Waswahili Walisema Ndoa........!???Cheki Hii!

kaka yako dhaifu

mkuu naomba niendelezee hapo ili ujumbe umfikie vizuri aliyeleta mada hii...familia dhaifu huzaa watoto wa kiume dhaifu ambao nao huoa wake dhaifu nao wake zao huzaa watoto dhaifu na mwishoni ni familia legelege.... Mwambie kaka yako ajifunze kwa baba yako..

Kwani babako nyumbani aliishi na ukoo wa mamako??

Na short cut ya wanawake wanaolea ukoo wao kwa waume zao ni kwenda kumuolea mke mwengine mtaa wa pili...

So braza wako kulala gheto kwa mshkaji ni upuuzi...mwambie apange chumba mtaa wa pili kisha amwoe rafiki wa mke wake ili awe na wake wawili nadhani bi mkubwa wifi yako wa sasa atatia disipilini...

adui wa mwanamke mwanamke mwenzie.
 
Hiyo nyumba ya nani? kaka au shemeji maana kama shemeji amejenga au kupanga, mpe pole kaka yako.
 
alaa kumbee sa ilikuwaje ukamshtua tb namna ile we mwanamume khaaaa leo hata lunch sijui kama ana hamu nayo
 
Lah! Huo msalaba aliotwishwa ni kabambe kweli. Ningelikuwa mimi ningepiga BAN wote siku ya pili yake tu.
 

Mchuma janga hula na ndugu zake. Huyu mwanaume anapalilia umasikini, mwisho wake watoto wakifikia umri wa kudai ada ataanza kuwapiga mizinga ndugu zake, achilia mbali kwamba hana uwezo wa kusaidia ndugu yake hata mmoja. Baba yangu enzi zake (R.I.P) anakuja mchana kweupeee, atawatukana wewe na mkeo kwa muda wa masaa kama 2 halafu wote mtajua kwamba hamna akili kuanzia siku hiyo! hii style ndio inayofaa kujiepusha na matatizo mnayowekeza sasa!
 
Duuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!!!!!!!!! npo tongue tied, kweli ndoa ndoano
 

Uvivu ndio sababu. Tena wakiondoka wanataka nauli. ukiwaendekeza, utaumia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…