Wasafi vs Fiesta, :Fid Q Awapiga dongo Wasafi festival "acheni ufala"

Kwanini usiseme kuwa hao wingine pia walishindwa vigezo na masharti hapo Clouds?
Kama unasema kuwa Clouds ni wanyonyaji Kwanini usiseme kwa hata hao Wasafi ni wanyonyaji pia kwa sababu wote wanafanya yaleyale tu?
Kwani fid q alishawai kuja wasafi hadi aseme n wanyonyaji... hapo kashoboka tu kutafuta sifa kwa kina mawingu
 
huyu na yeye anazeeka, hajitambui..! Sijui alichelewa wapi
 
Wasanii watanzania hawajui wanataka nini na wanao jijua wanataka nini wakiwa na mawazo mbadala ya kujitegemea wanaoneka maadui, kama hiyo comment kaandika fid q basi nishamshusha thamani, ila akae akijua hii ni dunia ya ushindani, wao wenyewe CMG wana kauli yao ya tunakufungulia dunia uwe unachotaka, sasa WCB wametaka kuwa kama wao sizani kama wanakosa.
 
Wasanii wanatakiwa kula pande zote
 
Mwisho Wa siku hao wote wafanyabiashara tu, acha nikafanye yangu mie....
 
Huyu jamaa n fala... hajui hawa mamawingu watamtumia baadae watamtupa kama bigiji... amuulize ruby, konki, jay dee na wengine kibao wako wapi, yaani laki tatu tu inamfanya anyee kambi?
Nyie vijana wa leo mnachekesha....hao mawingu ndio ilikuwa barabara ya hao mnaowatukuza sasa, huyo fid q toka 2007 namuona anashiriki matamasha ya fiesta,.kinachofanywa na media zingine kuandaa matamasha ni kizuri ila kudharau ulipopita ni ujinga, maana unaweza ukapita tena kwasababu hakuna njia ya peke yako.Ulishawahi kujiuliza kwanini njia za mto sio rahisi kubadilika?.
 
Uko sahihi fiesta ni kongwe kwenye burudani ila wengine kuanzisha isiwe chuki au ubaguzi na wengine kujiona Bora , iwe chachu ya kuongeza ubunifu na maslahi kwa wasanii
Kuwe na health competition
 
Uko sahihi fiesta ni kongwe kwenye burudani ila wengine kuanzisha isiwe chuki au ubaguzi na wengine kujiona Bora , iwe chachu ya kuongeza ubunifu na maslahi kwa wasanii
Kuwe na health competition
CMG hawataki health competition na ndio maana walimfanyia Majizo kitu kibaya sana,kipindi kile ameaandaa tamasha lake kubwa aliwaita Joe Thomas,Busy Signal,T-Pain jamaa kalipigia promo mwezi mzima,imebakia wiki moja CMG wanatangaza kumleta Fat Joe na Eve alafu tarehe ile ile,tofauti venue baadaye akina Gerald na KIbonde walimponda sana Majizo (kimafumbo) na ndio maana haya maneno mimi niliyategemea.
 
Ngoja nisiseme chochote kwanza nikahakikishe kama kweli kasema
 
Kama jamaa ksema hivyo kazingua na amejikosesha pesa kwa ujinga wake ila msanii mkubwa kama fid huwezi kumlipa laki tatu
 
Sasa wew umetaka aseme nini? Wakati teye anapata ugali kupitia Clouds
 
Sasa nyie mnamponda jamaa kusema hivyo tu, lakini mnaona sawa mtu kuimba nye.ge nye.ge au ipake mate. Jamaa yuko kazini binafsi naona ni sawa kwavile kalipwa kutoa tangazo hilo
 
Ni ujinga Fid Q msanii anayeaminika na wengi kwamba ni 'akili kubwa' kukubali kutumika kwa style hii kana kwamba yeye ni sehemu ya Fiesta, ajue yeye ni msanii tu hana nafasi CMG so asijifunge, kuwepo kwa matamasha mengi ni fursa ya kupiga hela so akiweka bifu upande mwingine uoni kwamba anajiharibia?
 
Hii ni kufurahaisha na kunogesha matamasha tu do not take it personal, kama ambavyo wasafi wamemtumia dudubaya kuwaponda clouds kuna kosa gani wakimtumia fid . Na uzuri hajataja ni tafsiri tu ya mashabiki huenda hata hakumaanisha mashabiki walicho tafsiri, ukizingatia Fid sidhani kama ana ugomvi na Diamond ndiyo maana diamond alivyo mcheki wafanye remix ya fresh alikubari kiroho safi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…