Washairi na Waswahili nawaomba mje hapa

Washairi na Waswahili nawaomba mje hapa

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
NAWAOMBA WASHAIRI NA WASWAHILI WAJE HAPA. TUJADILI FANI NA MAUDHUI. SIASA WEKA KANDO.

CCM NI SHETANI, PEPO HUTOA SHETANI?

Fikiri upime sana, sinilaumu bilashi,
Fikiri pasi sonona, uwe bora mtumishi,
Fikiri na tulizana, katu usiende joshi,
Fikiri hafidhina, njia zako hazitoshi.

Fikiri upate jua, sikia we kuku maji,
Fikiri waja gundua, dunia yote si maji,
Fikiri waja tambua, taifa lakuhitaji,
Fikiri waja ng'amua, barafu pia ni maji.

Rauka raia mwema, uvivu si jambo jema,
Rauka hima hima, chombo chaenda mrama,
Rauka ewe mjima, konde limejaa kima,
Rauka acha koroma, kujenga nchi lazima.

Rauka jionee, nchi ilivyozizima,
Rauka utembee, uone tulipo kwama,
Rauka jijengee, ule mji wa waroma.
Rauka ujiombee, kwa mola wetu Karima.

Tazama kule angani, nambie waona nini?
Tazama tena angani, pana nyota si utani,
Tazama ACT angani, nyota ya matumaini,
Tazama nyota angani, pigo la nyoka nchini.

Tazama upate jua, CCM ni shetani,
Tazama utagundua, pepo hatoi shetani,
Tazama waja ng'amua, mapepo yapo kazini,
Tazama waja tambua, ACT ni tumaini.

Wino wa zafarani,Umeisha si utani,
Ya manjano zafarani, hamna tone chupani,
Kuandika natamani, wino sinao jamani,
Loo!!! niko tamatini,wana jamvi kwahereni

Mchungaji Njano5.
0784845394.
 
Hongera kwa tungo nzuri iliyosheheni vina na nahau jadidi
 
NAWAOMBA WASHAIRI NA WASWAHILI WAJE HAPA. TUJADILI FANI NA MAUDHUI. SIASA WEKA KANDO.

CCM NI SHETANI, PEPO HUTOA SHETANI?

Fikiri upime sana, sinilaumu bilashi,
Fikiri pasi sonona, uwe bora mtumishi,
Fikiri na tulizana, katu usiende joshi,
Fikiri hafidhina, njia zako hazitoshi.

Fikiri upate jua, sikia we kuku maji,
Fikiri waja gundua, dunia yote si maji,
Fikiri waja tambua, taifa lakuhitaji,
Fikiri waja ng'amua, barafu pia ni maji.

Rauka raia mwema, uvivu si jambo jema,
Rauka hima hima, chombo chaenda mrama,
Rauka ewe mjima, konde limejaa kima,
Rauka acha koroma, kujenga nchi lazima.

Rauka jionee, nchi ilivyozizima,
Rauka utembee, uone tulipo kwama,
Rauka jijengee, ule mji wa waroma.
Rauka ujiombee, kwa mola wetu Karima.

Tazama kule angani, nambie waona nini?
Tazama tena angani, pana nyota si utani,
Tazama ACT angani, nyota ya matumaini,
Tazama nyota angani, pigo la nyoka nchini.

Tazama upate jua, CCM ni shetani,
Tazama utagundua, pepo hatoi shetani,
Tazama waja ng'amua, mapepo yapo kazini,
Tazama waja tambua, ACT ni tumaini.

Wino wa zafarani,Umeisha si utani,
Ya manjano zafarani, hamna tone chupani,
Kuandika natamani, wino sinao jamani,
Loo!!! niko tamatini,wana jamvi kwahereni

Mchungaji Njano5.
0784845394.
Mkuu mashairi yako mazuri sana.

Unatukosea haki kukatisha supply
 
Back
Top Bottom