Wasanii wa kizazi kipya waanza kampeni Kura ya "NDIYO" Katiba mpya Zanzibar

Wasanii wa kizazi kipya waanza kampeni Kura ya "NDIYO" Katiba mpya Zanzibar

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2010
Posts
1,710
Reaction score
3,681
Leo katika Uwanja wa Aman Zanzibar,makamu wa kwanza wa Rais Balozi Seif Idd amezindua kampeni rasmi ya wanamuziki wa kizazi kipya watakaozunguka Tanzania nzima kuhabarisha na kuhamasisha upigaji wa Kura ya "NDIYO" kwa rasimu ya katiba iliyopendekezwa,akiongea na hadhara ya watu ktk uwanja wa Amani,Seif amewaambia Wazanzibar waipigie katiba inayopendekezwa Kura ya "NDIYO " kwani ina mambo mengi inayowafaa na kuwaletea maendeleo wao na vizazi vyao.

Akiongea kwa niaba ya wasanii waliojiunga kuipigia kampeni rasimu ya katiba mpya,NIKI awA KWANZA amesema kwa muda wa Miaka 50 toka nchi hii ipate Uhuru wasanii hawakuwahi kutambulika ktk katiba na wala kazi zao hazikuweza kutambulika kisheria,anasema katiba iliyopo ilitambua haki za Mali inayohamishika na Mali isiyohamishika lkn haikutambua mali isiyoshikika,wao kama wasanii wamejitahidi kushinikiza kuwepo na utambuzi na urasimishaji wa haki za Mali zisizoshikika kama muziki wao wa kizazi kipya,hivyo kuwasihi Wananchi wa Zanzibar waipigie Kura ya ndio katiba inayopendekezwa sababu imegusa maslahi mapana ya Watu wa makundi yote.Nikki wa Pili amemwambia Balozi Seif kuwa tasnia ya Sanaa ya muziki wa Kizazi kipya Tz ina mtaji wa Watu milion kumi,hivyo watatumia uwingi wao na nguvu yao ya kiushawishi kwa Vijana kushawishi waipigie Kura ya NDIYO katiba inayopendekezwa,kwani katiba hii imebeba matumaini na mustakabali mzuri wa Taifa na watu wake.

Wasanii waliohudhuria ufunguzi huo ni Niki wa Pili,shilole,Peter Msechu,AT,Barnaba Boy n.k...kampeni hiyo itakuwa ni ya nchi nzima ili kuwahamasisha Watanzania kupiga Kura ya NDIYO na kuepukana na maneno ya wanasiasa na viongozi wa dini walioanza kujitokeza kuhamasisha kuikataa na kuipigia Kura ya HAPANA katiba pendekezwa.Kongamano hili lilionyeshwa moja kwa moja na TBC1 na ZBC1 ImageUploadedByJamiiForums1426430537.853023.jpgImageUploadedByJamiiForums1426430564.032478.jpgImageUploadedByJamiiForums1426430577.975379.jpg
 
Wasanii wamekalia kidole cha kati pamoja na waliowatuma.
 
Wanadhani hao wasanii wanaweza kushawishi mustakabali wa taifa hili kwa kuimba nyimbo tu! Never. Hatudanganyiki
 
Daaah,naamini sasa tumbo linanguvu kuliko ELIMU. Sikutegemea mtu kama NIKKI WA PILI na elimu yake yoooote + ujana wake,ashabikie katiba hii mfu!!
 
leo katika uwanja wa aman zanzibar,makamu wa kwanza wa rais balozi seif idd amezindua kampeni rasmi ya wanamuziki wa kizazi kipya watakaozunguka tanzania nzima kuhabarisha na kuhamasisha upigaji wa kura ya "ndiyo" kwa rasimu ya katiba iliyopendekezwa,akiongea na hadhara ya watu ktk uwanja wa amani,seif amewaambia wazanzibar waipigie katiba inayopendekezwa kura ya "ndiyo " kwani ina mambo mengi inayowafaa na kuwaletea maendeleo wao na vizazi vyao.

Akiongea kwa niaba ya wasanii waliojiunga kuipigia kampeni rasimu ya katiba mpya,niki awa kwanza amesema kwa muda wa miaka 50 toka nchi hii ipate uhuru wasanii hawakuwahi kutambulika ktk katiba na wala kazi zao hazikuweza kutambulika kisheria,anasema katiba iliyopo ilitambua haki za mali inayohamishika na mali isiyohamishika lkn haikutambua mali isiyoshikika,wao kama wasanii wamejitahidi kushinikiza kuwepo na utambuzi na urasimishaji wa haki za mali zisizoshikika kama muziki wao wa kizazi kipya,hivyo kuwasihi wananchi wa zanzibar waipigie kura ya ndio katiba inayopendekezwa sababu imegusa maslahi mapana ya watu wa makundi yote.

Wasanii waliohudhuria ufunguzi huo ni niki wa pili,shilole,peter msechu,at,barnaba boy n.k...kampeni hiyo itakuwa ni ya nchi nzima ili kuwahamasisha watanzania kupiga kura ya ndiyo na kuepukana na maneno ya wanasiasa na viongozi wa dini walioanza kujitokeza kuhamasisha kuikataa na kuipigia kura ya hapana katiba pendekezwa.kongamano hili lilionyeshwa moja kwa moja na tbc1 na zbc1View attachment 234839View attachment 234840View attachment 234841

safi sana wapeni vidonge vyao hao wasioelewa kuhusu katiba inayopendekezwa, coz imetulia sana.
 
Kumbe ndio naelewa kama hujiamini unaweza kugengendwa bila kujali ww ni ke ama me pumbuavu zao yaani tunawasapoti.na wao wanasapoti ujinga watapotea kama malow hivi yuko wapi cjamwona kwenye hii rist
 
watu wameenda kupata burudani......
 
Basi wamechemka na ndio maana wameanzia Zanzibar maana ni kugumu sana kwao walioudhulia wenyewe wachache aibu yao
 
Wasanii VS maaskofu ,ha ha ha ,mbona patanoga mwakahuu,hadi tutashuhudia alex malasusa akikata mauno kuhamasisha kura ya hapana kwa katiba mpya.
 
Hawa wasanii inabidi waonyeshwe nguvu ya umma wakiwa jukwaani.
 
Kutokana na mpasuko ninao uona ulioletwa na mchakato wa katiba mpya....ningeshauri serikali isogeze mbele muda wa upigaji kura ili elimu zaidi itolewe kuhusiana na katiba inayopendekezwa ili wananchi wapate kuielewa vyema katiba kabla hawajaamua kupiga kura ya ndio au hapana....
 
Daaah,naamini sasa tumbo linanguvu kuliko ELIMU. Sikutegemea mtu kama NIKKI WA PILI na elimu yake yoooote + ujana wake,ashabikie katiba hii mfu!!

mwenzenu Nicki wa Pili kaisoma na kaielewa na ndo mana kafanya hivyo. kazi kwenu nyie mnaobaki kulaumua pasipo kuisoma, kwanini mnalaumu wakati hamjaisoma na kubaini uzuri ama mapungufu mkaja na hoja?
 
Basi wamechemka na ndio maana wameanzia Zanzibar maana ni kugumu sana kwao walioudhulia wenyewe wachache aibu yao


7.jpg



IMG_6266.JPG

IMG_6281.JPG

Asee hata mimi naona walikuwa wachache....Hahahahaha watu bwana kwa kusikia ulizia waliohudhuria
 
Back
Top Bottom