Watanzania hatuwezi kushindana duniani kwa biashara zetu hizi tunazo zifanya

Watanzania hatuwezi kushindana duniani kwa biashara zetu hizi tunazo zifanya

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
Tanzania ni vigumu kushindana duniani kwa biashara hizi rahisirahisi zinazo endeshwa na Watanzania.
Watanzania wengi hawapendi biashara za kuumiza kichwa wanataka biashara rahisirahisi na ambazo hata siku moja haziwezi kutufukisha popote.
Nitatoa mfano
1. Biashara ya Baa au grosary
2. Saluni
3. Daladala
4.Satationary
4. Duka la kuuza vitu rejareja na jumla
5. Biashara ya kuuza nafaka
6. Biashara ya kuuza magari
7. Biashara ya kuuza simu
8. Biashara ya kuuza nguo na viatu na vyombo mbalimbali
9. Hardware
- Kuuza chips
- Kuuza vipodozi
- Duka la dawa za binadamu
10. Nyumba za kupangisha na kazalika
HIZI NDO BIASHARA ZINAZO PENDWA NA WATANZANIA, NI NZURI SANA. BUT KWA HIZI BIASHARA HUWEZI SHINDANA KIMATAIFA HATA SIKU MOJA.

-HAMNA MWEKEZAJI KUTOKA NJE AMBAE ANAWEZA KUBALI KUJA MUINGIE UBIA WA KUFANYA BIASHARA NILIZO OROZESHA HAPO JUU.

-HIZO HAPO JUU NDO BIASHARA ZA WABONGO HAZIHITAJI AKILI, BIASHARA AMBAZO UNAANZISHA ASUBUHI JIONI UNAFAIDA TIYALI.
- ILA KIMATAIFA HATA TAASISI KAMA BENK YA DUNIA KWENYE KITENGO CHA MIKOPO HAWAWEZI HATA SIKU OJA KUKUPATIA MKOPO KWA BIASHARA HIZO HAPO JUU LABDA KIDOGO NYUMBA ZA KUPANGA MEANS REAL ESTATE.
-BIASHARA ZA KUHITAJI AKILI NYINGI
- BIASHARA ZA CONSULTANCY
- UWEKEZAJI KATIKA KILIMO
- UFUGAJI WA AINA ZOTE
- MAHOTELI NA MIGAHAWA
- UTARII
- UJENZI
- NISHATI YA JUA, UPEPO NA KAZALIKA
- VIWANDA VIDOGOVIDOGO NA VYA KATI
- MADINI
- TEKINOLOJIA YA MAWASILIANO, -
SIMAANISHI KUUZA SIMU
HIZI BIASHARA ZINAHITAJI AKILI SANA NA NI BIASHARA AMBAZO ZINAWEZA KAMA ZIKIKUA KUSHINDANA KIMATAIFA, HIZI KUPATA WAWEKEZAJI WA KUINGIA NAO UBIA NI RAHISI SANA
 
kuna makampuni mengi ya watanzania nimeyaona zambia,botswana,namibia,na south africa,lakini wengi wanakuwa wachaga
sielewi kwa nini bawana
 
kuna makampuni mengi ya watanzania nimeyaona zambia,botswana,namibia,na south africa,lakini wengi wanakuwa wachaga
sielewi kwa nini bawana

Katika Ujasiriamali kuna aina 2. Born na Made. Wachaga ni kama walivyo wahindi yaani Entrepreneurs by Born, Wao wana spirit ya Ujasiriamali kama walivyo wahindi, na wamekuwa wanarithi kutoka kwa ndugu zao.
Ingawa kuna hata makabila mengine nao wana makampuni makubwa sana buti wachaga wao wamezariwa na ujasiriamli na Ujasiriamali wao si wa kutengeneza.
 
Tanzania ni vigumu kushindana duniani kwa biashara hizi rahisirahisi zinazo endeshwa na Watanzania.
Watanzania wengi hawapendi biashara za kuumiza kichwa wanataka biashara rahisirahisi na ambazo hata siku moja haziwezi kutufukisha popote.
Nitatoa mfano
1. Biashara ya Baa au grosary
2. Saluni
3. Daladala
4.Satationary
4. Duka la kuuza vitu rejareja na jumla
5. Biashara ya kuuza nafaka
6. Biashara ya kuuza magari
7. Biashara ya kuuza simu
8. Biashara ya kuuza nguo na viatu na vyombo mbalimbali
9. Hardware
- Kuuza chips
- Kuuza vipodozi
- Duka la dawa za binadamu
10. Nyumba za kupangisha na kazalika
HIZI NDO BIASHARA ZINAZO PENDWA NA WATANZANIA, NI NZURI SANA. BUT KWA HIZI BIASHARA HUWEZI SHINDANA KIMATAIFA HATA SIKU MOJA.

-HAMNA MWEKEZAJI KUTOKA NJE AMBAE ANAWEZA KUBALI KUJA MUINGIE UBIA WA KUFANYA BIASHARA NILIZO OROZESHA HAPO JUU.

-HIZO HAPO JUU NDO BIASHARA ZA WABONGO HAZIHITAJI AKILI, BIASHARA AMBAZO UNAANZISHA ASUBUHI JIONI UNAFAIDA TIYALI.
- ILA KIMATAIFA HATA TAASISI KAMA BENK YA DUNIA KWENYE KITENGO CHA MIKOPO HAWAWEZI HATA SIKU OJA KUKUPATIA MKOPO KWA BIASHARA HIZO HAPO JUU LABDA KIDOGO NYUMBA ZA KUPANGA MEANS REAL ESTATE.
-BIASHARA ZA KUHITAJI AKILI NYINGI
- BIASHARA ZA CONSULTANCY
- UWEKEZAJI KATIKA KILIMO
- UFUGAJI WA AINA ZOTE
- MAHOTELI NA MIGAHAWA
- UTARII
- UJENZI
- NISHATI YA JUA, UPEPO NA KAZALIKA
- VIWANDA VIDOGOVIDOGO NA VYA KATI
- MADINI
- TEKINOLOJIA YA MAWASILIANO, -
SIMAANISHI KUUZA SIMU
HIZI BIASHARA ZINAHITAJI AKILI SANA NA NI BIASHARA AMBAZO ZINAWEZA KAMA ZIKIKUA KUSHINDANA KIMATAIFA, HIZI KUPATA WAWEKEZAJI WA KUINGIA NAO UBIA NI RAHISI SANA
Sita nikubali wala kupingana nawe... nachofahamu hata mbuyu unaanza kama mchicha... biashra ni biashara tu.. tofauti ni ubunifu na uboreshaji.
 
mkuu

biashara ni general term inategemea lengo na uwezo kibiashara

biashara ina zaa = Manufacturing/production (goods/services) ===== wholesale /distribution ===== retail/final sales ===== after sales services , zote hizi ni biashara


labda tupate uchambuzi kwamba watanzania tunazembea part gani ya kibiashara hapo juu
 
Mtoa changamoto, I doubt if you're an enteroreneur or you've even tried here. Ni ngumu kuanzisha biashara bila mtaji. Na mtaji ninaousema hapa ni ule endelevu.
Naichukia TRA na ndo maana nakwepa vikodi vyao.
Eti wanataka kodi kwenye mkopo au ruzuku.
 
Sita nikubali wala kupingana nawe... nachofahamu hata mbuyu unaanza kama mchicha... biashra ni biashara tu.. tofauti ni ubunifu na uboreshaji.

Sawa Mbuyu Ulianza kama mchicha but lazima kwenye biashara ufocas mbali sana, Hebu niambie Unaanzisha biashara ya kuuza nguo za mitumba je unafocas nini miaka kazaa ijayo?

Tanzania kuna Business Man wengi sana but kuna Wajasiriamali wachache sana.
 
tatizo watu wengi hili neno ujasiriamali
hawalielewi

ndo maana utakuta mama ntilie nao wakiitwa wajasiriamali.....
na wamachinga nao wajasiriamali ,funny ...
 
Mtoa changamoto, I doubt if you're an enteroreneur or you've even tried here. Ni ngumu kuanzisha biashara bila mtaji. Na mtaji ninaousema hapa ni ule endelevu.
Naichukia TRA na ndo maana nakwepa vikodi vyao.
Eti wanataka kodi kwenye mkopo au ruzuku.

Hapa Duniani kuna Wafanya biashara na Wajasiriamali Kwa Tanzania kuna Wafanya biashara wengi sana na wajasiriamali wachache sana. Huwezi anzisha saruni ya kunyoa nywele ukajiita mjasiriamali au kuanzisha duka la kuuza dawa ukajiita mjasiriamali au ukaanzisha baa ukajiita mjasiriamali no.

Hao wote ni wafanya biashara. Mjasiriamali ni ambae anaanzisha somothing new, ni mgunduzi wa kitu fulani kipya. Huwezi anzisha kitu ambacho kisha anzishwa na watu wengine ukajiita mjasiriamali.

Kuhusu kuanzisha biashara bila capital nataka nikuambie inawezekana narudia kusema kwamba Ukiwa mjasiriamali kuna uwezekano wa kuanzisha biashara bila capita.


Your idea is the primary capital. Ukiwa na Idea nzuri sana nina uhakika unaweza kuuza Idea yako. Imegine unataka kuanza biashara ya kuuza magari chakavu hiyo siyo aidia hata siku moja.


Kihusu Kodi mimi nazani kwamba ni uoga tu, Bila kulipa kodi huwezi kufanya biashara kimataifa hata kuchukua mkopo benki ni ngumu sana.
 
tatizo watu wengi hili neno ujasiriamali
hawalielewi

ndo maana utakuta mama ntilie nao wakiitwa wajasiriamali.....
na wamachinga nao wajasiriamali ,funny ...

Ni kweli kabisa Watu wnazania kila anaye fanya biashara basi huyo ni mjasiriamali. Huwezi kuuza simu za kichina au kutembeza redio za kichina mtaani ukajiita mjasiriamali.

WAJASIRIAMALI WOTE NI WAFANYA BIASHARA BUT C WAFANYA BIASHARA WOTE NI WAJASIRIAMALI
 
Sawa Mbuyu Ulianza kama mchicha but lazima kwenye biashara ufocas mbali sana, Hebu niambie Unaanzisha biashara ya kuuza nguo za mitumba je unafocas nini miaka kazaa ijayo?

Tanzania kuna Business Man wengi sana but kuna Wajasiriamali wachache sana.

Mkuu nadhani hujanisoma... ni wachache sana walionza na biashara kubwa ka usemavyo... Nnachofahamu unaweza kuanza na biashara ndogo naikakuwezesha kufanya biashara kubwa na hatimaye kuwekeza.. nawafahamu watu walionza kwa kuuza ufuta magengeni na leo ni na wafanya biashara waliofanikiwa... Ni UBUNIFU na UJASIRI tu ndo mihimili katika biashara..
 
ni kweli kabisa watu wnazania kila anaye fanya biashara basi huyo ni mjasiriamali. Huwezi kuuza simu za kichina au kutembeza redio za kichina mtaani ukajiita mjasiriamali.

Wajasiriamali wote ni wafanya biashara but c wafanya biashara wote ni wajasiriamali

tatizo linaanzia na serikali
wao ndo wa kwanza kuwaita wachuuzi ,wajasiriamali
na taasisi pia zenye kutafuta misaada nje,
utasikia tuna wajasiriamali 300,
ukienda chunguza unakuta wajasiriamali hawafiki watano.
Mfano sido....
Ubabaishaji mtupu...
 
mkuu nadhani hujanisoma... Ni wachache sana walionza na biashara kubwa ka usemavyo... Nnachofahamu unaweza kuanza na biashara ndogo naikakuwezesha kufanya biashara kubwa na hatimaye kuwekeza.. Nawafahamu watu walionza kwa kuuza ufuta magengeni na leo ni na wafanya biashara waliofanikiwa... Ni ubunifu na ujasiri tu ndo mihimili katika biashara..

ni sawa kabisa but watanzania hawafocus, huwezi andaa project proposal ya kuuza chips halafu kwenye proposal unaandika kwamba nitauza chips but mimi natageti kuuza magari baadae.

Kama umeamua kuuza chips uza chips na tafuta ubunifu mbalambali katika kuuza chips.
Wabongo leo utakuta analima na anamashamba makubwa tu but akisha pata hela ataishia kwenda kununu basi, wala hana mpango wa kuendeleza kilimo chake ili kiwe cha kisasa zaidi.
 
tatizo linaanzia na serikali
wao ndo wa kwanza kuwaita wachuuzi ,wajasiriamali
na taasisi pia zenye kutafuta misaada nje,
utasikia tuna wajasiriamali 300,
ukienda chunguza unakuta wajasiriamali hawafiki watano.
Mfano sido....
Ubabaishaji mtupu...

True, Tatizo Hii dhana ya Ujasiriamali ni ngeni sana kwetu. Ujasiriamali ulikuwa sana kwenye nchi za Kibepari Huku kwenye Ujamaa kulikuwa hakuna kitu kama hicho.
 
unakuta mwanamke
ambae ni mama wa nyumbani
anaishi kwa kumtegemea mumewe
anaanzisha kibiashara kisicho na faida
utasikia na yeye ni mjasiriamali...
hata tra hawamjui
 
unakuta mwanamke
ambae ni mama wa nyumbani
anaishi kwa kumtegemea mumewe
anaanzisha kibiashara kisicho na faida
utasikia na yeye ni mjasiriamali...
hata tra hawamjui

C tatizo lao ni tatizo la uelewa.
Watanzania wao wanafahamu kwamba ukisha kuwa na kibanda au duka basi wewe ni mjasiriamali.
 
Back
Top Bottom