Wataalam naombeni ushauri wenu

yenyewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
621
Reaction score
94
Mi nimehitim chuo miaka miwili iliyopita nikiwa na degree moja katika social science. Baada ya kutafta ajira mda mref bila mafanikio nimepata wazo la kusoma masters.
Lengo langu ni kubadilisha fani na kusoma masters ya education ili angalau niweze kurahisisha mchakato huu wa kutafta ajira.
Naombeni ushauri wenu kuhusu hili ndg zangu.
 

kijana nakushauri usisome master utabugi tena mkuu,wizara ya elimu haiajiri mtu mweny masters,ushauri wangu kwako soma post graduate diploma=degree,mwaka mmoja watakupangia kituo moja kwa moja,inatolewa duce,udsm ,udom na chuo kiuu huria,ila udom ni bei rais sana mil.1 na lak 8, udsm mil3.lak 2.kuna jamaa zang wapo wanapiga.na sio mwaka mmoja exactly ni kama miez 8 au 9.thanx
 

Nimekuelewa sana mkuu. Ahsante sana
 
Pole sana,kwann mwanzoni hukusoma degree ya education?

Sikuipa kipaumbele na kwa sasa nataka niisome sio kwamba naipenda ila natafta wepesi wa kupata ajira nikaondoka hapa mtaani.
 
Nimeipenda hii kaka...ni kama vile katika football unakwenda mpaka golini kwa mpinzani wako halafu unarudisha pasi golini kwenu...iko safi kaka
 
kasome post graduate, vinginevyo hiyo master utakuja kuijutia. hiyo social science ulikuwa na GPA ya ngapi? maana pungufu ya 3.5 NI MSALA.
 
kasome post graduate, vinginevyo hiyo master utakuja kuijutia. hiyo social science ulikuwa na GPA ya ngapi? maana pungufu ya 3.5 NI MSALA.

Nilikuwa na 3.6 mkuu
 
Kama unaenda kusoma kwa ajili ya ajira bora usisome post-graduate maana ualim haupendi ni rahisi sana na ualim ktokukpenda.Nakushauri ukasome masters ya unacho kipenda MUNGU atasaidia utapata ajira unayo penda kuliko kwenda kuhalib ualim ambao wengine ndo tunasomea kwa mapenzi yet,ucje leta 0 nyingi.
 

Sasa nifanyenye wakat sisi hatuajiriwi na walim wanaajiriwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…