MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 32,408
- 50,809
Mara nyingi mnajipiga vifua mkisema tufungiane mipaka, kwamba hamtuhitaji kwa lolote wala chochote, ilhali data zinaonyesha Kenya ndio baba likija kwenye suala la masoko ya bidhaa zenu ukanda huu, yaani hata ujumuishe Uganda, Burundi, Rwanda bado hawafikii thamani ya manunuzi yetu kutoka kwenu.
Pia uhamiaji wakiwapa data ya idadi ya Watanzania wanaovuka mpaka wakija Kenya, mtashangaa sana.
Hivyo endeleeni kutamani kulianzisha na Kenya mkidhani sisi ndio tutaumia pekee yetu, ila kilio kitasikika kote huko, mtakula hiyo pamba wenyewe....hehehe
--------------------
THAMANI ya mauzo ya Tanzania katika Soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi (pichani) alisema hayo jana wakati wa hotuba yake ya Mpango wa Makadirio ya Bajeti ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2018 mauzo yaliongezeka kufikia Dola za Marekani milioni 448.5 kutoka Dola za Marekani milioni 312.5 mwaka 2017 sawa na ongezeko la asilimia 43.6 Waziri Kabudi alisema mauzo kwenda Kenya yalikuwa ni asilimia 47.7 wakati mauzo kwenda Uganda yalikuwa ni asilimia 23.4 ikifuatiwa na Rwanda asilimia 17.8 na kuwa bidhaa zilizouzwa kwa wingi ni pamoja na mahindi, karatasi, viuatilifu, saruji, marumaru, konyagi, ngano na mafuta ya kupaka.
Alisema thamani ya ununuzi wa bidhaa kutoka nchi wanachama wa jumuiya ilipanda kwa asilimia 27.7 kutoka Dola za Marekani milioni 237.0 mwaka 2017 hadi kufikia Dola milioni 302.7 mwaka 2018 na kuongeza kuwa bidhaa zilizonunuliwa kutoka Kenya zilikuwa ni asilimia 81.75 wakati asilimia 17.40 zilinunuliwa kutoka Uganda.
Kwa mujibu wa Waziri Kabudi, soko kubwa la biashara za Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Kenya ikifuatiwa na Uganda na kuwa wizara imeratibu utekelezaji wa Himaya Moja ya Forodha ya Afrika Mashariki ambayo ni sehemu ya Umoja wa Forodha.
Pia uhamiaji wakiwapa data ya idadi ya Watanzania wanaovuka mpaka wakija Kenya, mtashangaa sana.
Hivyo endeleeni kutamani kulianzisha na Kenya mkidhani sisi ndio tutaumia pekee yetu, ila kilio kitasikika kote huko, mtakula hiyo pamba wenyewe....hehehe
--------------------
THAMANI ya mauzo ya Tanzania katika Soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi (pichani) alisema hayo jana wakati wa hotuba yake ya Mpango wa Makadirio ya Bajeti ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2018 mauzo yaliongezeka kufikia Dola za Marekani milioni 448.5 kutoka Dola za Marekani milioni 312.5 mwaka 2017 sawa na ongezeko la asilimia 43.6 Waziri Kabudi alisema mauzo kwenda Kenya yalikuwa ni asilimia 47.7 wakati mauzo kwenda Uganda yalikuwa ni asilimia 23.4 ikifuatiwa na Rwanda asilimia 17.8 na kuwa bidhaa zilizouzwa kwa wingi ni pamoja na mahindi, karatasi, viuatilifu, saruji, marumaru, konyagi, ngano na mafuta ya kupaka.
Alisema thamani ya ununuzi wa bidhaa kutoka nchi wanachama wa jumuiya ilipanda kwa asilimia 27.7 kutoka Dola za Marekani milioni 237.0 mwaka 2017 hadi kufikia Dola milioni 302.7 mwaka 2018 na kuongeza kuwa bidhaa zilizonunuliwa kutoka Kenya zilikuwa ni asilimia 81.75 wakati asilimia 17.40 zilinunuliwa kutoka Uganda.
Kwa mujibu wa Waziri Kabudi, soko kubwa la biashara za Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni Kenya ikifuatiwa na Uganda na kuwa wizara imeratibu utekelezaji wa Himaya Moja ya Forodha ya Afrika Mashariki ambayo ni sehemu ya Umoja wa Forodha.