Wasomi Waliobobea katika Sayansi nchini Tanzania waingie Maabara Kutafiti Upatikanaji wa Chanjo ya magonjwa mbalimbali

Wasomi Waliobobea katika Sayansi nchini Tanzania waingie Maabara Kutafiti Upatikanaji wa Chanjo ya magonjwa mbalimbali

Intelligence Justice

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2020
Posts
3,443
Reaction score
4,006
Jukwaa la JF

Wito wangu ni kwa mamlaka ya nchi na Wataalamu wa Afya wafanye yafuatayo ili kuwa na uwezo wa kujikinga na kupambana na magonjwa mbalimbali:

1. Mamlaka ya nchi iwezeshe kifedha wataalamu wa afya na sayansi kwa ujumla kufanya utafiti wa uwezekano wa kutengeneza chanjo ya magonjwa mbalimbali yanayosumbua afya za wananchi;

2. Wasomi wa sayansi, wataalamu na madaktari wa afya wakutane haraka wakishirikisha na taasisi za utafiti kama NIMR, COSTECH , Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC), African Medical and Research Foundation (AMREF), Ifakara Health Research and development Centre (IHRDC), Mwanza Medical Research Centre (MMRC), Amani Medical Research Centre, Tukuyu Medical Research Centre nk wapange mikakati yenye tija kutafiti tiba na chanjo ya magonjwa mbalimbali.

Tanzania ina wasomi wengi sana na ambao wamebobea kwa yakini katika taaluma ya kuaminika . Madaktari waliosomea huko Cuba, Urusi, China, Ulaya, nk watumie taaluma yao kwa manufaa ya wananchi ambao ndio wateja wa uhakika kwa gharama nafuu. WAKUMBUKE AHADI HII: "Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumikia elimu yangu kwa faida ya wote"

3. Wananchi wajengewe hali ya kujiamini na kuondolewa HOFU maana ndicho kichocheo cha afya kunyong'onyea hatimaye magonjwa mengine nyemelezi kuchukua nafasi kushambulia.

Wenye fikra za kisiasa wakichangia mada hii wataharibu ni bora wakae pembeni wawaachie wataalamu na wenye mawazo chanya tu.

Karibu
 
Wanasayansi wa JF ambao ukiwapa teknolijia zilizo advance wanaona ni kama matunguli.

Kuna siku nilitoa teknolojia moja nikashangaa ugoro wa comment bila kuuliza kwa nini!?

Kama utafiti utakuwa JF basi ni nyungu na mashine ya juice ya miwa.
 
Chanjo kama hizi au kuna nyingine ?
0a0747e624def8d69f47497069312d82.jpeg
Screenshot_2021-02-01-19-47-58-834_com.android.chrome.jpg
 
Hawa wa kwetu nakumbuka hata maabara ya taifa waliicrash , ni baada ya kuipimisha mipapai na makondoo .

Kila jambo ni kusingizia mabeberu .
 
Bwana intelligence hao watu vyeti vyenyewe vya kununua!

No any research kaka politiki watamwachia nani
 
Mkuu tafiti zinahitaji uwekezaji mkubwa(PESA), pia tafiti hazihitaji siasa.

Haya mawili yakifanyika ugunduzi unawezekana.

Ila kwa taswira iliyopo hayo kufanyika ni ngumu,tumeruhusu siasa itawale kila kitu.
 
Ukweli lazima usemwe. Hakuna fedha za tafiti zinazotengwa tanzania kwenye afya
 
2. Wasomi wa sayansi, wataalamu na madaktari wa afya wakutane haraka wakishirikisha na taasisi za utafiti kama NIMR, COSTECH , Tanzania Food and Nutrition Centre (TFNC), African Medical and Research Foundation (AMREF), Ifakara Health Research and development Centre (IHRDC), Mwanza Medical Research Centre (MMRC), Amani Medical Research Centre...
What do you expect kama darasa la pili na la saba wanalipwa mshahara mkubwa kuliko Prof.

Msomi hataona sababu ya kuhangaika na tafiti kwakuwa mtu anagonga meza analipwa very high na anaheshimika kuliko msomi.
 
Mkuu wewe ulikuwa ?

Tayali wameshafanya utafiti na wamegundua dawa ya Kujifukiiza.
Mkuu, hawajagundua ila wameibia kile wataalamu wa miti shamba wanachoeleza wakati wanaomba usajili maana wanahojiwa vyote hivyo!!!

Walichokifanya sio kugundua dawa ila wamechanganya viini vya mimea lishe ili kuongeza kinga ya kupambana na athari za virusi. Virusi vikiwa ndani ya mwili wa binadamu ni ngumu kuviua na kusalimisha uhai wa kiumbe kinachoita mtu......haiwezekani, vinginevyo zamani sana wangekuwa wameshaipata.

Dawa ya kuua vijijidua vya virusi inahitaji kuwa na joto zaidi lile binadamu mwenye afya anatakiwa kuwa nalo, je itawezekanaje?

Ukimsikiliza vizuri aliyekuwa askofu mkuu wa EAGT Moses Kulola utapata jibu kwamba pamoja na kwamba sayansi ni sehemu ya tiba ya magonjwa ya milipuko kama Korona lakini bila kumtegemea Mungu aliye hai ni ubatili mtupu:

Please follow the link to corroborate on what is happening now:
 
Back
Top Bottom