Washiriki wa shindano la urembo wazuiwa kuvaa mawigi, watakiwa kuonyesha nywele zao za asili

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kamati ya maandalizi ya shindano la urembo nchini Ivory Coast (Miss Côte d’Ivoire 2025 -COMICI) imetangaza kuwa katika hatua za awali za mchujo, washiriki hawataruhusiwa kutumia nywele za bandia.

Badala yake warembo wote wanapaswa kuonyesha nywele zao za asili, iwe ni ndefu, fupi, au zimekatwa kabisa.

Kwa mujibu wa Victor Yapobi ambaye ni Rais wa COMITE MISS COTE D'IVOIRE - COMICI ambao ni waratibu wa shindano hilo, uamuzi huo unalenga kuhamasisha urembo wa asili wa Kiafrika na kuthamini uhalisia wa wanawake wa Afrika.

"Nywele za washiriki lazima ziwe za asili wakati wa hatua za awali za mchujo. Hakuna nywele za bandia. Hii inamaanisha kuwa rangi za nywele za kuongeza, nywele za kushonea, na mawigi haviruhusiwi," amesema Yapobi
 
Ni vyema mawigi yapigwe marufuku barani Africa ili dada/mama/ nk waishi uafrica zaidi.
 
Naungana na kamati
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…