Wataalam wa hisia DSE

Wataalam wa hisia DSE

amshapopo

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2014
Posts
1,834
Reaction score
4,161
Wasalam,

Naomba kujua ni hisa gani zinafanya vizuri Dse kwa sasa? Nataka nijitoe muhanga kununua hisa.
 
Mimi nadhani kabla hujanunua hisa ningekushauri kwanza ujielimishe kuhusu dhana nzima ya hisa na vitu gani vinavyofanya hisa zipande au kushuka. Nasema hivi kwa sababu hata hizo hisa utakazoambiwa uzinunue leo kwa kuwa zinafanya vizuri, hakuna guarantee kwamba kesho na kesho kutwa zitaendelea kufanya vizuri vile vile. Hili likitokea si ajabu utarudi na kuwalaumu waliokushauri uzinunue kwamba wamekudanganya. Kumbe hata wao wasingejua.

Kabla hujawekeza mahali - hasa kwenye mambo kama haya ya hisa, bonds..., hakikisha kwamba una maarifa na habari sahihi kwanza...
 
Kama unanunua hisa DSE kwa lengo la kupata gawio la mwaka hakuna maneno ila kama unawekeza kwa lengo la kufanya speculation sikushauri uingie.
 
Back
Top Bottom