Watanzania hasa Vijana tujifunze uvumilivu huu wa Kimafanikio kutoka kwa Mtangazaji Hassan Ngoma

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Muda mfupi tu uliopita wakati Muwasilishaji katika Kongamano la ' Fursa 2017 ' linaloendelea sasa Mkoani Morogoro Msanii na Msomi ' aliyetukuka ' Nikki wa Pili amesema kwamba amevutiwa mno na uvumilivu na kujituma kwa Rafiki yake mkubwa Mtangazaji wa 360 Clouds tv Hassan Ngoma.

Nikki wa Pili aliendelea na kusema kwamba Mtangazaji huyo ( Hassan Ngoma ) wakati alipokuwa Ulaya alikubali kujitoa kabisa katika kutafuta ' Fursa ' mbalimbali hadi akapangiwa Kazi za Kuzoa ' takataka ' huku nyingi zikiwa ni za Kuchambua ' Kinyesi ' cha binadamu ( kwa lugha nyepesi mavi au makimba )

Nikki wa Pili amesema kwamba kama isingekuwa uvumilivu wa Mtangazaji wa Clouds tv 360 wa kuchambua makimba / mavi ya Wazungu huko Ulaya leo hii asingekuwa ' Tajiri ' au mwenye ' mafanikio ' hivi aliyonayo sasa.

Binafsi ushuhuda huu nimeupenda na nimeugusa mno na sasa nami nataka kujiandaa kwenda Ubalozini kuomba ' Viza ' ya kwenda Ulaya / Ng'ambo ili nami pia nikatumie ' Fursa ' ya kusomba / kuzoa Kinyesi kwa malipo makubwa kama ambavyo alikuwa akifanya Mtangulizi wetu Mtangazaji wa Clouds tv Hassan Ngoma.

Kwa wale ambao labda mtakuwa na mashaka na hii taarifa nawaomba angalieni Clouds tv katika YouTube pale ambapo Nikki wa Pili alipokuwa akizungumza na akaligusia hili suala la Hassan Ngoma kuzoa ' takataka ' Vinyesi huko Ulaya ambazo kiukweli zimembadilishia sana maisha yake hadi kuwa ' Milionea ' kama alivyo sasa.

Haya Watanzania wenzangu tutumie ' Fursa ' Vinyesi vya Ulaya vinatusubiri kwa malipo yake ni makubwa sana. Haraka mno hebu tufuate ' nyayo ' za Mtanzania mwenzetu Mtangazaji Hassan Ngoma wa Clouds tv 360 katika utumiaji wa ' Fursa ' hasa katika nchi za wenzetu.

Akhsanteni sana Clouds Media Group kupitia Clouds tv kwani na Mimi GENTAMYCINE nimegundua ' Manta ' haipo tu Tanzania bali kumbe hata huko Ulaya kuna ' Manta ' takataka ' Kinyesi ' cha Wazungu na najiandaa sasa kutafuta Viza niiwahi ili nami ' nitusue ' kimaisha kama Mtangazaji Hassan Ngoma.

Nawasilisha.
 
Hiyo kazi ya kuzoa kinyesi kwakweli siifahamu lakini kama ipo lazima kutakuwa na vitendea kazi kama Muuza Sumu anavyoita vifaa maalumu vijulikanavyo kama vya kuzolea kinyesi. Au labda alikua anachambisha vizee.
 
Hiyo kazi ya kuzoa kinyesi kwakweli siifahamu lakini kama ipo lazima kutakuwa na vitendea kazi kama Muuza Sumu anavyoita vifaa maalumu vijulikanavyo kama vya kuzolea kinyesi. Au labda alikua anachambisha vizee.
Mstari wako wa mwisho ulipaswa kuwa wa kwanza Dada Tecla!
 
Hiyo kazi ya kuzoa kinyesi kwakweli siifahamu lakini kama ipo lazima kutakuwa na vitendea kazi kama Muuza Sumu anavyoita vifaa maalumu vijulikanavyo kama vya kuzolea kinyesi. Au labda alikua anachambisha vizee.

Mkuu unaogopa Kuchambua ' Nnya ' Ulaya / Ng'ambo kama Mtangazaji wa 360 Clouds tv Hassan Ngoma? au na Wewe siyo Manta?
 
mkuu na wewe unamkubali uyo jamaa maana kuna uzi kadhaa nilikuona unampinga sana..imekuwaje tena???au "nnya" za kizungu zimesababisha umkubali ghafla
 
mkuu na wewe unamkubali uyo jamaa maana kuna uzi kadhaa nilikuona unampinga sana..imekuwaje tena???au "nnya" za kizungu zimesababisha umkubali ghafla

Usipomuelewa vizuri GENTAMYCINE kila siku utakuwa unapata nae taabu humu Jamvini.
 
Basi tuseme mzee wa mafumbooo

shushushu VIP

Naomba nikae mbali na Wewe kwani utaniharibia kila kitu. Nafikiria ' kukuignoa ' kabisa ili usinione na nisikuone tena humu JF na milele amina.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…