Wasifu wa Julius Nyerere: Mikutano ya TANU Jangwani 1950s

Wasifu wa Julius Nyerere: Mikutano ya TANU Jangwani 1950s

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
WASIFU WA JULIUS NYERERE: MIKUTANO YA TANU JANGWANI 1950s

Bibi Titi Mohamed yuko pembeni kwa Julius Nyerere juu ya jukwaa dogo la miti.

Angalia hizo nyumba nyuma ya Nyerere hivyo ndivyo Kariakoo ya miaka hiyo ilivyokuwa.

Angalia umati wa watu waliokuja kuwasikiliza Nyerere na Bibi Titi.

Angalia baraghashia za wenyeji wa Mzizima zilivyoupamba mkutano wa TANU.

Waandishi wanasema mikutano ya TANU ya mwanzo ilikuwa inakosa watu.

Hili sikupatapo kulisikia.

Daisy Sykes katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake ameandika katika makala yake, "Abdulwahid Sykes I Knew," kuwa siku moja kabla ya mkutano Julius Nyerere, Dossa Aziz na viongozi wengine walikuwa wakikutana nyumbani kwao na baba yake Bwana Abdul alikuwa anapanga vipi akina mama watakuja uwanjani.

Mipango hii ilifanikiwa sana kuwahamasisha wake kwa waume kuhudhuria mikutano ya TANU.
 
WASIFU WA JULIUS NYERERE: MIKUTANO YA TANU JANGWANI 1950s

Bibi Titi Mohamed yuko pembeni kwa Julius Nyerere na upande wa pili ni Oscar Kambona juu ya jukwaa dogo la miti.

Angalia hizo nyumba nyuma ya Nyerere hivyo ndivyo Kariakoo ya miaka hiyo ilivyokuwa.

Angalia umati wa watu waliokuja kuwasikiliza Nyerere na Bibi Titi.

Angalia baraghashia za wenyeji wa Mzizima zilivyoupamba mkutano wa TANU.

Waandishi wanasema mikutano ya TANU ya mwanzo ilikuwa inakosa watu.

Hili sikupatapo kulisikia.

Daisy Sykes katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo cha baba yake ameandika katika makala yake, "Abdulwahid Sykes I Knew," kuwa siku moja kabla ya mkutano Julius Nyerere, Dossa Aziz na viongozi wengine walikuwa wakikutana nyumbani kwao na baba yake Bwana Abdul alikuwa anapanga vipi akina mama watakuja uwanjani.

Mipango hii ilifanikiwa sana kuwahamasisha wake kwa waume kuhudhuria mikutano ya TANU.
Angalia video:
 
Mzee Mohamed, Umewahi kufikiria kuandika historia ya maisha yako wewe binafsi? Naamini kuna mengi ya kujua kuhusu wewe.
 
Mzee Mohamed, Umewahi kufikiria kuandika historia ya maisha yako wewe binafsi? Naamini kuna mengi ya kujua kuhusu wewe.
Nsharighe,
Hili jambo linakuja kuja kwangu kila siku watu wakinambia ati niandike maisha yangu.

Lakini nashangaa kwani mimi sina umuhimu wa watu kutaka kusoma maisha yangu.

Sijafikiria jambo hili.
 
Nsharighe,
Hili jambo linakuja kuja kwangu kila siku watu wakinambia ati niandike maisha yangu.

Lakini nashangaa kwani mimi sina umuhimu wa watu kutaka kusoma maisha yangu.

Sijafikiria jambo hili.
inabidi uandike historia ya maisha yako, usipoiandika, hakuna atakaeweza kuiandika kwa usahihi, vitabu, mada zako zitaishi milele, kuna muda miongo mingi ijayo, vizaz vijavyo vitataka kukufahamu na kama hujaandika , havitapata nafasi hiyo,
 
inabidi uandike historia ya maisha yako, usipoiandika, hakuna atakaeweza kuiandika kwa usahihi, vitabu, mada zako zitaishi milele, kuna muda miongo mingi ijayo, vizaz vijavyo vitataka kukufahamu na kama hujaandika , havitapata nafasi hiyo,
Laki...
Muhimu ni yale niliyoandika katika makosa kusahihisha historia ya TANU na historia ya kudai uhuru.

Sidhani kama historia yangu binafsi ina umuhimu wowote.
 
Back
Top Bottom