Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Wizara ya Afya ya Kenya imetangaza kuongezeka kwa kasi ya maambukizi ya ukimwi katika nchi hiyo. Wizara hiyo imeoa takwimu zifuatazo:
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu hizi za Wizara ya Afya kenya zinabainisha 98 wa miaka 10-19 huambukizwa ukimwi kila wiki nchini Kenya (Januari na Februari 2022). Kesi 45,724 za mimba za utotoni zilirekodiwa mnamo Januari na Februari ya mwaka 2022. Asilimia 21 ya mahudhurio yote ya kliniki za uzazi yalihusisha mabinti wenye umri kuanzia miaka 10-19 kwa mwaka (2021).
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu zinabainisha kuwa kesi 12,520 za unyanyasaji wa kijinsia na kingono ziliripotiwa nchini Kenya kwa mwaka (2021) ambapo katika kesi hizo, kesi 2,196 zilihusu wasichana wenye umri wa miaka 12-17 (Januari na Februari 2022). Wasichana 4,664 kati ya hao walipatiwa huduma za kuzuia VVU wakati 53 kati yao walikutwa na Virusi vya Ukimwi.
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu hizo zinaonesha kuwa Mikakati ya kupambana na Ukimwi nchini Kenya ilipunguza vifo vitokanavyo na Virusi vya Ukimwi kwa asilimia 67% kuanzia mwaka (2013 - 2021). Aidha, inaelezwa kuwa 83% ya watu wenye VVU nchini Kenya wanapokea na kutumia dawa za kurefusha maisha (ARV) mpaka mwaka (2021). Hii inamaanisha kuwa Watu wanaopokea dawa za kurefusha maisha walikuwa (600,000) mwaka 2013 na (1,200,000) mwaka 2021
Hivyo, kutokana na takwimu hizo ambazo zinaonesha ongezeko la maambukizi na unyanyasaji wa kingono nchini Kenya Serikali imeendelea kutoa wito kuundwa kwa sheria kali kudhibiti tatizo hilo sambamba na kuwataka wanajamii wa kenya wawe wamoja katika kuhakikisha wanapaza sauti na kudhibiti tatizo hili.
Nation Kenya
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu hizi za Wizara ya Afya kenya zinabainisha 98 wa miaka 10-19 huambukizwa ukimwi kila wiki nchini Kenya (Januari na Februari 2022). Kesi 45,724 za mimba za utotoni zilirekodiwa mnamo Januari na Februari ya mwaka 2022. Asilimia 21 ya mahudhurio yote ya kliniki za uzazi yalihusisha mabinti wenye umri kuanzia miaka 10-19 kwa mwaka (2021).
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu zinabainisha kuwa kesi 12,520 za unyanyasaji wa kijinsia na kingono ziliripotiwa nchini Kenya kwa mwaka (2021) ambapo katika kesi hizo, kesi 2,196 zilihusu wasichana wenye umri wa miaka 12-17 (Januari na Februari 2022). Wasichana 4,664 kati ya hao walipatiwa huduma za kuzuia VVU wakati 53 kati yao walikutwa na Virusi vya Ukimwi.
Chanzo cha Takwimu: Wizara ya Afya Kenya
Takwimu hizo zinaonesha kuwa Mikakati ya kupambana na Ukimwi nchini Kenya ilipunguza vifo vitokanavyo na Virusi vya Ukimwi kwa asilimia 67% kuanzia mwaka (2013 - 2021). Aidha, inaelezwa kuwa 83% ya watu wenye VVU nchini Kenya wanapokea na kutumia dawa za kurefusha maisha (ARV) mpaka mwaka (2021). Hii inamaanisha kuwa Watu wanaopokea dawa za kurefusha maisha walikuwa (600,000) mwaka 2013 na (1,200,000) mwaka 2021
Hivyo, kutokana na takwimu hizo ambazo zinaonesha ongezeko la maambukizi na unyanyasaji wa kingono nchini Kenya Serikali imeendelea kutoa wito kuundwa kwa sheria kali kudhibiti tatizo hilo sambamba na kuwataka wanajamii wa kenya wawe wamoja katika kuhakikisha wanapaza sauti na kudhibiti tatizo hili.
Nation Kenya