Huu mfumo upo Dunia nzima.
Kuna baadhi ya vitu unapotaka kuvifanya inabidi usogee kwenye eneo ambalo ndo kitovu (hub) cha vitu utakavyo kuvifanya, ili iwe rahisi kupata kile unachokitaka kwa muda husika.
Why Dar-es-Salaam??
Sabb Tanzania kwetu hapa, DSM ndo kitovu cha Biashara za mambo ya Viwanda vya Burudani (Entertainment Industry)..
DSM ndo walipo Mapromota wazuri wa Muziki. (promo & marketing ni muhimu sana ktk muziki, usione tu miziki inaenda redioni tu, muziki mgumu sana).
Pia DSM ndo walipo watu wenye connections za huu Muziki wa Tanzania. (Muziki unahitaji sana "Connections")....
Alafu pia DSM ndo nyumbani kwa MEDIA HOUSES zenye USHAWISHI na NGUVU katka Kiwanda cha Burudani Tanzania (TV & Radio Stations, Online Media, Magazeti ya Burudani etc.)..
Ukishaiteka DSM Kiburudani tu basiiii ni rahis kufahamika Nchi Nzima ya TANZANIA.
Na ukishafahamika nchi nzima ya TZ ktk muziki basi automatically hata nchi za UGANDA na KENYA pia watakufahamu tu.
Narudia Tena huu Mfumo Upo Dunia nzima..
TEKNOLOJIA:-
Mfano: MARK ZUCKERBERG wakat akiwa ndo anaanzsha KAMPUNI YA FACEBOOK (inayomiliki FB, Messenger, WhatsApp na Instagram) ilimlazimu kuhama kutoka JIMBO LA MASSACHUSETTS (ambko alkuw aksoma Chuo) na kuhamia JIMBO LA CALIFORNIA (Silicon Valley) Sababu CALIFORNIA ndo kitovu (hub) cha Mambo ya Teknolojia ya Computer na Internet kwa USA...
Na pia hapo SILICON VALLEY ndo inakuwa rahis kutafuta Deals na Wawekezaji wa Biashara za Teknolojia ya COMPUTER/SOFTWARE, INTERNET na SEMICONDUCTOR....
Na pia mambo yote muhimu ktk kuendeleza kampuni za Teknolojia kwa USA yanapatkana hapo kirahisi....
Na ndo sabb asilimia kuuuuuubwaa ya Makampuni yote makubwa ya Internet, Semiconductor na Software nchini USA yapo California (sehem moja inaitwa Silicon Valley)
Mfano: GOOGLE (YOUTUBE, ANDROID), SNAPCHAT, DROPBOX, TWITTER, HP, APPLE (Wazee wa iPhone, iPad, Macbook), UBER, AIRBNB, SALESFORCE, PAYPAL, eBAY, AMD, NVIDIA, INTEL, FACEBOOK (WhatsApp, Instagram), ORACLE, IBM, VERIZON, YAHOO!, TESLA MOTORS, etc... Yooooooteee hayo HeadQuarters zao zinapatkana California - Silicon Valley.
Hayapo California kwa bahati mbaya HAPANAAAA, Bali yapo hapo NI KWA SABABU HAPO SILICON VALLEY NDO KITOVU cha Teknolojia kwa Marekani, na wengi wanaoanzsha makampuni yao wakt bado yakiwa machanga huenda hapo kwa sabb maalum kujaribu kutafuta Deals zitazofaniksha dreams zao,
sabb hapo ndo kitovu na itakuwa rahis wao kufikia kile wanachokitaka...
ELON MUSK (Founder of TESLA MOTORS and SPACE "X") ilimlazimu tu kuhama nchi yake alipozaliwa ya AFRIKA KUSINI na kwenda CANADA na baadae MAREKANI ambako ndo ilikuw ndo anapataka ili kuifanikisha ndoto yake ktk Teknolojia.
NB:- Tesla Motors wale wanaotengeneza Gari za Umeme, gari zisizotumia mafuta (Petrol, Diesel).
SOKA:-
Hata CRISTIANO RONALDO ilimlazimu tu kuhama SPORTING LISBON na kwenda Uingereza (ktk club ya MAN UTD) sabb sio kufata kwenda Mijini kushangaa Maghorofa HAPANAAAA bali kuanzia pale ingekuw rahis kw yeye kufika alpotaka REAL MADRID.
LIONEL MESSI..
Hata MESSI naye kuhama Bara la AMERICA KUSINI kwenda ULAYA, sabb sio kushangaa maghorofa au kwenda mjini LA HASHAaaa! Bali ni ili awe ktk kitovu cha Soka LA Juu Duniani. (na ndo ilvyo hivo, soka kwa sasa, SOKA LA ULAYA ndo kitovu cha soka DUNIANI na the place to be km unataka kuwa up there juuuuu kisoka duniani)
NEYMAR JR, EDINSON CAVANI, ALEXIS SANCHEZ, THIAGO SILVA, DAVID LUIZ, PHILIPE COUTINHO, LUIS SUAREZ, YAYA TOURE, SAMUEL ETO'O, VICTOR WANYAMA, MBWANA SAMATTA etc...
Woteee hao sabb sio kushangaa mjini au maghorofa, bali ilibidi tu waende sehm ambyo ndo itafanya ndoto zao kutimia.
FILAMU:-
Mara nyingi sanaaa watu wamehama NEW YORK, MIAMI, ATLANTA, MICHIGAN, TORONTO, MUMBAI, NEW DELHI, LONDON, PARIS, CAPE TOWN, JOHANNESBERG etc. na kuanza kutafuta "Connections" za kuwapeleka JIMBO LA CALIFORNIA (HOLLYWOOD) ili tu waweze kutimiza ndoto zao za kuwa MOVIE STARS wakubwa duniani.
Simply because HOLLYWOOD ndo kitovu cha movies duniani, na pale ndo Kila kitu.
So you want to be up there basi muhimu uwe pale eneo husika...
HOPEFULLY sasa umepata idea ni kwa nn watu huwa wanahama hapa na pale ktk kufanikisha ndoto zao ngumu ngumu...
HALAFUUUUUU BY THE WAY..., SIO KILA SEHEMU DAR-ES-SALAAM NI TOWN KIVILEEE, [emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] MJINI NI "KARIAKOO", " KISUTU (Posta Kule)", "MNAZI MMOJA", " MAGOGONI"...
NA SEHEMU ZNGNE ANGALAU "MASAKI", " MSASANI", "OYSTERBAY", "UPANGA".
KWA MBAAALIII "MBEZI BEACH" NA "MIKOCHENI"...
ILA SEHM ZINGNE HAPANA AISEE [emoji2][emoji2] HONESTLY SPEAKING ZIPO BUSH NYINGIIII TU NDANI YA HAPA HAPA DAR-ES-SALAAM..
USWAZIIII HUWA NI BUSH TU... TOFAUTI NI KWAMBA NAULI KWENDA TOWN NDO SIO KUBWA KIVIIIILEEE....
ILA CHARACTERISTICS ZA USWAZI NI BUSH TU, NA DSM IPO MISWAZI MINGI SANA.
SIO MBAYA LAKINI SABB MWENYEWE NATOKEA USWAZI... [emoji41]
Tunacheki Movies zetu za Kutafsiriwa zile kwa Kiswahili flani Style za akina Lufufu, Mkandala,.. Movies za Low Quality kwny Display...
Tunacheza Vigodoro mulemuleee km watu wa Bush tu...
Maji ya shida, au pia maji ya chumvi kama bush tu..
[emoji41]
#NataniaTuLakini #PopoteKambi #UswaziNdoNyumbani #HomeSweetHome
#DareSalama #Daslamu
Natumaini mko vyema, kuna jambo linajitokeza sana kuhusu wasanii wamikoani sana sana hawa chipukizi kiukweli fikra zao zimetawaliwa nanini au sijui ndio menejimenti za muziki zimewasahau hawa vijana.
Unakuta msanii anauza kila kitu kwao na wengine utoroka kwa kuiba ilimradi tu akimbilie Dar es Salaam ambako wengi wanaamini kua usipogusa hilo jiji basi huwezi kutoka kimuziki.
Hivi wasanii wamikoani huko Dar kumewapa nini hasahasa kwani huwezi kutoka kimuziki bila kukimbilia Dar..?
Na wengineo mrudipo mikoani mnajiona tayari mastar kwakuvaa nguo mpya na baada ya wiki vumbi la mikoani laanza kukubukisha.
{KOKOTE KAMBI}