Wasimamizi wa Mabasi ya Mwendokasi Kimara hawajali abiria, wanawapuuza kama sio binadamu

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Kituo cha mwendokasi Kimara pia usimamizi ni mbovu sana, yaani unakuta magari yapo ya kutosha, abiria wanajaa kituoni kwa zaidi ya saa mbili.

Madereva wanapitapita tu kama hawaoni kinachoendelea,kuna muda magari yanaondoka yakiwa tupu kituoni, yanaacha abiria.

Vituo vya DART Mwendokasi havithamini abiria, wanafanya watakavyo.

 
Wangeanza na hii mpaka sijaona faida ya mwendokasi zaidi ya watanzania kupata shida tu!
 
Mwendokasi ibinafsishwe kwa wachina.
 
Hakika wanakera, nimeingia kituoni saa nane na 40dk mchana huu, nimekaa hadi saa 9 na 20dk nimeamua kutoka kwenda kupanda daladala, kwani muda hausubiri. Magari yalikuwa yanakuja ya Moroko yakija kima mara 2 yamejaa hadi pa kuingia hakuna. Inakera sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…