Wasafirishaji mnafanyaje hii biashara??

Just imagine milioni 700+ afu unapakia abiria 50 kwa elfu 50 Dar Kahama, unalipa wafanyakazi, engine kubwa inanyonya mafuta kama walevi wa KASKAZINI.

Bado ukodi ofisi, trafiki, Latra etc!!
Mnapigaje hapo???View attachment 2854877
50x50,000 = 2,500,000 hii ni kwa siku.

2,500,000 x 280 = 700,000,000 (tume assume lina fanya kazi siku 280 tu kwa mwaka).

Chukua 700,000,000 x miaka 3 unakua hujarudisha hela ya kununulia? Yani hapo weka na hizo gharama zote kuanzia matengenezo nk nk!
 
-Hilo gari una uhakika wa abiria wa Kahama tuuu!
Jibu ni hapana. Hivyo,hesabu hiyo kwa siku huwezi kuipata.
-unajua maintenance ya gari?
-umeshaweka gharama utakazoibiwa?
Je, baada ya wiki likipata ajali?

Kwenye hesabu za biashara ukilenga faida bila kukumbuka na hasara utalia. Sema kwa hesabu zako,anaongezea kidogo anapata za mchina 2, hesabu itakayolala ndo hiyo hiyo
 
Bado hujaweka pesa ya mizigo.Hakuna mfanyabiashara anakubali kufanya biashara kama inaingiza hasara.
 
Hesabu zako ziko vizuri lakini huwezi toka Dar Asubuhi jioni ukafika Kahama
Bado kuna mafuta + vipuli
 
hiyo 50k umepigia anayopewa boss au nauli aliyokatiwa mteja? maana naonaga kama nauli ni 50 kuna hela kiasi ya mkata ticket (huku wanaita kyagora sijui vyagora[emoji23]) tufanye 5000 then kwa bosi inafungiwa 45,000
 
Nusu ya hiyo cash collection inaenda kwenye running cost. Tra,fuel,salary,tyre, servise etc.

sema wajanja wanaliuza baada ya muda flani.ukiliacha likuchokee linakula hela zako.sawa na biashara ya boda boda au taxi.

unapata profit on disposal,usipoliuza inakula kwako
 
Biashara ya Gari:

Phase One: Inaingiza: Haili kabisa(Garage)—Ndio kipindi cha kukusanya hasa hela. PROFIT 95%

Phase Two: Inaingiza: Garage kidogo—Bado unakusanya kingi, ila sio kama phase one. PROFIT 80%
Phase One & Two just two years.

Phase Three: Inaingiza: Inakula kiasi kikubwa (Garage 50-60% of Running Cost). PROFIT 40-50%
Huu ni mwaka wa Tatu.

Hapa unapeleka njia ya pori, inafanya kazi kiangazi tu sababu abiria ni wengi, hawachagui gari, ni wavumilivu kwa delays tofauti na wamjini, mizigo mingi na abiria unabeba upto 50% zaidi ya uwezo—hence big revenue; So cash flow ni kubwa. MAY to OCTOBER.

Business model hii ndio inafanya kampuni kama Allys imedumu sana kwenye biashara. Nguzo ya Allys ni upcountry routes.
 

imagine kama abood anapata 11,000×65 = 715,000/=, kwa trip moja Dar-Moro, sijui huwa basi moja linapiga trip ngapi, naona kama ni ndogo hiv.sijui wanafanyeje biashara kiasi kwamba utakuta pia ameagiza mabasi 20 mapya kwa mpigo..
 
imagine kama abood anapata 11,000×65 = 715,000/=, kwa trip moja Dar-Moro, sijui huwa basi moja linapiga trip ngapi, naona kama ni ndogo hiv.sijui wanafanyeje biashara kiasi kwamba utakuta pia ameagiza mabasi 20 mapya kwa mpigo..
Kuna possibilities hawa jamaa wanatakatisha fedha za madawa ya kulevya!!
 
Biashara ya mabasi ni biashara pasua kichwa kuliko zote.

Scandinavia iliyofanya Mapinduzi kwenye hii sekta ilikufa kifo Cha mende.

Hood imekufa.

Sumry chali.

Sauli yupo hoi siku zake zinahesabika, Achimwene got him in the headlock.

Dar express, Dar Lux, Rungwe waliokuwa powerhouse kwenye hii sekta wote wapo hoi. Etc etc

Turnover kwenye hii sekta ni kubwa mno. Kila miaka miwili wanakuja wengine na kupotea kama upepo household names.

Utasema usimamizi na sababu zote ila sio rahisi kusema hao wote hawajui wanachokifanya. Fanya hii biashara kama unataka kufukia pesa zako.
 
Msweden tofauti na mchina ...Mchina miaka 2 tu lipo nyang'anyang'a ila scania linapiga kazi zaidi ya miaka 10 ..service tu
 
Gari mpaka ipate ajali, ajali unajua maana yake, unajua maana ya bima kubwa kwenye gari kubwa?
Hamna mfanyabiashara anawaza kuibiwa. Ndugu huna biashara nn, jamaa mbona kakupigia hesabu nzuri sana. 280 days only. Unataka hesabu gani tena?
Biashara hyo ni kama zingine. Risks ni matarajio tu, na hamna mtu anatarajia. Kama mmiliki wa bajaji ndio hesabu anapiga huyo, ila kwa level yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…