Wataalam msaada kwenye hili kama lina ukweli ndani yake

Joined
Jun 20, 2015
Posts
15
Reaction score
6
"Men have nipples because everyone is a female until the Y chromosome kicks in. You were all girl embryos."
 
Kwanza tuanzie kwenye chromosomes za jinsia; mke anakuwa na XX, mme ana XY. Yai la mama kabla ya kurutubishwa linakuwa na chromosome X, na mbegu ya baba inakuwa sex chromosome X au Y. Yai la mama likirutubishwa na mbegu ya baba yenye sex chromosome Y basi kiumbe kinachoumbika kitakuwa na maumbile ya kiume kwa sababu hizi: Y chromosome ina sehemu maalum ya kuamrisha utengenezaji wa pumbu (testicle) na baada ya hapo pumbu hizo zitatoa aina ya hormone iitwayo Anti-Mullerian factor ambayo itazuia kuumbika maumbile ya kike.
Uwepo wa chuchu upo kwenye ngozi ambayo huumbwa mapema kabla ya kuumbika kwa pumbu na AMF.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…