Wataalam wa Hisabati, swali hili

Sijakuelewa, 1 umeitoa wapi?

Nikutolee mfano:

Chungwa ukilitakata sehemu nne sawa, utapata kila kipande ni robo (1/4), na ukijumlisha robo nne jibu lake ni moja. Na hata usipogawa sawasawa, ukijumlisha sehemu zote ulizokata jibu lake lazima liwe moja.

Moja inatoka wapi?
Swali linazungumzia vipande (fractions), kwahiyo ukimjulisha vipande vyote, jibu linatakiwa kuwa 1, lakini kwenye swali, kuna mmoja kapewa machungwa 15. Kwa hiyo ni sahihi kusema, machungwa 15 ni matokeo ya kutoa sehemu nzima ya machungwa (1) kutoa sehemu ya machungwa yaliyogawiwa kwa wengine.
 

Kumbuka tulishatafuta idadi ya machungwa ya Juma tangu mwanzo (3/4 ya machungwa yaliyobakia ambapo tukichukua 1 tukatoa 1/3 aliyopata Haruna) na kujua kuwa alipata nusu ya machungwa. So it is just a matter ya kumultiply.
 
Kumbuka tulishatafuta idadi ya machungwa ya Juma tangu mwanzo (3/4 ya machungwa yaliyobakia ambapo tukichukua 1 tukatoa 1/3 aliyopata Haruna) na kujua kuwa alipata nusu ya machungwa. So it is just a matter ya kumultiply..


Tufanye hivi:

Ukichukua sehemu (fractions) za machungwa waliopata Juma, Haruna na Petro jibu lazima liwe moja. Kama sehemu hizo utazipa majina a kwa Haruna, b kwa Juma na c kwa Petro basi, hiki ndiyo ukweli:
a + b + c = 1

Lakini Petro, yeye hatujui sehemu bali tumepewa idadi, basi expression yetu itabadilika na kuwa:
c = 1 - (a + b)
c = 1 - a - b
ambayo ni sawa na kuandika: 1- a -b = 15..................... (i)

Kama machungwa yote yalikuwa x , basi idadi ya machungwa ya:

a= 1/3x

b = 2/3*3/4x
= 1/2x

c = 15

ukiinginza idadi hapo juu kwenye (i), unapata:

1 - 1/3x - 1/2x = 15

Nimejaribu kurahisisha sana.......
 

Sasa 1-1/3-1/2 si ndo 1/6

Au hujauona huo mstari ulioanza na Neno Petro?

Sijui hata unasahihisha nini kwa kurudia kile kile kilichoandikwa
 
Swali halina vipande vya machungwa Ila ni sehemu ya ya idadi ya machungwa(mazima)
 
Mkuu ukisema a+b+c=1 hautakua sahihi Haruna, Juma na Petro hawakugawana chungwa moja bali idadi fulani ya machungwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…