Wasomi waamua kumuanika Makamba

Joined
Jan 16, 2007
Posts
721
Reaction score
178
Wasomi waamua kumuanika Makamba
Thobias Mwanakatwe
Mtandao wa Wasomi na Wataalam Mkoa wa Mbeya, umemshambulia Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba na kumuonya kuacha kuingiza porojo na utani anapojibu hoja za msingi zinazowagusa Watanzania kwani anakiweka chama katika wakati mgumu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani.
Mtandao huo ulitoa kauli hiyo katika mkutano na waandishi wa habari jana, kuelezea kauli ya Makamba aliyoitoa Ijumaa iliyopita alipoitisha mkutano kujibu mapigo dhidi ya taarifa zilizoripotiwa katika kongamano la Mwalimu Nyerere lililofanyika wiki iliyopita.
Katika kongamano hilo, vyombo vya habari kadhaa viliripoti kwamba baadhi ya watu wanashauri kuwa Rais Jakaya Kikwete atoswe kwa vile anasita kufanya maamuzi magumu ndani ya chama hicho.
Mwenyekiti wa mtandao huo, Prince Mwaihojo, alisema tatizo la Makamba ni kupenda kuingiza porojo na utani wakati wa kujibu hoja za msingi ambazo zinaelekezwa kwa chama na serikali hali ambayo imesababisha wananchi na viongozi kutokuwa na imani naye.
Mwaihojo ambaye ni mwanachama wa CCM mwenye kadi namba 725928 aliyoikata mwaka 2000 katika tawi la CCM Ghana, jijini Mbeya, alisema Makamba ni mzigo kwa chama kutokana na kila mara kuingiza porojo na utani hata katika mambo ya msingi ambayo yanakuwa yanalalamikiwa na Watanzania.
“Makamba ajibu hoja: hakuna Mtanzania asiyefahamu kuwa Rais Kikwete amekuwa mgumu katika kuchukua maamuzi dhidi ya wanachama wanaotuhumiwa kwa ufisadi, na hayo ndiyo malalamiko ya msingi aliyopaswa kuyajibu na siyo kuingiza porojo zake ambazo tumezizoea,” alisema Mwaihojo.
Mwaihojo ambaye aligombea ubunge uchaguzi wa 2005 katika Jimbo la Mbeya Mjini kupitia CCM na kuangushwa kwenye kura za maoni, alisema Makamba ni miongoni mwa viongozi ambao hawatambui dhamana na thamani ya nafasi walizonazo katika chama na umma na ndiyo maana hawana mtazamo mpana wa kujua kwa sasa Watanzania wanataka nini.
“Makamba asiwe mropokaji awe anajenga hoja na kujua nini umma wa Watanzania unataka, anawaondoa watu kwenye hoja za msingi analeta vichekesho na porojo, hii ni dharau kwa wananchi na kuwafanya hawana akili,” alisema Mwaihojo.
Mwenyekiti huyo alisema udhaifu wa kiutendaji unaoonyeshwa na Makamba, ndiyo umeanza kusababisha umaarufu wa CCM kuanza kuporomoka taratibu kadri siku zinavyoendelea ikilinganishwa na miaka ya nyuma hali ambayo kama chama hakitachukua tahadhari Uchaguzi Mkuu wa 2010 utakuwa mgumu kwa chama hicho.
Alisema chama kinapaswa kujiuliza mara kadhaa “hivi kuendelea kuwa na kiongozi kama Makamba kitapiga hatua kimaendeleo au kitadidimia kwa sababu kuwa kiongozi ndani ya chama kikogwe kama CCM, lazima mtu awe makini anapojibu hoja na malalamiko yanayotolewa na Watanzania ambao ndio wanakiwezesha chama kiendelee kushika hatamu ya uongozi.
Akizungumza na waandishi wa habari Ijumaa iliyopita, Makamba alidai tuhuma dhidi ya Rais Kikwete zinatolewa na watu wenye visasi, walioshindwa uchaguzi na ambao wanafadhiliwa na matajiri wale wale wanaoitwa mafisadi wa CCM.
Makamba alidai tuhuma hizo zimejengwa katika misingi ya chuki kwani wengi wa makada wa chama hicho waliokuwa wakizungumza katika kongamano hilo, ama wao wenyewe au wagombea wao waliangushwa katika harakati zao za kisiasa huko nyuma.
 
Rooney ni maarufu kushinda Manchester United= Kikwete ni maarufu kushinda CCM
Huo ndio ulinganisho anaomanisha Mgosi wa ndima
 
Huyu mzee aliishia darasa la ngapi? anadiriki kuwatukana wazee ni WEHU kwa kusema ukweli? ...... @@@@ .....
 
wamwache kikongwe wa watu Makamba. He is only good for nothing. Mwenzenu anatetea kitumbua chake tu, akamate pension yake ili apumzike na mafisadi muda si mrefu.
 
Uzee unamsumbua huyo! Wamshauri akapumzike sasa
 
Tutakuwa tunarudia yale yale. Chama cha kishkaji kitazaa serikali ya kishkaji pia. Ukiangalia jinsi ilivyo rahisi kummwaga Makamba utashangaa kwanini bado yupo na anaboronga? Jibu mstari wa kwanza wa message hii.
 
Makamba kaja na hoja kitabu cha warumi kuwa mamlaka zote zimewekwa na Mungu hivyo ziheshimiwe. Asichoweza kupambanua makamba ni ikiwa hizo mamlaka zimewekwa na Mungu haina maana kwamba zimetakaswa. Hivyo kuna kazi binafsi ya hizo mamlaka kujitakasa zenyewe kwa kipimo cha haki ya Mungu la sivyo Mungu mwenyewe huzipindulia mbali na ni kwa kupitia WATU tena wale wale aliowatumia kuzisimika hizo mamlaka. Na Mungu amefanya hivyo mara nyingi na kujivunia hiyo kazi ya kuzing'oa kwamba ni UKOMBOZI!!
 
Uzee unamsumbua huyo! Wamshauri akapumzike sasa

Safi,

Mzee makamba majuzi kule Dodoma mwakumbuka wabunge wa CCM walirushiana maneno na baaadae yeye aka sema Umri wa mwanadamu kuishi ni miaka 70 na yeye na miaka nadhani 71 kwahiyo ana miaka 4 iliyobani ya kuishi tumwache, sas hizo ndizo dalili za mwisho wa uhai wake mawazo kufilisika na kutoa kauli za ajabu.

Siku ile hakujibu hoja na hakulinda hoja yake esp kuhusu matajiri kuwa na nguvu ndani ya CCM hatukutaka kusikia swala la matajiri wanachangia nini CCM au maskini wanachangia nini CCM, swala lilikuwa kwanini matajiri wananguvu,nafasi nyingi ndani ya CCM? kipindi cha Mwl.JKN matajiri walikuwepo ila hawakuwa na nguvu lakini walikichangia chama na hii ni kwa kuwa Mwl.JKN alikuwa na hoja ndani ya chama na chama kikawa na uadilifu na uongozi bora ingawa pia kulikuwepo na mapungufu kama tulivyo wote sie ni binadamu, ila hii CCM ya kipindihiki kwa kweli wamekosa Dila kabisa, Hawapendi kukosorewa sasa hawa ni viongozi gani wao ni Mungu au??

 
"Ukiita Masikini utapata Kuku"....Yusufu Makamba!
 
Angekuwa amesoma asingeishia uluteni (Lt.) Natumaini std viii ya enzi hizo.
 
"Ukiita Masikini utapata Kuku"....Yusufu Makamba!

Kwa maana nyingine CCM haihitaji kuku, hivyo badala ya kuwaita maskini ni bora iwaite matajiri waliotajirika kupitia ufisadi.
 
Angekuwa amesoma asingeishia uluteni (Lt.) Natumaini std viii ya enzi hizo.


Kwani uluteni unataka elimu gani?? Mkulu wa kaya mbona naye aliishia uluteni na Degree yake............??

Mbona akina msuguli, Mayunga na wengine wengi walikuwa mageneral bila hata hayo madarasa??

May be sema huku jeshini waligundua hana kipaji cha kuongoza kama mkulu wetu. Ila siasa za bongo ndiyo zinawafaa watu asio na sifa za kuongoza bali sifa za kupiga domo tu kama akina ...........!!! Wako wengi tu mpaka naona kuwataja wachache ni kuwaonenea tu!!!
 
hahahahaha,

ngoja niende jukwaa la jokes nkapumdhike
 
Mwakalinga anayo point kusema:

“Makamba asiwe mropokaji awe anajenga hoja na kujua nini umma wa Watanzania unataka, anawaondoa watu kwenye hoja za msingi analeta vichekesho na porojo, hii ni dharau kwa wananchi na kuwafanya hawana akili."

Mzee Makamba anasahau kwamba Chama anachoongoza ni Chama cha Wananchi wenye akili timamu waliopiga kura na kutoa uongozi kwa viongozi walio madarakani hivi sasa na hatimaye yeye naye kuambulia cheo alichonacho.

Yaliyozungumzwa kwenye Kongamano lile mengi ni yale ambayo yamekuwa yakizingumzwa na wananchi mitaani wakiwemo wanachama wenyewe wa CCM. Haiwezekani Wazee wazima na akili zao waende pale kuzungumza mambo yasiyo na maana kwa mustakabali wa Taifa. Naamini kabisa Mzee Makamba asingelikuwa kwenye nafasi aliyonayo, naye pia angelikerwa kama ambavyo Wazee wengine kama yeye wanavyokerwa na angelikuwa mstari wa mbele kuungana na Wazee wenzake kuelezea mapungufu yaliyopo yanavyohatarisha mustakabali wa Taifa letu.

Pia Mzee Makamba amejaribu kukwepa ukweli kudai kwamba yaliyosemwa kwenye kongamano lile yamesemwa kutokana na visasi vya uchaguzi uliopita miaka 4 iliyopita. Hivi Wazee wa nchi yetu waache kusema pale wanapoona mambo yanakwenda kombo kwa kuwa tu walitumia haki yao ya kidemokrasia kugombea uongozi na kukosa? Mimi nadhani wenye visasi hapa ni viongozi kama Mzee Makamba ambao hawataki kuwasikiliza wazee wenzao kwa sababu tu waligombea uongozi mwaka 2005.

Jambo la busara ambalo angeliweza kulifanya Mzee Makamba akiwa Katibu Mkuu wa Chama tawala ni kuchukua mawazo yaliyotolewa kwenye Kongamano lile na Wazee wa nchi hii na kuyapeleka kwenye vikao vya Chama ili yajadiliwe na yafanyiwe kazi kwa manufaa ya taifa zima. Kejeli hazisaidii kuondoa ukweli wa mambo.

Kwa kuwa Mzee Makamba anapenda sana 'vibwagizo' basi bora akumbushwe kwamba kuna kibwagizo kimoja kinasema "Mficha ficha maradhi kifo kitamuumbua". Tusitakie nchi yetu ifike huko kwa viburi visivyokuwa na sababu! Pia mchezo wa akina Makamba wa kutupa madongo/mawe kwenye bwawa lililojaa sie akina vyura ni mauti yetu sote ndio maana wapo vyura waliojitolea kupiga kelele.
 
Mtu kama katibu mkuu wa chama tawala kuwaita viongozi wenzake wehu ni aibu kwa taifa na aliyempa dhamana hiyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…