Nipo kwenye makundi mengi ya WhatsApp ya CCM mikoa mitano. Ni dhahiri kwa hoja za Lissu ni hakika kuna miguno ya kuvumilia maumivu. Tofauti na matarajio ya wanaCCM wengi waliodhani hoja za miundombinu zingembeba Magufuli, la hasha, hoja za Lissu ndiyo mahitaji ya wananchi wengi.
Kutokana na ilani ya CCM kusheheni ndege, meli na reli, na kukosa ahadi zinazowagusa watanzania wengi, kumetokea sintofahamu ndani ya chama hiki ya kudandia hoja za Lissu ambazo hazipo kwenye ilani ya CCM.
Kwa mfano, hoja ya kuboresha maslahi ya watumishi haipo sehemu yeyote katika ilani ya chama chetu cha kijani. Lakini baada ya Lissu kuiongea Mara kwa mara kwa kuwa ipo kwenye ilani ya Chadema, Naye Magufuli ameidandia bila utaratibu na sasa inamtesa sio yeye tu bali na watetezi wake.
Hoja nyingine ambazo chama chetu kimedandia ni hoja ya Bima ya Afya kwa wote, kulipwa madeni yote kwa watumishi, mikopo kwa wanafunzi, TRA na wafanyabiashara, nk.
Hivi karibuni Bashiru aliwaamuru vijana wa CCM wajibu hoja za wapinzani haraka. Hahaha!!. Nipo kwenye makundi manne ya wasomi wa vyuo vikuu, yaani shirikisho la vyuo vikuu, kuna mjadala mzito kuwa hoja za Lissu hazijibiki kwa kuwa anayoahidi ndiyo hasa mahitaji ya jamii. Kundi moja likaenda mbele zaidi na kujadili kuwa kukosekana kwa mikopo kwa wanachuo wa vyuo vikuu ni kero ambayo inakiangusha CCM kwa vijana wa vyuo vikuu.
Ndugu zangu mwanaccm wanaojielewa, naomba nishauri ila najua ushauri wangu hautakubalika kwa kuwa mwenye akili ndani ya chama chetu ni Magufuli peke yake. Nashauri tuipitie ilani yetu iliyosheheni miundimbinu, tuweke mambo yanayowagusa wananchi wa kada nyingi hususani vijana.
Naomba kuwasilisha
Ajira elfu 13 za walimu hoyeee
Kutokana na ilani ya CCM kusheheni ndege, meli na reli, na kukosa ahadi zinazowagusa watanzania wengi, kumetokea sintofahamu ndani ya chama hiki ya kudandia hoja za Lissu ambazo hazipo kwenye ilani ya CCM.
Kwa mfano, hoja ya kuboresha maslahi ya watumishi haipo sehemu yeyote katika ilani ya chama chetu cha kijani. Lakini baada ya Lissu kuiongea Mara kwa mara kwa kuwa ipo kwenye ilani ya Chadema, Naye Magufuli ameidandia bila utaratibu na sasa inamtesa sio yeye tu bali na watetezi wake.
Hoja nyingine ambazo chama chetu kimedandia ni hoja ya Bima ya Afya kwa wote, kulipwa madeni yote kwa watumishi, mikopo kwa wanafunzi, TRA na wafanyabiashara, nk.
Hivi karibuni Bashiru aliwaamuru vijana wa CCM wajibu hoja za wapinzani haraka. Hahaha!!. Nipo kwenye makundi manne ya wasomi wa vyuo vikuu, yaani shirikisho la vyuo vikuu, kuna mjadala mzito kuwa hoja za Lissu hazijibiki kwa kuwa anayoahidi ndiyo hasa mahitaji ya jamii. Kundi moja likaenda mbele zaidi na kujadili kuwa kukosekana kwa mikopo kwa wanachuo wa vyuo vikuu ni kero ambayo inakiangusha CCM kwa vijana wa vyuo vikuu.
Ndugu zangu mwanaccm wanaojielewa, naomba nishauri ila najua ushauri wangu hautakubalika kwa kuwa mwenye akili ndani ya chama chetu ni Magufuli peke yake. Nashauri tuipitie ilani yetu iliyosheheni miundimbinu, tuweke mambo yanayowagusa wananchi wa kada nyingi hususani vijana.
Naomba kuwasilisha
Ajira elfu 13 za walimu hoyeee