Wasanii Wengi wa Tanzania wana UKIMWI – Dude

Wasanii Wengi wa Tanzania wana UKIMWI – Dude

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
Staa wa Filamu za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ ameibuka na kusema kuwa kuelekea mwisho wa mwaka mastaa wengi wana Ukimwi na mbaya zaidi wanaambukizana wao kwa wao.

Akizungumza na gazeti la Ijumaa, Dude alisema kuwa mastaa wazima ni wa kuhesabika na kutaja sababu kubwa kuwa ni kubadilishana na kuibiana wapenzi bila kuwa na woga .

“Utakuta Mbongo Fleva ana mtu kwenye Bongo Muvi na Mbongo Muvi ana mtu kwenye dansi au kwa mamis au hata wacheza mpira, ukitaka kuujua ukweli tangaza dau kuwapima mastaa uone watakaojitokeza,” alisema Dude.
Kulwa Kikumba ‘Dude’.


Aidha, Dude alisema anavyoona yeye ingeanzishwa kampeni ya mastaa wa Bongo kupima Ukimwi kwani anawahofia watoto wa kizazi kipya zaidi ambao wanajikuta wanaingia pabaya na kuzima ndoto zao.
 
Hopelu amehapima nani kasema ukiwa na ukimwi ndoto zinafutika,ndoto zinafutika ukipata ajali na kufa au kuugua maralia na kufa pamoja na magonjwa mengine ila sio ukimwi
 
Ukimwi mbona sio issue siku hizi ni kama malaria tu but mmmh! Simulia sana omba yasikukute
 
Na hapo utasikia mara kaugua ghafla na kufariki dunia ndani ya muda mfupi, kumbe ARV work imefika mwisho na wanakufa wengi kwa style hiyo
 
Kila mtu ni muathirika mtarajiwa au maiti mtarajiwa...so ikifika siku yako lazima utang'oka kwa namna yoyote ile...si vyema kunyoosheana vidole kwani hakuna aliyewahi kuiona kesho....sijui kesho yangu itakuwaje na wala wewe hujui kesho yako itakuwaje.....ndio maana wahenga wakanena kuwa hujafa hujaumbika....watu wanapata haya maradhi kwa njia mbali mbali kwa si vyema kumkebehi mtu unless umepata chanjo....
Dude hakutumia hekima kuyaongea hayo ni kama ameropoka.....
 
Ujumbe umefika: wadau wabadili tabia. Condom kibao siku hizi... Waache ngono zembe!
 
Back
Top Bottom