Wasimamizi wa Kivuko cha KIGONGO FERY wanakera sana

ntamaholo

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
12,938
Reaction score
6,942
Leo nilikuwa natokea Sengerema, nikavukia Kigongo Fery. Nikiwa kwenye kivuko kuna suala la kipuuzi limetokea mahali pale kuna gari ambalo ni mali ya SABEDI lenye namba za usajili UAH 868 NA TELE lake UAD305Q.

Gari hili, linapakia mzigo kwa njia ya hatari kiasi kwamba halina uwezo wa kukaa vizuri kwenye FERRY. Nilichokishuhudia leo, ilibidi liingie kinyumenyume kwa kuwa mwishoni mwa gari hilo lingekuwa na uwezo wa kuingia kwenye feery.

Wakati likiingia kinyumenyume, mara kwa mara bodi ya gari ilikuwa inaparaza kwenye vyuma vya ferry na kusababisha uhabifu ambao kwa macho huwezi kuona.

Swali kwa TANROADS POLISI.
1. Kwa nini mnaruhusu magari ambayo yanapakia mzigo unaozidi limits na ferry kuingia kwa kuvunja sheria na pengine kusababisha uharibifu.
2. Polisi, kwa nini mnapopiga fine ya kubeba mzigo kwa njia ya hatari msimtake dereva kurekebisha upakiaji wake na kama mzigo unavuka gari kiasi kinachobaki kisishushwe?

Zifuatzo ni picha japokuwa sijazichukua vizuri










bila shaka unaweza kuona jinsi bodi la gari lilivyosugua chama cha ferry.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…