Wassira: Watanzania wafikirie kuulinda muungano

Wassira: Watanzania wafikirie kuulinda muungano

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,277
Reaction score
8,860
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira amesema ni vyema Watanzania wakafikiria kudumisha Muungano kwa kutazama kero zilizoonekana miaka 50 iliyopita ikiwemo kero za watendaji, sheria na kuondoa kabisa kero zote ili kuweza kusonga mbele.

Aidha alisema serikali mbili bado zinafaa zaidi kwani kuwa na serikali tatu kutakuwa ni gharama zaidi kuendesha nchi. Kauli hiyo aliitoa juzi wakati wa mahojiano mjini hapa kuhusu masuala mbalimbali yanayokabili taifa kwa sasa, ikiwamo mwenendo wa Bunge Maalumu la Katiba.

"Kuna mambo makubwa zaidi ambayo bunge hili linatakiwa kuamua kuliko hili la serikali mbili, kufikiria kuwa na serikali tatu utalipa gharama kubwa zaidi," alisema.

‪source: clouds radio
 
Kwa muda uliokwisha dumu sidhani tena kama kuna haja ya kutaja mazuri na mabaya yake, kila kitu kipo hadharani waaamini kuwa sasa wananchi wamekomaa na wanajua walitakalo so haina haya ya kukumbushana juu ya hicho kitu kwa wakati huu!!!!!!

Yeye amekuwa sehemu ya serikali kwa muda mrefu so matendo yake ni sehemu ya au mazuri au mabaya ya muungano husika maneno tu hayatoshi wasubiri wapimwe kwa matendo yao kwa muda wote wa muungano!!!!
 
Ningefurahi sana kuona kiongozi aliye na ujasiri wa kuwaambia ndugu zetu wazanzibari kuwa wafikirie kuhusu kudumisha muungano, maana pande ambao hawautaki kabisa muungano ni Zanzibar. Halafu hili la kusema serikali tatu ni gharama, hiki siyo kisingizio kizuri wakati Zanzibar imebadolisha katiba na kujitambulisha kama nchi, wakati Tanganyika haijulikani ilipopotelea. Kama mambo ya muungano yatahusu baadhi ya wizara, je yaliyopo upande wa Tanganyika pekeyake yatasimamiwa vipi? Je wazanzibari wapo tayari kubadili katiba yao iliyojipa mamlaka (bendera na wimbo wa taifa). Na vilevile Kama ni kweli kigezo ni gharama, basi iundwe serikali moja.
 
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira amesema ni vyema Watanzania wakafikiria kudumisha Muungano kwa kutazama kero zilizoonekana miaka 50 iliyopita ikiwemo kero za watendaji, sheria na kuondoa kabisa kero zote ili kuweza kusonga mbele.

Aidha alisema serikali mbili bado zinafaa zaidi kwani kuwa na serikali tatu kutakuwa ni gharama zaidi kuendesha nchi. Kauli hiyo aliitoa juzi wakati wa mahojiano mjini hapa kuhusu masuala mbalimbali yanayokabili taifa kwa sasa, ikiwamo mwenendo wa Bunge Maalumu la Katiba.

“Kuna mambo makubwa zaidi ambayo bunge hili linatakiwa kuamua kuliko hili la serikali mbili, kufikiria kuwa na serikali tatu utalipa gharama kubwa zaidi,” alisema.‪source clouds radio

Hivi wassira unajua chanzo cha kuundwa wizara ya muungano?lakini imeshindikana kutatua kero sasa sidhani hata mkipewa miaka 100 chini ya serikali 2 zitatatulika
 
Mnaweza mkataja sababu nyingi sana za kuunda serikali tatu, lakini sababu moja tuu kubwa ya kuulinda muungano ni serikali mbili na sababu moja tuu ya kuuvunja muungano ni serikali tatu.
 
asiramkono.jpg
 
Waulize kwanza Crimea inavyotaka kugawana mbao na Uraine! Muungano siyo vitabu vitakatifu ambavyo hauwezi kubadili hata nukta!
 
Back
Top Bottom