Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Hii tabia ya kuzuzuka na kusheherekea pale Mtanzania hasa mwanasiasa akijua kuongea Kingereza hata kwa kunyoosha sentesi mbili tu imepitwa na wakati na ni ushamba.
Pia wanasiasa wasiojua Kingereza ni vyema wakatumia Kiswahili tu, hakuna aibu kutumia lugha yako unayoimudu vizuri, hakuna haja ya kulazimisha lugha usiyoimudu vizuri.
Pia tabia ya kusherehekea na kushangaa mtu asiye Mtanzania anapozungumza Kiswahili kilichonyooka ni ushamba uliopitwa na wakati.
Kiswahili kimekuwa lugha kubwa sana, kinazungumzwa na raia wengi wa nchi zilizotuzunguka kama lugha yao na pia kwa sababu ya kuongezeka kwa muingiliano wa watu.
Pia watu wengi duniani hata nchi za mbali wanajifunza Kiswahili katika vyuo na wanaongea Kiswahili vizuri tu kabisa.
Tuache kuwa kama tuko kwenye chungu.
Pia wanasiasa wasiojua Kingereza ni vyema wakatumia Kiswahili tu, hakuna aibu kutumia lugha yako unayoimudu vizuri, hakuna haja ya kulazimisha lugha usiyoimudu vizuri.
Pia tabia ya kusherehekea na kushangaa mtu asiye Mtanzania anapozungumza Kiswahili kilichonyooka ni ushamba uliopitwa na wakati.
Kiswahili kimekuwa lugha kubwa sana, kinazungumzwa na raia wengi wa nchi zilizotuzunguka kama lugha yao na pia kwa sababu ya kuongezeka kwa muingiliano wa watu.
Pia watu wengi duniani hata nchi za mbali wanajifunza Kiswahili katika vyuo na wanaongea Kiswahili vizuri tu kabisa.
Tuache kuwa kama tuko kwenye chungu.