Wasafi Festival:Tarehe 26 Desemba nchini kenya tamasha la wasafi litakuepo kulikoni tena?

Freelancer Wakala

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2016
Posts
1,193
Reaction score
828
Habari ndugu na wadau mbalimbali wapenda burudani,
Ebu tueleweshane maana mambo yanaenda tofauti kwa msanii Nasibu na Basata.
Basata wametoa tamko la kutofanyika kwa tamasha la Wasafi Festival ndani na nje ya nchi.
Vipi tena hilo tamasha kufanyika nchini Kenya tarehe 26 desemba?
Maana uko atakuepo Morgan Heritage lile kundi la Jamaica la reggae walioshinda Tuzo za Grammy.
Mbona kuna sintofahamu hapa?
 
Nyimbo ya nyegezi ilipigwa marufuku within our country lakini nchi za jirani kama kawa, na kama walimzuia aisifanye matamasha basi ni ya ndani hayo ya nje ya nchi watajibeba
 
Hapo ni Serikali vs Wasafi. Mambo ni motooooooo kitu cha fireeee
 
Hata mlezi wao kawa mkimya maana yake imetoka oda ili wajifunze kuheshimu
 
Kama Diamnond akifanya tamasha lolote inabidi awekwe ndani huyo mtu kwa kudharau amri halali ya serikali(BASATA).
 
Umesikiliza vizuri adhabu aliyopewa juzi?
Kasikilize tena!

Hakuna kufanya tamasha lolote ndani na nje ya nchi!
Nyimbo ya nyegezi ilipigwa marufuku within our country lakini nchi za jirani kama kawa, na kama walimzuia aisifanye matamasha basi ni ya ndani hayo ya nje ya nchi watajibeba
 
Tanzania full kukomoana wangemfungia ndani tu wakamwacha akafanye huko maana kama serikali ya Kenya haijaona tatizo sisi kwanini tuone tatizo. Yani sisi full mitima nyongo sasa wanadhani wanamkomoa jamaa dah kuishi tanzania sometimes yataka moyo. Lakini na yeye ngoja aonje joto la jiwe maana wenzake walivyonyimwa uwanja alichekelea sana wazi wazi mwisho wa siku Mungu ni wetu sote
 
Karma is an ugly bitch
 
Basata inamamlaka nchini tu
 
Diamond keshakula advance ya watu (viingilio) na ratiba ilishakuwepo kabla ya basata kumfungia...sasa asipoenda kufanya show hiyo hela BASATA watawalipa wao mashabiki? na gharama nyengine za maandlizi je?
 
Diamond keshakula advance ya watu (viingilio) na ratiba ilishakuwepo kabla ya basata kumfungia...sasa asipoenda kufanya show hiyo hela BASATA watawalipa wao mashabiki? na gharama nyengine za maandlizi je?
Atalipia yy mwenyewe aliyechukua advance...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…