoja wao, amekubali kuwa yeye hatafanya tena mipango ya ugaidi na sasa Libya imefutwa katika orodha ya nchi zinazofadhili ughaidi na pengine hatujui kama Mugabe nae atakubali.
 
Last edited:
nitafurahia sana siku nikisikia huyu gaidi namba wani wa afrika ambaye ni rafiki wa kikwete, atakapo kamatwa na kuwekwa ndani. siku hiyo nitafanya hadi sherehe.
 
super hiyoo, walichelewa sana kuianzisha koti hii, manake ingewakumba akin a mobutu, idd amin, bokasa nk, wanaotaka iwakamate wazungu ni lini uliwahi kuwasikia madikteta kama bashir, bokasa, au vinganganizi wa madaraka kama museveni, kibaki kule ulaya au amerka? hiii koti itatusaidia sana kukomesha hawa watawala wetu, wananweza wasipelekwe kisutu lakini wakimwaga tone la damu ni lazima waende the hague.

mkapa ni lazima aende pale kwa yale mauaji ya wapemba
 
kuna watu hamnazo.......eti wanasema El bashiri kakamatwa kisa muisilamu.....yaani..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…