Wasanii bongo zero kichwani

patrickkkkky

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2014
Posts
468
Reaction score
286
Nilikua nafuatilia Sporah show ya mdada Recho a.k.a Recho mapenzi, yaani hana answering skills kabisa, hajui kujieleza, anauliza maswali mengi kama yeye ndio ana host show.

Nilipochoka ni pale Sporah alipomuuliza tofauti na mziki unapendelea kazi gani nyingine akajibu KWENDA BEACH! wtf??

Hawa wasanii wetu kichwani hamna kitu. Ningekua host ningemfukuza, kama mbaya acha iwe mbaya.
 
ha ha ha... Hata walioenda shule wengi hawajiwezi.
 
Anatia huruma sana ukimsikiliza kwa makini unaweza ukatokwa na machozi kwa namna alivyo empty-headed.
 
Ktk msiba wa KANUMBA pale SINZA, muda wote wa msiba STEVE NYERERE alikuwa ktk hali yake ya kawaida tu, mcheshi kwa sana! Ghafla alipoingia JK, steve Nyerere akaanza kuangusha kilio! Kilio cha zaidi ya mtu aliefiwa na ***** ama mke! Steve Nyerere akaanza kugalagala, mbele ya rais! Akalia!
Akalia!
Akagalagala!
Akazimia!
Mara baada ya rais kuondoka, akarudia hali yake ya kawaida!
Kuanzia pale nikawa Nimeshaelewa kuwa ubongo wa wasanii wengi sana hauko sawa!
 
mi nilikuwa namsikiliza Mtitu na Pastor Miyamba kwenye kipindi cha Radio One juzi jioni daah hawa wasanii hamnazo kabisa kujieleza hawawezi zaidi ni kulalamika tu. TOPIC ilikuwa Kampuni ya STEPS kuamua kuuza DVD Original kwa Tsh. 1000/= sasa wao hawataki mtangazaji anawauliza watoe sababu ya kwa nini STEPS asiuze DVD kwa 1,000/= wanabaki kulia lia tu. Hebu achene woga wekeni Filamu zenu kwenye mitandao kama YOUTUBE na mingineyo mpate kujulikana na followers wa kutosha kama ina ubora utapata kazi za maana zaidi (Matangazo ya biashara) hata kuitwa kucheza filamu zaidi ndani na nje ya nchi PUNGUZENI KULALAMIKA.
 
mkuu nini kinaweza kua tatizo?

Mkubwa zipo nyingi, kama vile
*ulimbukeni
*kuiga maisha ya sio yao
*ulevi na bangi
*matumizi ya madawa ya kulevya
*kuw na ma team ya ushindani, mtu anaongea ujinga tu hata kama ukweli anaujua
*management mbovu, msanii haandaliwi nini aongee
*etc.

Nilipata chance ya kumsikia GK ktk kipindi cha Mkasi, nilitaka zima tv. Anadai ana masters lakin kujieleza F.

WABADILIKE.
 
nini maana ya "kazi"
 
sikumbuki kama ni wolper au uwoya aliwahi kusema kuwa hawez kuigiza nafasi ya msichana wa kazi za ndani katika filamu yoyote....nikajiuliza hivi hajaangalia muvie ya maid in manhatan ya j lo alioigiza kama bar maid?? au sinema ya smith ya pursuit of happiness jins smith alivoigiza kama mtu wa chini sana??? na hao ni mastaa wakubwa duniani lakin kunako kazi wanaigiza nafasi yoyote tu mrad wanaitendea vyema..sasa wewe msanii wa bongo una nini?? daaahh hekima kitu muhimu sana aisee
 

Mbona unageneralize ? Mmoja tu assbabibishe wote waoze?
 
Inabidi sasa jamii baada ya kutambua hili muanzishe course special kwa wasanii wetu maana badae wasije kututia aibu katika nchi za watu
 

Hahahahahaaaaa daah....
 

Ni Aunty Ezekiel. Ila baadaye alikuja kuigiza kama MREMBO KIKOJOZI!Sasa sijui kipi bora kati ya house girl na mrembo kikojozi.
 

Kumbe huyu jamaa nae ni empty hivi…?
 
Anatia huruma sana ukimsikiliza kwa makini unaweza ukatokwa na machozi kwa namna alivyo empty-headed.

Alikua akiulizwa swali kwa kingereza anatoa macho tu hadi aulizwe tena kwa kiswahili ndio aanze kujiumauma.
Hii ni moja kati ya interview mbovu kabisa nilizowahi kuziona!
 
Mbona unageneralize ? Mmoja tu assbabibishe wote waoze?

hiyo kwenye red ni ishara tosha.

sentensi ilipaswa kuwa "Mmoja tu hawezi kusababisha wote waoze au mmja tu ndiye asababishe wote waoze?"
 
hiyo kwenye red ni ishara tosha.

sentensi ilipaswa kuwa "Mmoja tu hawezi kusababisha wote waoze au mmja tu ndiye asababishe wote waoze?"

Jamaa amekosea uandishi tu...mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…