Wasanii wajitambue na wajue kuwa wao ni vioo vya jamii

Wasanii wajitambue na wajue kuwa wao ni vioo vya jamii

said sabari

Member
Joined
Jan 26, 2016
Posts
26
Reaction score
32
Karne hii baadhi ya wasanii wanajichetua mno maadiri ya mtanzania miaka 10 ijayo sijui itakuaje inasikitisha sana...
 
Nadhani tatizo halipo kwa wasanii bali kwenu mnaowaona wao ni wa kuigwa kwakuwa tu "Ni watu maarufu"

Kioo kazi yake ni kuonyesha taswira, na kusema msanii ni kioo cha jamii inamaana tunapowaangalia wasanii tunapata kuona mazuri na mabaya ya jamii yetu..

Sidhani kama kuna kioo unachoangalia kinachokuonyesha upo safi usoni na kuzificha chunusi na michirizi wakati ipo..

Ndio maana kutofautisha viumbe wengine na binadamu, MUNGU ametupatia "akili na utashi" tuyatambue mazuri na mabaya kabla ya kuamua kuyafuata, kwahiyo kazi kwenu mnaoangalia "Gigy Money" kafanya nini ili muige...!!
 
Maadili peleka kwako na familia yako! Period!!!

Hata tukisema watz waimbe na gauni za ubatizo ilhali watoto wenu wenyewe wanaexposure na kina Nick Minaj bado haitasaidia kitu.
 
Unajua kazi ya kioo ni kuakisi na sio kuleta taswira mpya.unayoyaona kwa wasanii ndio hali halisi ya wanajamii huku mtaani.kama huamini tembea usiku wikiend utaelewa
 
MSANII SIO KIOO CHA JAMII NA HAWEZI KUWA KIOO CHA JAMII!.......isipokua SANAA NI KIOO CHA JAMII as what is portrayed through it kinaweza kuakisi hali halisi ya jamii husika,iliopita,ya sasa au ya baadae!WASANII NI WABEBA KIOO TU!MSIWAPOTOSHE WALA KUPOTOSHANA.msanii ni sehemu ya jamii na anachowasilisha kwenye sanaa yake kinaweza hata kumuhusu yeye mwenyewe.anabeba kioo lakini YEYE SIO KIOO!Please....
 
Nadhani tatizo halipo kwa wasanii bali kwenu mnaowaona wao ni wa kuigwa kwakuwa tu "Ni watu maarufu"

Kioo kazi yake ni kuonyesha taswira, na kusema msanii ni kioo cha jamii inamaana tunapowaangalia wasanii tunapata kuona mazuri na mabaya ya jamii yetu..

Sidhani kama kuna kioo unachoangalia kinachokuonyesha upo safi usoni na kuzificha chunusi na michirizi wakati ipo..

Ndio maana kutofautisha viumbe wengine na binadamu, MUNGU ametupatia "akili na utashi" tuyatambue mazuri na mabaya kabla ya kuamua kuyafuata, kwahiyo kazi kwenu mnaoangalia "Gigy Money" kafanya nini ili muige...!!
Nimekumbuka mjadala mmoja humu kama sio mwaka jana ni mwaka juzi. " Msanii kioo cha jamii" inatafsiriwa kimakosa siku zote. Labda hawajui kazi za kioo.
 
Nimekumbuka mjadala mmoja humu kama sio mwaka jana ni mwaka juzi. " Msanii kioo cha jamii" inatafsiriwa kimakosa siku zote. Labda hawajui kazi za kioo.

Kweli, wengi tunataka kugeuza maana kwamba kioo (msanii) kionyeshe mazuri tu na si kila kilicho mbele yake (jamii)
 
Back
Top Bottom