Wastaafu tumewakosea nini Serikali?

Wastaafu tumewakosea nini Serikali?

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Leo ilikuwa ni siku ya Wafanyakazi dunia nzima. Hapa Tanzania sherehe hii iliadhimishwa Mjini Morogoro na mgeni rasmi alikuwa Mhe. Samia Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Sherehe kama ya leo ndiyo wafanyakazi wanawasilisha kero zao mbele ya Mgeni Rasmi ili zifanyiwe kazi. Sisi Wastaafu tuna kero nyingi sana lakini hatuna nafasi ya kukutana na Mhe. Rais ili tuziwasilishe kwake. Mojawapo ya kero zetu ni Pensheni ndogo tunayopata.

Kutokana na kupanda kwa maisha Wastaafu wanatakiwa kufikiriwa ili pensheni zao ziweze kurekebishwa. Aliyekuwa Rais wa Awamu ya nne aliweza kuturekebishia kidogo pensheni zetu lakini mpaka leo hakuna kilichofanyika.

Mhe Rais sisi Wastaafu tunaishi maisha magumu sana tunakuomba sana utufikirie kwa kuongeza kiwango cha pensheni zetu. Tumetumikia nchi hii. Tumeikosea nini Serikali?
 
Kuna haja ya Kumwona Mh.RAIS Kwani anapowashughulikia WATUMISHI ajue WASTAFU walikuwa Watumishi
 
Kijana wenu ambaye ni Rais wa Zanzibar amewachekesha wazee kweli kweli yaani, amewapandishia pensheni na ile allowance ya mwezi kwa 100% na kawaahidi kuongeza hadi kufikia 150%.

Japo chama ndiyo hiko hiko ila nyie wa bara huko shauli zenu na ccm yenu!.

Fanyeni tu mpango mpate kamba mle kwa urefu utakaowatosha huko kwenye makamati na uteuzi wa wenyeviti wa bodi wa mashirika.
 
Leo ilikuwa ni siku ya Wafanyakazi dunia nzima. Hapa Tanzania sherehe hii iliadhimishwa Mjini Morogoro na mgeni rasmi alikuwa Mhe. Samia Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Yaani hakuna anaewajali Wala kuwakumbuka..

Nyie zamu yenu mlishamaliza
 
Sgr zikiisha mtapandishiwa 🤪🤪

Msijali zamu yenu ni mwaka ujao kuelekea uchaguzi
 
Kijana wenu ambaye ni Rais wa Zanzibar amewachekesha wazee kweli kweli yaani, amewapandishia pensheni na ile allowance ya mwezi kwa 100% na kawaahidi kuongeza hadi kufikia 150%.

Japo chama ndiyo hiko hiko ila nyie wa bara huko shauli zenu na ccm yenu!.

Fanyeni tu mpango mpate kamba mle kwa urefu utakaowatosha huko kwenye makamati na uteuzi wa wenyeviti wa bodi wa mashirika.
Unaiponda CCM kwani Rais wa Zanzibar ni wa chama gani. CCM chama dume.
 
Vyama vya Kupigania haki naa maslai yq wafanyakazi wachukue gili ice sehemu ya kupigania haki zao. Itasaidia sana
 
Wasoma risala jana walizingua ajabu na kweli hawakuzingatia wala kugusia tatizo la kikokotoo ambalo limeathiri pakubwa mafao ya wastaafu wetu.Sijui waliogopa nini?

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom