Watanzania kwenye Mpira(AFCON 2019): Matumaini makubwa mno kabla ya mechi na Lawama kubwa mno baada ya mechi.

Watanzania kwenye Mpira(AFCON 2019): Matumaini makubwa mno kabla ya mechi na Lawama kubwa mno baada ya mechi.

mr mkiki

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
5,588
Reaction score
11,668
Tumekuwa na matatizo haya kwenye mambo mengi sana sijajua ni tabia za kikoloni au la lakini ni lazima tujue kuwa mpira sio mchezo wa miujiza sana

Mpaka Senegal wamekuwa hivi walitumia miaka zaidi ya ishirini kutengeneza timu yao, sisi hatujui hilo tunawaza miujiza tu.

Tunazania kama Senegal kuwafunga France kipindi kile ulikuwa miujiza, hapana wenzetu walitengeneza timu yao

Tuache kuzani mpira ni miujiza watanzania tutengeneze timu, miujiza itakuja baada ya hapo. Yani tunaenda tofauti hata na vitabu vya dini.

Kwangu hakuna hata mchezaji moja mwenye uwezo wakucheza mpira kusaidia timu yetu kwa sasa.

Lazima tujue uzoefu wetu upo vipi katika mechi kubwa kama hizi, Yani tunawapa lawama wachezaji wetu kwa kutaka kufikia matumaini yetu timu ni mbovu lazima tulijue hilo.

Yani tumekaa tukimuomba Mungu awe shabiki wetu tukifikiri wasenegal hawamjui Mungu au.

Tuache tabia za ajabu.

Wenzetu wamejianda kupambana na pia hata kisaikolojia wapo vizuri kama itaitajika.






IMG-20190623-WA0018.jpeg
IMG_20190623_223833.jpeg
IMG_20190623_113547.jpeg


mr mkiki
 
Kama huyo mzungu amemkubali huyo jamaa basi na mimi nitapata mwanamke mzuri tu
 
Niliangalia mechi lakini sikuwaona mashabiki waliovaa 'vazi rasmi la ushangiliaji' lililozinduliwa kwa heshima na taadhima!
 
Niliangalia mechi lakini sikuwaona mashabiki waliovaa 'vazi rasmi la ushangiliaji' lililozinduliwa kwa heshima na taadhima!
Watanzania wanamatatizo sana
 
Tunaanzia kwenye vilabu vyetu vya simba na Yanga. Mambo yale yale tunayapeleka stars! Tunadhani kuna ushindi wa kirahisi rahisi tuuu! Angalia physique ya wachezaji wa Senegal na wetu yaani tofauti, wenzetu timu nzima ni professionals wanacheza ulaya. Tushangilie tu kufuzu mashindanoni lkn sidhani kama tutashinda hata mechi moja. Tuanze na vijana wetu sio hawa ambao hawana background ya mpira. Ukimuuliza mchezaji miaka mitano iliyopita alikuwa wapi atakwambia sikuwa na wazo kabsaa la mpira wakati wenzetu wanaanza na miaka 10 kwenye academies. Kuwa na Samatta pekee hatuwezi fanya lolote. Ni Sawa na Kenya kuwa na Yule jamaa wa spurs kusivowasaidia katika hii grand stage. Mechi yetu na Algeria sijui itakuwaje
 
Tunaanzia kwenye vilabu vyetu vya simba na Yanga. Mambo yale yale tunayapeleka stars! Tunadhani kuna ushindi wa kirahisi rahisi tuuu! Angalia physique ya wachezaji wa Senegal na wetu yaani tofauti, wenzetu timu nzima ni professionals wanacheza ulaya. Tushangilie tu kufuzu mashindanoni lkn sidhani kama tutashinda hata mechi moja. Tuanze na vijana wetu sio hawa ambao hawana background ya mpira. Ukimuuliza mchezaji miaka mitano iliyopita alikuwa wapi atakwambia sikuwa na wazo kabsaa la mpira wakati wenzetu wanaanza na miaka 10 kwenye academies. Kuwa na Samatta pekee hatuwezi fanya lolote. Ni Sawa na Kenya kuwa na Yule jamaa wa spurs kusivowasaidia katika hii grand stage. Mechi yetu na Algeria sijui itakuwaje
Nazani Kuna vitu tunapaswa tujue
 
Back
Top Bottom