wasichana wengi wanaomaliza vyuo vikuu hawaolewi

Hapo kwenye nyekundu sijakuelewa vizuri kaka yangu. Ubora kwa maana ya kitu gani? kuwa wanawezakuwa wake wema au? kwa sababu kwangu mie sidhani kama kuwa mke mwema kunahusiana na elimu! labda unambie tabia ambayo nayo ni kigezo kinachotegemea na mtu na mtu! Labda kama utawezathibitisha kuwa tabia ya mtu inategemeana na kiwango cha elimu yake, kuwa akiwa na elimu zaidi anakuwa na tabia mbaya kulinganisha na mwenye elimu ya chini na tukifikia huko itabidi tuidefine tabia kwa mapana yake!
 


Umenena jambo zuri sana, tatizo wengi tuna mtazamo wa mapokeo ya tamaduni zetu, na mapokeo haya yanaathiri sana kisaikolojia wasichana wengine wenye mtazamo finyu kuona kuendelea kusoma wanapoteza nafasi ya kuolewa, na wengi wao wakishaolewa wanajikuta nafasi ya kujiendeleza kielimu imeshakuwa finyu.

Na si wasichana wote wanaoishi kama mbuzi aliyefungiwa zizini muda mrefu na akishafunguliwa ni balaa kila kionekanacho mbele yake hakimtoshi ila kile cha mbali ndo kizuri chenye kumpa shibe. Wasichana wengi wenye malezi mazuri ni bora pengine kuliko hawa wasichana wabichi tunaowachangamkia wanaume. Tukubali kwamba wachache mienendo yao imetupofusha wanaume kuona wasichana wengi wasomi wako hivyo.
 

Wanaume tumetofautiana kimtazamo kama ambavyo wanawake mpo. Mwanamke aliyeelimika anakuwa amejifunza mengi ikiwa ni pamoja na haki zake katika jamii. Wanaume tumekuwa na hoja za kujali mapokea zaidi badala ya haki za wanawake. matokea hii ikawa ni moja wapo ya hoja za wanaume kuwakwepa wasichana wasomi. Kuna wanaume wanaopenda mfumo dume badala ya mfumo wa umoja na kifamilia katika nyumba kushauriana namna ya kujenga familia kwa pamoja.
 

I support you, siamini wasichana/wanawake wanaosoma chuo wanamaliza na umri mkubwa. Tunawaona, tumesoma nao, ni ndugu zetu, wengi wao wana'range kati ya miaka 22-25 unless anaongelea wanaofanya Masters Degree au/na Doctorate, that age is just perfect for a girl to be married.

My observation, wanaume wanaoogopa kuoa wasomi ni wale wasiotaka kuoa msichana anaelingana nae kielimu au aliemzidi. Most men believe wanawake wa aina hii watataka kuwa juu yao kila siku kwa imani ya kwamba na wao 'wanajua' kutokana na usomi wao.
 
hasa wa udsm ndo hawaolewi. kinacho waponza ni dharau na kujifanya kujua. wanapenda starehe kuliko kazi(kuchuna mabuzi). wanaume wa siku hizi wamepewa maono na Mungu ya kugundua mapungufu ya msichana ndani ya wiki moja ndani ya mahusiano. ndo maana wanaishia kumegwa tu. hadi wajifunze kuishi kitanzania. ajue kupika, kufua,(asiwe mfuga kucha), ale matembele na Ugali (sio kila siku chips kuku), ajue kubana matumizi sio safari ndogo tu taxi, bajaj,(waache matanuzi yasio ya msingi). hata mimi ntaoa. Mia
 

utafiti what for?
 
Jamaa Kapiga panapotakiwa. Hii tafiti ina ukweli ndani yake. Wale wanaopinga ni watu wenye fikra finyu hawajui walisemalo. Big up mtu wangu, acha na watu hawa wenye fikra finyu.

Kusema kweli wasichana waliosoma wengi huwa wanakuwa kuwa na kiburi, wanaenda kinyume na maandiko ya MWENYEZI MUNGU ambaye alisema mwanamke amheshimu mmewe. Wengine wanageuka kuuza miili yao, na hii inawafanya wanawake wakose thamani. Hususani wanawake wa Kitamzania hawaheshimu ndoa zao. Hata akiolewa yuko tayari kutoka na mwanaume mwingine.

Nina rafiki yangu Manaijeria amekaa hapa kwa mda kidogo, alinieleza kuwa wanawake wa bongo hawafai kabisa, hii ni kwasababu siyo waaminifu ndio maana wanaume wanawapiga chini.

Kusema ukweli hawaolewi kwa sababu ya tabia mbaya. Wenye tabia nzuri wanaolewa. Wanafurahia tu sasa hivi lakini mwisho wake matati.

USHAURI: Nawashauri akinadada wamrudie MUUMBA wao na mambo yote yatakuwa sawa. Au wajitolee akinadada waweze kuwaombea hawa.

Mimi ni MAN.

 
kwa mtazamo wangu naona wanawake waliograduate wanakuwa na goals nyingi za maisha, kwahiyo once they graduate, marriage is not on top of their list of priorities, by the time they accomplish what they wanted wanajikuta wapo on their thirties and by this age, most women know what they want and they wont jump to marriage with just any man. by this age wanakuwa wanachagua sana na unakuta wanaume wengi of their choice na age zao wanakuwa wameshaoa au kama hawajaoa, they prefer younger women ndio hapo unakuta mdada anaamua kujizalia vitoto vyake (most of the time with a married man) na kustay single.
 
Yawezekana kweli ila sababu sio umri ni mtazamo wa mtu binafsi, mbona wengi wanamaliza vyuo na miaka 23-27. maisha ya chuo kama ya mtaani tu kutegana kupo tena mtaani ndo kumezidi,ila wanategwa wasijuo jitambua unajiingiza tu kwenye mahusiano bila kujua unataka nini, utategwa maisha yako yote maana hata maofisini waume/wake za watu wasiojitambua wanategwa
 

Aksante kwa kulifafanua vizuri hili la tabia. Hii post yako imenifanya niwaze kitu
Wasichana wasomi hawafai kuolewa kwa kuwa wana viburi, wanadharau
wasichana wazuri (kwa sura na maumbo) hawafai kuolewa kwa kuwa wana kiburi na dharau (kuna topics zilishakuja juu ya hili)

Je ina maana wasichana wazuri (whatever that means) ndio wanaosoma kufikia kiwango cha kuitwa wasomi au??
 
Inaonekana kuna sababu nyingi za kwa nini graduates wengi hawaolewi - Tabia, umri, haki za wanawake, mfumo dume nk. Ni wakati wa jamii na hasa sisi great thinkers kujadili umuhimu wa msichana kuolewa; yaani aolewe au azae tu ili mradi apate watoto? Je kusoma sana kunaathiri nini katika ndoa? Je kama wanaume wanaogopa wasichana wasomi inamaana msichana akitaka kuolewa asisome?. Suala hili ni pana zaidi. Kwa kuwa inaonekana kuna asilimia fulani ya ukweli (elimu ya msichana na kuolewa), then tumuombe aliyafanya utafiti huu afanya utafiti zaidi - tunaweza kupata matokeo ya kuisaidia jamii.
 

Sikiza nikuambie MUNGU aliweka utaratibu kaitka kila jambo. Kiburi cha hawa wasichana ni hiki.
1. Wanaona mtu mweye level (Education level) sawa na wao hawawezi.
2. Pepo limewaingia wanahitaji maombi. (Wanasema Marriage is not first thing) Unaona ujinga huo. Je najiuliza wanasoma kwa ajili ya nn? MAMBO YA KIZUNGU YAMEWATEKA

 
Mh utafiti huu unebagua kitu kinoja kikubwa nacho ni nafasi yetu wanaume kulipelekea hilo...............nadhani zaidi ya nusu yake wanaume tuhusika pia katika kusababisha hali hii...........mimi ni man
 

hawasomi hata biblia
 
asante kaka kwa maelezo mazuri yenye ukweli mtupu
 
Nashangaa katika mada nyingi hawa dada ni wachangiaji wazuri sana, lakini leo mada hii nzuri inayowahusu nilitegemea kusheheni hapa lakini ni mmoja mmoja tu anaingia kama mwizi na kutoroka, wengi wanaishia kuwa visitors tu. Wao wanajua sababu zaidi kuliko sisi wanaume kwa kuwa yaliwasibu, yanawasibu na yatawasibu, vema kama wangekuja hapa tujadili ili watutoe wasiwasi na khofu tuliyo nayo.

Kuna kila dalili ya ilmu yao waipatayo inachangia kuwafanya wasijione kama wanawake bali wamejiweka mahali fulani ambapo si pao kwa vile hawawezi kufikia pale kwa wanaume kwa vile siyo nature yao. Kwa maana hiyo kuendelea kuwa mahali amapo si pako utaonekana kama kichokoo tu.

Ilmu kwa mategemeo yangu yaweza msidia zaidi mwanake kujikomboa kwa maana ya kutambua haki zake katika jamii na kuzienzi badala ya kutoka kwenye hulka yake na kujiweka pasipohusika na hatima yake kuonekana si pake na kukwepwa na wanaume, matokeo yake anabaki kuwa chombo cha kuridhia wengi badala ya heshima ya mwenzi wa maisha yanye kumlindia heshima na utu wake.

Kwamba elimu waliyopata inawafungua akili na kuamua kubaki walivyo bila kuolewa kwa ridhaa yao ni hoja dhaifu, maana kuna kitu kinachofichwa hapo na kuegemea tu kutoa hitimisho ambalo ni matokeo ya udhaifu fulani wanaokuwa nao hawa akina dada wasomi. Wanaume wasomi wengi tu wanachamgamkia kuoa licha ya umri wao kuwa umepita, ingawa hii kwa wanaume haileti athari binafsi kukosa wa kumwoa hata kama mwanaume umri umeingia hatua ya umakamu.

Dalili za wazi ni msichana ajiweke na kuonekana ni msichana, mwenye hulka ya kiusichana, mwenye mtazamo wa kusikilizana asijiweke juu ya kichwa cha mtazamiwa wake, ambaye anaonekana kulinda haki na kupenda utamaduni wetu ambao mambo yake ni mazuri na mabaya kutoyaruhusu kwa malengo ya kujenga familia bora.

Mitindo ya wasichana wasomi kupendelea mambo ya viigizo vya kwenye net work ambavyo ni asili yake kubuniwa na wafanya biashara hizo ili kutunza misuli yao kuwawezeswha kufanya shughuli za biashara kwa muda mrefu kumewazodoa wengi na kujikuta pengine kuogopwa na wanaume wengi. Maana utembezaji wa bidhaa hizo za kimachinga mwanaume anaogopa kuchakaza kandambili nyingi kwa siku moja kutokana na mizunguko isiyoisha ya kuzungukia kupata vitumbua au mapambizo ya pilau anayotaka. Yaliyo mbele hayaoni kama yanafaa ingawa yanaweza kufanya pilau ipendeza na kutoa harufu nzuri tu kwa kutumia hizi nazi za kukunwa tulizozoea tangu utotoni na mababu zetu walitumia hawakupungukiwa na kitu.

Kwa vyo vyote kuna mengi, ila cha msingi tungemweka Mungu mbele ya macho yetu na kujikuta tunatembea mbele ya macho ya Mungu yanayotuangalia kila saa nadhani tungejenga na kuridhia yale ambayo Muumba anatuandalia, vinginevyo yapekee tuyatakayo katu hayataturidhia maana dhana ya binadamu ni hii ya kila zaidi apatavyo ndivyo atamanivyo, na hatima ni kuishia kuhangaika maisha yote bila kuamua moja na kuridhia hakuna kutulia, maana ya kuamua kubaki peke ndiyo nzuri na katika uzani madhara ni makubwa wakati fulani kuliko unafuu tunaofikiria.
 
Bonge la Futuhi, teh teh teh:lol::lol::lol::lol::lol:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…